< Ezekieli 35 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de Yahweh me fut adressée en ces termes:
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya mlima Seiri, utabiri dhidi yake
" Fils de l'homme, tourne ta face vers la montagne de Séir et prophétise contre elle, et dis-lui:
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume nawe, ee mlima Seiri, nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya ukiwa na usiyekaliwa na watu wala kulimika.
Ainsi parle le Seigneur Yahweh: Voici que je viens à toi, montagne de Séir, je vais étendre ma main sur toi, et faire de toi une solitude et un désert.
4 Nitaifanya miji yako kuwa magofu nawe utakuwa ukiwa. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Je réduirai tes villes en ruines, tu seras une solitude; et tu sauras que je suis Yahweh.
5 “‘Kwa sababu ulificha moyoni uadui wa siku nyingi nawe ukawatoa Waisraeli wauawe kwa upanga wakati wa maafa yao, wakati adhabu yake ilipofikia kilele chake,
Parce que tu as une haine éternelle et que tu as livré au glaive les enfants d'Israël, au temps de leur calamité, au temps de l'iniquité finale,
6 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutia katika umwagaji damu nao utakufuatia. Kwa kuwa hakuchukia kumwaga damu, kumwaga damu kutakufuatia.
à cause de cela, je suis vivant, — oracle du Seigneur Yahweh: Je te mettrai à sang, et le sang te poursuivra; parce que tu n'as pas haï le sang, le sang te poursuivra.
7 Nitaufanya Mlima Seiri ukiwa na usiokaliwa na watu wala kulimika na kuukatilia mbali na wote wanaokuja na wanaokwenda.
Et je ferai de la montagne de Séir une solitude et un désert, et j'en retrancherai tout allant et venant.
8 Nitaijaza milima yenu kwa watu wake waliouawa, wale waliouawa kwa upanga wataanguka juu ya vilima vyako na katika mabonde yako na katika makorongo yako yote.
Je remplirai ses monts de ses blessés à mort; sur tes collines, dans tes vallées et dans tous tes ravins tomberont les hommes égorgés par l'épée.
9 Nitakufanya ukiwa milele, watu hawataishi katika miji yako. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Je te réduirai en solitudes éternelles, et tes villes ne seront plus habitées; et vous saurez que je suis Yahweh.
10 “‘Kwa sababu umesema, “Mataifa haya mawili na nchi hizi zitakuwa zetu nasi tutazimiliki,” ingawa hata mimi Bwana nilikuwa huko,
Parce que tu as dit: " Les deux nations et les deux pays seront à moi, et nous en prendrons possession! " — et Yahweh était là! —
11 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutenda kwa kadiri ya hasira na wivu uliouonyesha katika chuki yako juu yao nami nitafanya nijulikane miongoni mwao wakati nitakapokuhukumu.
à cause de cela, je suis vivant, — oracle du Seigneur Yahweh: j'agirai selon ta colère, et selon ta jalousie, que tu as montrées dans ta haine contre eux, et je me ferai connaître au milieu d'eux quand je te jugerai.
12 Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesikia mambo yote ya dharau uliyosema dhidi ya milima ya Israeli. Ulisema, “Wamefanyika ukiwa na kutiwa mikononi mwetu tuwararue.”
Et tu sauras que moi, Yahweh, j'ai entendu tous tes outrages, que tu proférais contre les montagnes d'Israël, en disant: " Elles sont dévastées, elles nous sont données comme une proie à dévorer "
13 Ulijigamba dhidi yangu na kusema maneno dhidi yangu bila kujizuia, nami nikayasikia.
Vous m'avez bravé par vos discours; et vous avez multiplié vos paroles contre moi; moi, j'ai entendu!
14 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati dunia yote inashangilia nitakufanya ukiwa.
Ainsi parle le Seigneur Yahweh: Quand toute la terre se réjouira, je ferai de toi une solitude.
15 Kwa sababu ulishangilia wakati urithi wa nyumba ya Israeli ulipofanyika ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea. Utakuwa ukiwa, ee mlima Seiri, wewe na Edomu yote. Kisha ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
Comme tu t'es réjouie au sujet de l'héritage de la maison d'Israël parce qu'il était dévasté, je te ferai de même: tu seras dévastée, montagne de Séir, ainsi que l'Idumée tout entière. Et l'on saura que je suis Yahweh. "

< Ezekieli 35 >