< Ezekieli 36 >

1 “Mwanadamu, itabirie milima ya Israeli na useme, ‘Ee milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana.
Also, thou son of man, prophesy to the mountains of Israel, and say: Ye mountains of Israel, hear the word of Jehovah.
2 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu adui wanasema juu yako, “Aha! Mahali palipoinuka pa zamani pamekuwa milki yetu.”’
Thus saith the Lord Jehovah: Because the enemy hath said concerning you, “Aha! the everlasting heights have become our possession”;
3 Kwa hiyo tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu wamewafanya ukiwa na kuwagandamiza kila upande ili mpate kuwa milki ya mataifa mengine na kuwa kitu cha kusimangwa na kudhihakiwa miongoni mwa watu,
therefore prophesy and say, Thus saith the Lord Jehovah: Because, yea, because they have made you desolate, and swallowed you up on every side, so that ye have become a possession to the residue of the nations, and a subject for the lips of talkers, and a derision to the people;
4 kwa hiyo, ee milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana Mwenyezi: Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa milima na vilima, kwa makorongo na mabonde, kwa mahame yaliyo ukiwa, miji iliyoachwa ambayo imetekwa nyara na kudharauliwa na mataifa mengine yanayowazunguka,
therefore, ye mountains of Israel, hear the word of the Lord Jehovah. Thus saith the Lord Jehovah, to the mountains and the hills, the valleys and the plain, to the desolate wastes and to the forsaken cities, which are become a prey and a derision to the residue of the nations which are round about, —
5 hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika wivu wangu uwakao nimenena dhidi ya mataifa mengine na dhidi ya Edomu yote, kwa maana kwa furaha na hila katika mioyo yao waliifanya nchi yangu kuwa milki yao ili wapate kuteka nyara sehemu yake ya malisho.’
therefore thus saith the Lord Jehovah: Surely in the fire of my jealousy have I spoken against the residue of the nations, and against all Edom, who have allotted my land to themselves for a possession, with joy of their whole heart, and with a despiteful mind, to cast it out for a prey.
6 Kwa hiyo tabiri kuhusu nchi ya Israeli na uiambie milima na vilima, makorongo na vijito na mabonde: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninanena katika wivu wa ghadhabu yangu kwa sababu mmedharauliwa na mataifa.
Prophesy, therefore, concerning the land of Israel, and say to the mountains and to the hills, to the valleys and the plains, Thus saith the Lord Jehovah: Behold, I have spoken in my jealousy and in my fury, because ye have borne the reproach of the nations.
7 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninaapa kwa mkono wangu ulioinuliwa kwamba mataifa wanaowazunguka nao pia watadharauliwa.
Therefore thus saith the Lord Jehovah: I have lifted up my hand, that the nations that are round about you, that they shall bear their reproach.
8 “‘Lakini ninyi, ee milima ya Israeli, mtatoa matawi na matunda kwa ajili ya watu wangu Israeli, kwa sababu hivi karibuni watakuja nyumbani.
But ye, O mountains of Israel, shall shoot forth your branches, and bear your fruit for my people Israel; for they are near coming.
9 Mimi ninawajibika nanyi na nitawaangalia kwa upendeleo, mtalimwa na kupandwa mbegu,
For behold, I am for you, and I will turn to you, and ye shall be tilled and sown;
10 nami nitaizidisha idadi ya watu kwenu, naam, nyumba yote ya Israeli. Miji itakaliwa na watu na magofu yatajengwa upya.
and I will multiply men upon you, even all the house of Israel, all of it; and the cities shall be inhabited, and the waste places shall be built.
11 Nitaongeza idadi ya watu na wanyama juu yenu, nao watazaana sana na kuwa wengi mno. Nitawakalisha watu ndani yenu kama ilivyokuwa wakati uliopita, nami nitawafanya mfanikiwe kuliko hapo kwanza. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
I will multiply men upon you, and beasts; and they shall increase and be fruitful; and I will cause you to be inhabited as of old, and will do better to you than in the ancient time; and ye shall know that I am Jehovah.
12 Nitawafanya watu, watu wangu Israeli, kutembea juu yenu. Watawamiliki ninyi, nanyi mtakuwa urithi wao, kamwe hamtawaondolea tena watoto wao.
