< Ezekieli 35 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
And the word of Yahweh came unto me, saying,
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya mlima Seiri, utabiri dhidi yake
Son of man Set thy face against Mount Seir, —and prophesy against it;
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume nawe, ee mlima Seiri, nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya ukiwa na usiyekaliwa na watu wala kulimika.
and thou shalt say to it Thus saith My Lord Yahweh, Behold me! against thee Mount Seir, —Therefore will I stretch out my hand against thee, And I will make thee a desolation and an astonishment:
4 Nitaifanya miji yako kuwa magofu nawe utakuwa ukiwa. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Thy cities, will I lay waste, And thou—a desolation, shalt become, So shalt thou know that I, am Yahweh.
5 “‘Kwa sababu ulificha moyoni uadui wa siku nyingi nawe ukawatoa Waisraeli wauawe kwa upanga wakati wa maafa yao, wakati adhabu yake ilipofikia kilele chake,
Because thou hast had an age-abiding enmity, And hast delivered up the sons of Israel unto the hands of the sword, - In the time of their misfortune, In the time of the final punishment for iniquity,
6 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutia katika umwagaji damu nao utakufuatia. Kwa kuwa hakuchukia kumwaga damu, kumwaga damu kutakufuatia.
Therefore, as I live, Declareth My Lord Yahweh, Surely regarding blood, will I deal with thee, Blood therefore, shall pursue thee, -Since blood thou hast not hated, Therefore blood, shall pursue thee,
7 Nitaufanya Mlima Seiri ukiwa na usiokaliwa na watu wala kulimika na kuukatilia mbali na wote wanaokuja na wanaokwenda.
So then I will deliver up Mount Seir to desolation after desolation, - And will cut off therefrom him that passeth by and him that returneth,
8 Nitaijaza milima yenu kwa watu wake waliouawa, wale waliouawa kwa upanga wataanguka juu ya vilima vyako na katika mabonde yako na katika makorongo yako yote.
And I will fill his mountains with his slain, — As for thy hills and thy hollows and all thy channels, they who are thrust through by the sword shall fall therein:
9 Nitakufanya ukiwa milele, watu hawataishi katika miji yako. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Desolations age-abiding, will I make thee, And thy cities, shall not be inhabited, - So shall ye know that, I, am Yahweh.
10 “‘Kwa sababu umesema, “Mataifa haya mawili na nchi hizi zitakuwa zetu nasi tutazimiliki,” ingawa hata mimi Bwana nilikuwa huko,
Because thou hast said, the two nations, and the two lands, mine, shall become, that we may possess it Whereas Yahweh, had been there,
11 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutenda kwa kadiri ya hasira na wivu uliouonyesha katika chuki yako juu yao nami nitafanya nijulikane miongoni mwao wakati nitakapokuhukumu.
Therefore as I live, Declareth My Lord Yahweh, I will even deal according to thine anger, and according to thine envy, wherewith thou hast dealt, out of thy hatred with them, - So will I make myself known among them as soon as I shall judge thee
12 Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesikia mambo yote ya dharau uliyosema dhidi ya milima ya Israeli. Ulisema, “Wamefanyika ukiwa na kutiwa mikononi mwetu tuwararue.”
And thou shalt know that, I Yahweh, have heard all thy revilings which thou hast uttered against the mountains of Israel saying, They have become desolate, — To us, have they been given for food;
13 Ulijigamba dhidi yangu na kusema maneno dhidi yangu bila kujizuia, nami nikayasikia.
And so ye have magnified yourselves against me with your mouth, And have caused to abound against me your words, —I, have heard!
14 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati dunia yote inashangilia nitakufanya ukiwa.
Thus, saith My Lord Yahweh, — When all the earth is rejoicing, a desolation, will I make thee:
15 Kwa sababu ulishangilia wakati urithi wa nyumba ya Israeli ulipofanyika ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea. Utakuwa ukiwa, ee mlima Seiri, wewe na Edomu yote. Kisha ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
As thou didst rejoice over the inheritance of the house of Israel because it had become a desolation, so, will, I, do unto thee, — A desolation, shalt thou become, O Mount Seir And all Edom all of it, So shall they know that, I, am Yahweh.