< Ezekieli 35 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de Yahvé me fut adressée, en ces termes:
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya mlima Seiri, utabiri dhidi yake
Fils d'homme, tourne ta face vers la montagne de Séir, prophétise contre elle,
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume nawe, ee mlima Seiri, nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya ukiwa na usiyekaliwa na watu wala kulimika.
et dis-lui: « Le Seigneur Yahvé dit: « Voici, j'en veux à toi, montagne de Séir, et j'étendrai ma main contre toi. Je ferai de toi un objet de désolation et d'épouvante.
4 Nitaifanya miji yako kuwa magofu nawe utakuwa ukiwa. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Je dévasterai tes villes, et tu seras dévastée. Alors tu sauras que je suis Yahvé.
5 “‘Kwa sababu ulificha moyoni uadui wa siku nyingi nawe ukawatoa Waisraeli wauawe kwa upanga wakati wa maafa yao, wakati adhabu yake ilipofikia kilele chake,
"« Parce que tu as eu une hostilité perpétuelle, et que tu as livré les enfants d'Israël au pouvoir de l'épée au temps de leur calamité, au temps de l'iniquité de la fin,
6 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutia katika umwagaji damu nao utakufuatia. Kwa kuwa hakuchukia kumwaga damu, kumwaga damu kutakufuatia.
c'est pourquoi, je suis vivant, dit le Seigneur Yahvé, je te préparerai au sang, et le sang te poursuivra. Puisque vous n'avez pas haï le sang, c'est le sang qui vous poursuivra.
7 Nitaufanya Mlima Seiri ukiwa na usiokaliwa na watu wala kulimika na kuukatilia mbali na wote wanaokuja na wanaokwenda.
Ainsi, je ferai de la montagne de Séir un objet d'étonnement et de désolation. J'en retrancherai celui qui y passe et celui qui y retourne.
8 Nitaijaza milima yenu kwa watu wake waliouawa, wale waliouawa kwa upanga wataanguka juu ya vilima vyako na katika mabonde yako na katika makorongo yako yote.
Je remplirai ses montagnes de ses morts. Les morts par l'épée tomberont dans tes collines, dans tes vallées et dans tous tes cours d'eau.
9 Nitakufanya ukiwa milele, watu hawataishi katika miji yako. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Je ferai de toi une désolation perpétuelle, et tes villes ne seront pas habitées. Alors tu sauras que je suis Yahvé.
10 “‘Kwa sababu umesema, “Mataifa haya mawili na nchi hizi zitakuwa zetu nasi tutazimiliki,” ingawa hata mimi Bwana nilikuwa huko,
« Parce que vous avez dit: Ces deux nations et ces deux pays seront à moi, et nous en prendrons possession, alors que Yahvé était là,
11 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutenda kwa kadiri ya hasira na wivu uliouonyesha katika chuki yako juu yao nami nitafanya nijulikane miongoni mwao wakati nitakapokuhukumu.
c'est pourquoi, je suis vivant, dit le Seigneur Yahvé, j'agirai selon votre colère et selon la jalousie que vous avez manifestée par votre haine contre eux, et je me ferai connaître au milieu d'eux quand je vous jugerai.
12 Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesikia mambo yote ya dharau uliyosema dhidi ya milima ya Israeli. Ulisema, “Wamefanyika ukiwa na kutiwa mikononi mwetu tuwararue.”
Vous saurez que moi, Yahvé, j'ai entendu toutes les injures que vous avez proférées contre les montagnes d'Israël, en disant: « Elles ont été dévastées. On nous les a données à dévorer ».
13 Ulijigamba dhidi yangu na kusema maneno dhidi yangu bila kujizuia, nami nikayasikia.
Vous vous êtes glorifiés contre moi par votre bouche, et vous avez multiplié vos paroles contre moi. Je l'ai entendu. »
14 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati dunia yote inashangilia nitakufanya ukiwa.
Le Seigneur Yahvé dit: « Quand toute la terre se réjouira, je te réduirai en désolation.
15 Kwa sababu ulishangilia wakati urithi wa nyumba ya Israeli ulipofanyika ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea. Utakuwa ukiwa, ee mlima Seiri, wewe na Edomu yote. Kisha ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
Comme vous vous êtes réjouis de l'héritage de la maison d'Israël parce qu'il était dévasté, ainsi je vous traiterai. Tu seras dévasté, ainsi que la montagne de Séir et tout Édom, tout entier. Alors ils sauront que je suis Yahvé.'"

< Ezekieli 35 >