Yea, I will cause men, even my people Israel, to walk upon you, and they shall possess thee, and thou shalt be their inheritance, and thou shalt no more henceforth bereave them of children.
13 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu watu wanakuambia, “Unawala watu na kuliondolea taifa lako watoto wake,”
Thus saith the Lord Jehovah: Because they say of you, “Thou hast devoured men, and made thy people childless!”
14 kwa hiyo hutakula tena watu wala kulifanya tena taifa lako lisiwe na watoto, asema Bwana Mwenyezi.
therefore thou shalt devour men no more, and no more make thy people childless, saith the Lord Jehovah.
15 Sitakufanya tena usikie dhihaka za mataifa, wala kudharauliwa na kabila za watu, wala kulifanya taifa lako lianguke, asema Bwana Mwenyezi.’”
Neither will I cause the reproach of the nations to be heard against thee any more, neither shalt thou bear the derision of the nations any more, neither shalt thou make thy nation childless any more, saith the lord Jehovah.
16 Neno la Bwana likanijia tena, kusema:
Moreover, the word of Jehovah came to me, saying:
17 “Mwanadamu, nyumba ya Israeli walipokuwa wakiishi katika nchi yao wenyewe, waliinajisi kwa mwenendo wao na matendo yao. Mwenendo wao mbele zangu ulikuwa kama mwanamke aliye katika hedhi.
Son of man, when the house of Israel dwelt in their own land, they defiled it by their way and by their doings; their way before me was as the impurity of an unclean woman.
18 Hivyo nilimwaga ghadhabu yangu juu yao kwa sababu walikuwa wamemwaga damu katika nchi na kwa sababu walikuwa wameitia nchi unajisi kwa sanamu zao.
Wherefore I poured my fury upon them for the blood which they had shed in the land, and because they had polluted it with their idols.
19 Nikawatawanya miongoni mwa mataifa, nao wakaenda huku na huko katika nchi mbalimbali, nikawahukumu sawasawa na mwenendo wao na matendo yao.
And I scattered them among the nations, and they were dispersed through the countries; according to their way and according to their doings I judged them.
20 Tena popote walipokwenda miongoni mwa mataifa walilitia unajisi Jina langu takatifu, kwa kuwa watu walisema kuwahusu, ‘Hawa ndio watu wa Bwana, lakini imewapasa kuondoka katika nchi yake.’
And when they came to the nations whither they went, they polluted my holy name, in that it was said of them, “These are the people of Jehovah, and they are gone forth out of his land.”
21 Lakini niliwahurumia kwa ajili ya Jina langu takatifu, ambalo nyumba ya Israeli imelitia unajisi miongoni mwa mataifa huko walikokwenda.
Therefore I will have regard to my holy name, which the house of Israel have polluted among the nations whither they are gone.
22 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Si kwa ajili yako, ee nyumba ya Israeli, kwamba ninafanya mambo haya, bali ni kwa ajili ya Jina langu takatifu, ambalo mmelitia unajisi miongoni mwa mataifa mliyoyaendea.
Therefore say to the house of Israel, Thus saith the Lord Jehovah: Not for your own sakes do I this, O house of Israel, but for my holy name, which ye have polluted among the nations whither ye are gone.
23 Nitauonyesha utakatifu wa Jina langu kuu, ambalo limetiwa unajisi miongoni mwa mataifa, jina ambalo limetiwa unajisi miongoni mwao. Ndipo mataifa watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana, asema Bwana Mwenyezi, nitakapojionyesha mwenyewe kuwa mtakatifu kwa kuwapitia ninyi mbele ya macho yao.
And I will sanctify my great name, which hath been polluted among the nations, which ye have profaned in the midst of them; and the nations shall know that I am Jehovah, when I shall be sanctified in regard to you, before their eyes, saith the Lord Jehovah.
24 “‘Kwa kuwa nitawaondoa ninyi toka mataifa, nitawakusanya kutoka nchi zote na kuwarudisha kwenye nchi yenu wenyewe.
For I will take you from among the nations, and gather you out of all countries, and bring you into your own land.
25 Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi, nitawatakasa kutoka uchafu wenu wote na kutoka sanamu zenu zote.
