< Ezekieli 35 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
Und das Wort Jehovahs geschah an mich, sprechend:
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya mlima Seiri, utabiri dhidi yake
Menschensohn, richte dein Angesicht wider den Berg Seir und weissage dawider!
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume nawe, ee mlima Seiri, nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya ukiwa na usiyekaliwa na watu wala kulimika.
Und sprich zu ihm: So spricht der Herr Jehovah: Siehe, Ich bin wider dich, Berg Seir, und strecke Meine Hand aus wider dich und mache dich zur Verwüstung und Wüstenei.
4 Nitaifanya miji yako kuwa magofu nawe utakuwa ukiwa. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Zur Öde will Ich deine Städte machen, und zur Verwüstung sollst du werden, und du sollst wissen, daß Ich Jehovah bin.
5 “‘Kwa sababu ulificha moyoni uadui wa siku nyingi nawe ukawatoa Waisraeli wauawe kwa upanga wakati wa maafa yao, wakati adhabu yake ilipofikia kilele chake,
Darum, daß du ewige Feindschaft hast und Israels Söhne in die Hände des Schwertes hingabst zur Zeit ihrer Not, zur Zeit des Endes der Missetat.
6 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutia katika umwagaji damu nao utakufuatia. Kwa kuwa hakuchukia kumwaga damu, kumwaga damu kutakufuatia.
Darum, bei Meinem Leben, spricht der Herr Jehovah, mache Ich dich zu Blut, und Blut soll dich verfolgen; da du Blut nicht haß-test, soll dich Blut verfolgen.
7 Nitaufanya Mlima Seiri ukiwa na usiokaliwa na watu wala kulimika na kuukatilia mbali na wote wanaokuja na wanaokwenda.
Darum mache Ich den Berg Seir zur Verwüstung und Wüstenei und rotte aus von ihm, der darüber hingeht und zurückkehrt.
8 Nitaijaza milima yenu kwa watu wake waliouawa, wale waliouawa kwa upanga wataanguka juu ya vilima vyako na katika mabonde yako na katika makorongo yako yote.
Und seine Berge fülle Ich mit seinen Erschlagenen; deine Hügel und deine Schluchten und all deine Flußbette - vom Schwert Erschlagene sollen allda fallen!
9 Nitakufanya ukiwa milele, watu hawataishi katika miji yako. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Zur ewigen Verwüstung mache Ich dich, und deine Städte sollen nicht bewohnt werden, und ihr sollt wissen, daß Ich Jehovah bin.
10 “‘Kwa sababu umesema, “Mataifa haya mawili na nchi hizi zitakuwa zetu nasi tutazimiliki,” ingawa hata mimi Bwana nilikuwa huko,
Weil du gesprochen hast: Die zwei Völkerschaften und die zwei Länder sollen mein sein, und wir werden sie erblich besitzen; und Jehovah ist dort,
11 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutenda kwa kadiri ya hasira na wivu uliouonyesha katika chuki yako juu yao nami nitafanya nijulikane miongoni mwao wakati nitakapokuhukumu.
Darum, bei Meinem Leben, spricht der Herr Jehovah, so tue Ich nach deinem Zorn und nach deiner Eifersucht, wie du aus deinem Haß wider sie hast getan, und tue Mich kund an ihnen, wenn Ich dich richte,
12 Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesikia mambo yote ya dharau uliyosema dhidi ya milima ya Israeli. Ulisema, “Wamefanyika ukiwa na kutiwa mikononi mwetu tuwararue.”
Und du sollst wissen, daß Ich, Jehovah, hörte all deine Lästerungen, die du wider die Berge Israels gesprochen hast, sprechend: Sie sind verwüstet, sind zur Speise uns gegeben.
13 Ulijigamba dhidi yangu na kusema maneno dhidi yangu bila kujizuia, nami nikayasikia.
Und ihr tatet groß wider Mich mit eurem Munde, und eure Worte wider Mich habt ihr gehäuft. Ich hörte es.
14 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati dunia yote inashangilia nitakufanya ukiwa.
So spricht der Herr Jehovah: Während fröhlich ist die ganze Erde, mache Ich zur Verwüstung dich.
15 Kwa sababu ulishangilia wakati urithi wa nyumba ya Israeli ulipofanyika ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea. Utakuwa ukiwa, ee mlima Seiri, wewe na Edomu yote. Kisha ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
Wie du fröhlich warst über das Erbe des Hauses Israel, daß es verwüstet ward, also werde Ich tun an dir. Zur Verwüstung sollst du werden, der Berg Seir und ganz Edom zumal, und sie sollen wissen, daß Ich Jehovah bin.