< Ezekieli 34 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
And the word of Jehovah came to me, saying:
2 “Mwanadamu, tabiri juu ya wachungaji wa Israeli, tabiri na uwaambie: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wa wachungaji wa Israeli ambao hujitunza wenyewe tu! Je, haiwapasi wachungaji kutunza kundi la kondoo?
Son of man, prophesy against the shepherds of Israel; prophesy, and say to them, to the shepherds, Thus saith the Lord Jehovah: Woe to the shepherds of Israel, who feed themselves! Should not the shepherds feed the flocks?
3 Mnakula mafuta ya wanyama, mnavaa mavazi ya sufu na kuchinja kondoo walionona, lakini hamlitunzi kundi.
Ye eat the fat, and ye clothe you with the wool, ye kill that which is fatted; but ye feed not the flock.
4 Hamkuwatia nguvu walio dhaifu wala hamkuwaganga wenye maradhi wala kuwafunga waliojeruhiwa. Hamkuwarudisha waliotangatanga wala kuwatafuta wale waliopotea. Badala yake mmewatawala kwa ukali na kwa ukatili.
The weak do ye not strengthen, and the sick do ye not heal, and the wounded do ye not bind up; ye bring not back that which hath been driven away, neither seek ye that which hath been lost; but with force and with cruelty do ye rule them.
5 Hivyo walitawanyika kwa sababu hapakuwepo mchungaji, nao walipotawanyika, wakawa chakula cha wanyama wa mwitu wote.
Therefore are they scattered abroad, because there is no shepherd, and they are food to all the beasts of the field, or are scattered abroad.
6 Kondoo wangu walitawanyika, wakatangatanga kwenye milima yote na kwenye kila kilima kirefu. Kondoo wangu walitawanyika juu ya uso wa dunia yote bila kuwa na yeyote wa kuwaulizia wala wa kuwatafuta.
My sheep wander through all the mountains, and upon every high hill; yea, over the whole face of the land is my flock scattered, and none careth for them, or seeketh them.
7 “‘Kwa hiyo, ninyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana:
Therefore, ye shepherds, hear the word of Jehovah:
8 Kwa hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa sababu kondoo zangu wamekosa mchungaji na hivyo wametekwa nyara na kuwa chakula cha wanyama wote wa mwituni na kwa sababu wachungaji wangu, hawakuwatafuta kondoo zangu, bali wachungaji wamejitunza wenyewe, nao hawakuwalisha kondoo zangu,
As I live, saith the Lord Jehovah, surely, because my flock is become a prey, and my flock is become meat to all the beasts of the field because there is no shepherd, and because my shepherds search not for my flock, and feed themselves, and feed not my flock, —
9 kwa hiyo enyi wachungaji, sikieni neno la Bwana:
therefore, ye shepherds, hear the word of Jehovah.
10 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume na wachungaji nami nitawadai kondoo zangu mikononi mwao. Nitawafukuza kutoka kwenye kuchunga kundi langu, ili wachungaji wasiendelee kujitunza wenyewe. Nitaokoa kondoo zangu kutoka kwenye vinywa vyao, nao kondoo hawatakuwa tena chakula chao.
Thus saith the Lord Jehovah: Behold, I am against the shepherds, and I will require my flock at their hand, and cause them to cease from feeding the flock; neither shall the shepherds feed themselves any more; for I will deliver my flock from their mouth, and they shall not be meat for them.
11 “‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi mwenyewe nitawaulizia kondoo wangu na kuwatafuta.
For thus saith the Lord Jehovah: Behold I, even I, will seek my flock, and look after them;
12 Kama vile mchungaji atafutavyo kundi lake lililotawanyika wakati akiwa pamoja nalo, hivyo ndivyo nitakavyowatafuta kondoo wangu. Nitawaokoa kutoka mahali pote walipokuwa wametawanyikia katika siku ya mawingu na giza nene.
as a shepherd looketh after his flock in the day when he is among his sheep that are scattered, so will I look after my sheep, and will deliver them out of all the places where they have been scattered in the day of clouds and darkness.
13 Nitawatoa katika mataifa na kuwakusanya kutoka nchi mbalimbali, nami nitawaleta katika nchi yao wenyewe. Nitawalisha kwenye milima ya Israeli, katika mabonde na mahali pote panapokalika katika nchi.
And I will bring them out from the nations, and gather them from the countries; and I will bring them to their own land, and feed them upon the mountains of Israel, in the valleys, and in all the dwelling-places of the land.
14 Nitawachunga kwenye malisho mazuri na miinuko ya mlima wa Israeli patakuwa mahali pao pa malisho. Huko watajipumzisha kwa amani katika nchi ya malisho mazuri, nao watajilisha huko katika malisho tele katika milima ya Israeli.
I will feed them in a good pasture, and upon the high mountains of Israel shall their fold be; there shall they lie down in a good fold, and in a fat pasture shall they feed upon the mountains of Israel.
15 Mimi mwenyewe nitawachunga kondoo zangu na kuwafanya wapumzike, asema Bwana Mwenyezi.
I will feed my flock, and I will cause them to lie down, saith the Lord Jehovah.