Then will I sprinkle clean water upon you, and ye shall be clean. From all your uncleanness and from all your idols will I cleanse you.
26 Nitawapa moyo mpya na kuweka roho mpya ndani yenu, nitaondoa ndani yenu moyo wenu wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
A new heart also will I give you, and a new spirit will I put within you; and I will take out of your body the heart of stone, and I will give you a heart of flesh.
27 Nami nitaweka Roho yangu ndani yenu na kuwafanya ninyi mfuate amri zangu na kuwafanya kuwa waangalifu kuzishika sheria zangu.
And I will put my spirit within you, and cause you to walk in my statutes, and ye shall keep my commandments and do them.
28 Mtaishi katika nchi niliyowapa baba zenu, ninyi mtakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu.
And ye shall dwell in the land which I gave to your fathers, and ye shall be my people, and I will be your God.
29 Nitawaokoa ninyi kutoka unajisi wenu wote. Nitaiita nafaka na kuiongeza iwe nyingi sana nami sitaleta njaa juu yenu.
And I will save you from all your uncleanness. And I will call for the corn, and will increase it, and bring no famine upon you.
30 Nitaongeza matunda ya miti na mazao ya mashamba, ili kwamba msipate tena aibu miongoni mwa mataifa kwa ajili ya njaa.
And I will multiply the fruit of the tree, and the increase of the field, that ye may receive no more the reproach of famine among the nations.
31 Ndipo mtakapozikumbuka njia zenu za uovu na matendo yenu maovu, nanyi mtajichukia wenyewe kwa ajili ya dhambi zote na matendo yenu ya kuchukiza.
Then shall ye remember your evil ways, and your doings which were not good, and ye shall loathe yourselves for your iniquities, and for your abominations.
32 Ninataka ninyi mjue kwamba sifanyi hili kwa ajili yenu, asema Bwana Mwenyezi. Oneni aibu na mkatahayari kwa ajili ya mwenendo wenu, ee nyumba ya Israeli!
Not for your own sakes do I this, saith the Lord Jehovah, be it known to you. Be ye ashamed and confounded for your ways, O house of Israel!
33 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Siku ile nitakapowasafisha kutoka dhambi zenu zote, nitarudisha watu waishi katika miji yenu na magofu yatajengwa upya.
Thus saith the Lord Jehovah: In the day when I shall cleanse you from all your iniquities, then will I cause the cities to be inhabited, and the waste places to be rebuilt;
34 Nchi iliyokuwa ukiwa italimwa badala ya kukaa ukiwa machoni mwa wale wote wanaopita ndani yake.
and the desolate land shall be tilled, whereas it lay desolate in the sight of all that passed by.
35 Watasema, “Hii nchi iliyokuwa imeachwa ukiwa sasa imekuwa kama bustani ya Edeni, miji ile iliyokuwa magofu, ukiwa na kuangamizwa, sasa imejengewa ngome na kukaliwa na watu.”
Then shall it be said, “This land, that was desolate, is become as the garden of Eden; and the waste and desolate and ruined cities are become fenced, and are inhabited.”
36 Ndipo mataifa yanayowazunguka yaliyobakia watakapojua kuwa Mimi Bwana nimejenga tena kile kilichoharibiwa na nimepanda tena kile kilichokuwa ukiwa. Mimi Bwana nimenena, nami nitalifanya.’
Then the nations that are left around you shall know that I, Jehovah, have built that which was ruined, and planted that which was desolate. I, Jehovah, have spoken it, and I will do it.
37 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mara nyingine tena nitasikia maombi ya nyumba ya Israeli na kuwatendea jambo hili: Nitawafanya watu wake kuwa wengi kama kondoo,
Thus saith the Lord Jehovah: Yet will I listen to the house of Israel, and do this for them. I will increase
38 kuwa wengi kama kundi la kondoo kwa ajili ya dhabihu huko Yerusalemu wakati wa sikukuu zao za wakati ulioamriwa. Hivyo ndivyo miji iliyokuwa magofu itajazwa na makundi ya watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
them with men like a flock; as the holy flock, as the flock of Jerusalem in her solemn feasts; so shall the waste cities be filled with flocks of men; and they shall know that I am Jehovah.

< Ezekieli 36 >