< Ezekieli 35 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
Moreover, the word of Jehovah came to me, saying:
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya mlima Seiri, utabiri dhidi yake
Son of man, set thy face against Mount Seir, and prophesy against it,
3 na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume nawe, ee mlima Seiri, nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya ukiwa na usiyekaliwa na watu wala kulimika.
and say to it, Thus saith the Lord Jehovah: Behold, I am against thee, O Mount Seir, and I will stretch out my hand against thee, and I will make thee an utter desolation;
4 Nitaifanya miji yako kuwa magofu nawe utakuwa ukiwa. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
I will lay thy cities waste, and thou shalt be desolate, and thou shalt know that I am Jehovah.
5 “‘Kwa sababu ulificha moyoni uadui wa siku nyingi nawe ukawatoa Waisraeli wauawe kwa upanga wakati wa maafa yao, wakati adhabu yake ilipofikia kilele chake,
Because thou bearest a perpetual hatred, and deliverest up the sons of Israel to the sword in the time of their calamity, in the time when iniquity bringeth destruction:
6 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutia katika umwagaji damu nao utakufuatia. Kwa kuwa hakuchukia kumwaga damu, kumwaga damu kutakufuatia.
therefore, as I live, saith the Lord Jehovah, surely, to blood will I bring thee, and blood shall pursue thee; since thou hast not hated blood, blood shall pursue thee.
7 Nitaufanya Mlima Seiri ukiwa na usiokaliwa na watu wala kulimika na kuukatilia mbali na wote wanaokuja na wanaokwenda.
Thus will I make Mount Seir an utter desolation, and cut off from it him that passeth out, and him that returneth.
8 Nitaijaza milima yenu kwa watu wake waliouawa, wale waliouawa kwa upanga wataanguka juu ya vilima vyako na katika mabonde yako na katika makorongo yako yote.
And I will fill his valleys with the slain. Upon thy hills and in thy plains and in thy valleys shall fall they that are slain with the sword.
9 Nitakufanya ukiwa milele, watu hawataishi katika miji yako. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
I will make thee a perpetual desolation, and thy cities shall not be inhabited; and ye shall know that I am Jehovah.
10 “‘Kwa sababu umesema, “Mataifa haya mawili na nchi hizi zitakuwa zetu nasi tutazimiliki,” ingawa hata mimi Bwana nilikuwa huko,
Because thou hast said, “These two nations and these two countries shall be mine, and we shall possess them,” whereas Jehovah was there;
11 kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutenda kwa kadiri ya hasira na wivu uliouonyesha katika chuki yako juu yao nami nitafanya nijulikane miongoni mwao wakati nitakapokuhukumu.
therefore, as I live, saith the Lord Jehovah, I will do according to thine anger and according to thine envy which in thy hatred against them thou hast practised, and I will make myself known to them when I judge thee.
12 Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesikia mambo yote ya dharau uliyosema dhidi ya milima ya Israeli. Ulisema, “Wamefanyika ukiwa na kutiwa mikononi mwetu tuwararue.”
And thou shalt know that I am Jehovah, and that I have heard all thy blasphemies which thou hast spoken against the mountains of Israel, saying: “They are laid desolate; to us are they given to be devoured.”
13 Ulijigamba dhidi yangu na kusema maneno dhidi yangu bila kujizuia, nami nikayasikia.
Thus with your mouth have ye magnified yourselves against me, and multiplied your words against me; I have heard them.
14 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati dunia yote inashangilia nitakufanya ukiwa.
Thus saith the Lord Jehovah: When the whole land rejoiceth, I will prepare desolation for thee.
15 Kwa sababu ulishangilia wakati urithi wa nyumba ya Israeli ulipofanyika ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea. Utakuwa ukiwa, ee mlima Seiri, wewe na Edomu yote. Kisha ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
As thou didst rejoice over my inheritance, the house of Israel, because it was desolate, so will I do to thee! Mount Seir shall be desolate, and all Edom, even all of it; and they shall know that I am Jehovah.

< Ezekieli 35 >