16 Nitawaulizia kondoo waliopotea na kuwaleta waliotangatanga. Nitawafunga waliojeruhiwa na kuwatia nguvu walio dhaifu lakini wale waliojikinai na wenye nguvu nitawaangamiza. Nitalichunga kundi kwa haki.
I will seek that which was lost, and bring back that which was driven away, and will bind up that which was broken, and will strengthen the sick; but the fat and the strong will I destroy; I will feed them as they deserve.
17 “‘Kwa habari yenu, enyi kundi langu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitahukumu kati ya kondoo na kondoo, kati ya kondoo dume na mbuzi.
And as for you, O my sheep, thus saith the Lord Jehovah: Behold, I will judge between the weak of the flock and the strong ones, even the rams and the he-goats.
18 Je, haiwatoshi ninyi kujilisha kwenye malisho mazuri? Je, ni lazima ninyi kuyakanyaga pia malisho yenu yaliyobaki kwa miguu yenu? Je, haiwatoshi ninyi kunywa maji safi? Je, ni lazima kuyachafua maji mengine kwa miguu yenu?
Seemeth it a small thing to you to eat up the good pasture, but ye must tread down with your feet the residue of your pastures? and to drink of the clear waters, but ye must foul the residue with your feet?
19 Je, ni lazima kundi langu wajilishe kwa yale mliyoyakanyaga na kunywa maji mliyoyachafua kwa miguu yenu?
and that my sheep eat that which ye have trodden with your feet, and drink that which ye have fouled with your feet?
20 “‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi awaambialo: Tazama, mimi mwenyewe nitahukumu kati ya kondoo wanono na waliokonda.
Therefore thus saith the Lord Jehovah to them: Behold I, even I, will judge between the fat and the lean of the flock.
21 Kwa sababu mmewapiga kikumbo na kuwapiga kwa pembe zenu kondoo wote walio dhaifu mpaka wakawafukuza,
Because ye thrust with your side and with your shoulder, and push all the weak with your horns, till ye scatter them abroad,
22 nitaliokoa kundi langu na hawatatekwa nyara tena. Nitahukumu kati ya kondoo na kondoo.
therefore will I save my sheep, and they shall no more be a prey; and I will judge between sheep and sheep.
23 Nitaweka juu yao mchungaji mmoja, mtumishi wangu Daudi, naye atawachunga, atawachunga na kuwa mchungaji wao.
And I will raise up one shepherd over them, and he shall feed them, even my servant David; he shall feed them, and he shall be their shepherd.
24 Mimi Bwana nitakuwa Mungu wao, naye mtumishi wangu Daudi atakuwa mkuu miongoni mwao. Mimi Bwana nimenena.
And I, Jehovah, will be their God, and my servant David a prince among them. I, Jehovah, have spoken it.
25 “‘Nitafanya nao Agano la amani na kuwaondoa wanyama wa mwitu kutoka nchi yao ili kondoo wangu waweze kupumzika nyikani na msituni kwa salama.
And I will make with them a covenant of peace, and will cause evil beasts to cease out of the land, so that they shall dwell safely in the desert, and sleep in the woods.
26 Nitawabariki wao pamoja na maeneo yanayozunguka kilima changu. Nitawanyeshea mvua kwa majira yake, kutakuwepo mvua za baraka.
And I will make them, and the places round about my hill, a blessing; and I will cause the shower to come down in its season; showers rich in blessings shall there be.
27 Miti ya shambani itatoa matunda yake na ardhi itatoa mazao yake, watu watakaa salama katika nchi yao. Watajua kuwa Mimi ndimi Bwana, nitakapovunja vifungo vya nira zao na kuwaokoa kutoka mikono ya wale waliowafanya watumwa.
And the tree of the field shall yield her fruit, and the earth shall yield her increase; and they shall be secure in their land, and shall know that I am Jehovah, when I shall break the bands of their yoke and deliver them out of the hand of them that made them servants.
28 Hawatatekwa tena nyara na mataifa, wala wanyama pori hawatawala tena. Wataishi kwa salama, wala hakuna yeyote atakayewatia hofu.
And they shall no more be a prey to the nations, neither shall the beasts of the land devour them; but they shall dwell in security, and none shall make them afraid.
29 Nitawapa nchi yenye sifa kutokana na mazao yake, hawatapatwa na njaa katika nchi tena wala hawatadharauliwa na mataifa.
And I will raise up for them a plantation for my glory; and they shall no more be consumed with hunger in the land, neither shall they bear the reproach of the nations any more.
30 Ndipo watakapojua kuwa Mimi, Bwana, Mungu wao, niko pamoja nao, na kwamba wao, nyumba ya Israeli, ni watu wangu, asema Bwana Mwenyezi.
Then shall they know, that I, Jehovah, their God, am with them, and that they, the house of Israel, are my people, saith the Lord Jehovah.
31 Ninyi ni kondoo wangu, kondoo wa malisho yangu, ninyi ni watu wangu, nami ni Mungu wenu, asema Bwana Mwenyezi.’”
For ye, my flock, the flock of my pasture, are men, and I am your God, saith the Lord Jehovah.