< Ezekieli 35 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya mlima Seiri, utabiri dhidi yake
O son of humankind set face your on [the] mountain of Seir and prophesy on it.
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume nawe, ee mlima Seiri, nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya ukiwa na usiyekaliwa na watu wala kulimika.
And you will say to it thus he says [the] Lord Yahweh here I [am] against you O mountain of Seir and I will stretch out hand my on you and I will make you a desolation and a waste.
4 Nitaifanya miji yako kuwa magofu nawe utakuwa ukiwa. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Cities your a ruin I will make and you a desolation you will be and you will know that I [am] Yahweh.
5 “‘Kwa sababu ulificha moyoni uadui wa siku nyingi nawe ukawatoa Waisraeli wauawe kwa upanga wakati wa maafa yao, wakati adhabu yake ilipofikia kilele chake,
Because belonged to you enmity of antiquity and you poured [the] people of Israel over [the] hands of [the] sword at [the] time of disaster their at a time of punishment of [the] end.
6 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutia katika umwagaji damu nao utakufuatia. Kwa kuwa hakuchukia kumwaga damu, kumwaga damu kutakufuatia.
Therefore [by] [the] life of me [the] utterance of [the] Lord Yahweh that to blood I will appoint you and blood it will pursue you if not blood you have hated and blood it will pursue you.
7 Nitaufanya Mlima Seiri ukiwa na usiokaliwa na watu wala kulimika na kuukatilia mbali na wote wanaokuja na wanaokwenda.
And I will make [the] mountain of Seir into a desolation and a desolation and I will cut off from it [one who] passes through and [one who] returns.
8 Nitaijaza milima yenu kwa watu wake waliouawa, wale waliouawa kwa upanga wataanguka juu ya vilima vyako na katika mabonde yako na katika makorongo yako yote.
And I will fill mountains its slain [ones] its hills your and valleys your and all ravines your [those] slain of a sword they will fall in them.
9 Nitakufanya ukiwa milele, watu hawataishi katika miji yako. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Desolations of perpetuity I will make you and cities your not (they will return *Q(K)*) and you will know that I [am] Yahweh.
10 “‘Kwa sababu umesema, “Mataifa haya mawili na nchi hizi zitakuwa zetu nasi tutazimiliki,” ingawa hata mimi Bwana nilikuwa huko,
Because saying you [the] two the nations and [the] two the lands to me they will belong and we will take possession of it and Yahweh there he was.
11 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutenda kwa kadiri ya hasira na wivu uliouonyesha katika chuki yako juu yao nami nitafanya nijulikane miongoni mwao wakati nitakapokuhukumu.
Therefore [by] [the] life of me [the] utterance of [the] Lord Yahweh and I will act according to anger your and according to jealousy your which you did from hatred your with them and I will make myself known among them when I will judge you.
12 Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesikia mambo yote ya dharau uliyosema dhidi ya milima ya Israeli. Ulisema, “Wamefanyika ukiwa na kutiwa mikononi mwetu tuwararue.”
And you will know that I Yahweh I have heard - all insults your which you have said on [the] mountains of Israel saying - (they have been desolated *Q(K)*) to us they have been given for devouring.
13 Ulijigamba dhidi yangu na kusema maneno dhidi yangu bila kujizuia, nami nikayasikia.
And you have magnified yourselves on me with mouth your and you have multiplied on me words your I I have heard.
14 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati dunia yote inashangilia nitakufanya ukiwa.
Thus he says [the] Lord Yahweh when rejoices all the earth desolation I will make for you.
15 Kwa sababu ulishangilia wakati urithi wa nyumba ya Israeli ulipofanyika ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea. Utakuwa ukiwa, ee mlima Seiri, wewe na Edomu yote. Kisha ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
According to rejoicing your to [the] inheritance of [the] house of Israel on that it had been desolated so I will do to you a desolation you will be O mountain of Seir and all Edom all of it and they will know that I [am] Yahweh.