< Ezekieli 32 >

1 Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema:
Pada tanggal satu bulan dua belas dalam tahun kedua belas masa pembuangan kami, TUHAN berkata kepadaku,
2 “Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Farao mfalme wa Misri na umwambie: “‘Wewe ni kama simba miongoni mwa mataifa, wewe ni kama joka kubwa baharini, unayevuruga maji kwa miguu yako na kuchafua vijito.
"Hai manusia fana, berilah peringatan keras kepada raja Mesir. Sampaikanlah pesan-Ku ini kepadanya, 'Engkau berlagak seperti singa muda di antara bangsa-bangsa, tetapi engkau lebih menyerupai buaya yang berkecimpung di dalam air. Kakimu mengeruhkan dan mengotorkan segala sungai.
3 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Nikiwa pamoja na wingi mkubwa wa watu nitautupa wavu wangu juu yako, nao watakukokota katika wavu wangu.
Pada waktu bangsa-bangsa berkumpul, Aku akan menangkap engkau dengan jala-Ku, dan membiarkan bangsa-bangsa itu menyeret engkau ke darat.
4 Nitakutupa nchi kavu na kukuvurumisha uwanjani. Nitawafanya ndege wote wa angani watue juu yako na wanyama wote wa nchi watajishibisha nyama yako.
Engkau akan Kuhempaskan ke tanah dan semua burung serta binatang dari seluruh dunia akan Kusuruh memakan engkau.
5 Nitatawanya nyama yako juu ya milima na kujaza mabonde kwa mabaki yako.
Lalu gunung-gunung dan lembah-lembah akan Kupenuhi dengan bangkaimu yang membusuk itu.
6 Nitailowanisha nchi kwa damu yako inayotiririka njia yote hadi milimani, nayo mabonde yatajazwa na nyama yako.
Darahmu akan Kutumpahkan sehingga membasahi gunung-gunung dan memenuhi sungai-sungai.
7 Nitakapokuzimisha, nitafunika mbingu na kuzitia nyota zake giza; nitalifunika jua kwa wingu, nao mwezi hautatoa nuru yake.
Pada saat Aku membinasakan engkau, langit akan Kuselubungi dan bintang-bintang akan Kuredupkan. Matahari akan Kusembunyikan di balik awan dan bulan tidak akan bercahaya.
8 Mianga yote itoayo nuru angani nitaitia giza juu yako; nitaleta giza juu ya nchi yako, asema Bwana Mwenyezi.
Sungguh, segala terang di langit akan Kupadamkan, dan bumi akan Kujadikan gelap gulita. Aku, TUHAN Yang Mahatinggi telah berbicara.
9 Nitaifadhaisha mioyo ya mataifa mengi nitakapokuangamiza miongoni mwa mataifa, nikikuleta uhamishoni miongoni mwa nchi ambazo haujapata kuzijua.
Pada waktu Aku menyiarkan berita tentang kehancuranmu di negeri-negeri yang belum kaukenal, banyak bangsa akan menjadi cemas.
10 Nitayafanya mataifa mengi wakustaajabie, wafalme wao watatetemeka kwa hofu kwa ajili yako nitakapotikisa upanga wangu mbele yao. Siku ya anguko lako kila mmoja wao atatetemeka kila dakika kwa ajili ya maisha yake.
Sungguh, Aku akan mengayunkan pedang-Ku dan mengalahkan engkau. Raja-raja dan bangsa-bangsa akan melihat tindakan-Ku itu terhadap engkau. Pada saat itu mereka akan gemetar ketakutan dan menggigil karena takut mati.'"
11 “‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Upanga wa mfalme wa Babeli utakuja dhidi yako.
TUHAN Yang Mahatinggi berkata kepada raja Mesir, "Pedang raja Babel akan diacungkan kepadamu.
12 Nitafanya makundi yako ya wajeuri kuanguka kwa panga za watu mashujaa, taifa katili kuliko mataifa yote. Watakivunjavunja kiburi cha Misri, nayo makundi yake yote ya wajeuri yatashindwa.
Prajurit-prajurit dari bangsa-bangsa yang kejam akan Kusuruh mencabut pedang mereka dan membantai seluruh rakyatmu. Rakyatmu dan segala apa yang kaubanggakan akan hancur lebur.
13 Nitaangamiza mifugo yake yote wanaojilisha kando ya maji mengi, hayatavurugwa tena kwa mguu wa mwanadamu wala kwato za mnyama hazitayachafua tena.
Ternakmu akan Kubantai di tepi sungai-sungai tempat mereka minum. Baik manusia maupun hewan tak akan mengeruhkan air sungai itu lagi.
14 Kisha nitafanya maji yake yatulie na kufanya vijito vyake vitiririke kama mafuta, asema Bwana Mwenyezi.
Maka sungai-sungai di negerimu akan Kujernihkan dan Kubuat mengalir dengan tenang. Aku, TUHAN Yang Mahatinggi telah berbicara.
15 Nitakapoifanya Misri kuwa ukiwa na kuiondolea nchi kila kitu kilichomo ndani yake, nitakapowapiga wote waishio humo, ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’
Bilamana Mesir Kujadikan padang gurun yang sepi, serta Kubinasakan semua yang tinggal di situ, mereka akan tahu bahwa Akulah TUHAN.
16 “Hili ndilo ombolezo watakalomwimbia. Binti za mataifa wataliimba, kwa kuwa Misri na makundi yake yote ya wajeuri wataliimba, asema Bwana Mwenyezi.”
Peringatan yang keras ini akan menjadi nyanyian kabung. Kaum wanita dari bangsa-bangsa lain akan menyanyikannya sebagai tanda berkabung bagi Mesir dan seluruh rakyatnya. Aku, TUHAN Yang Mahatinggi telah berbicara."
17 Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kwanza, siku ya kumi na tano ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
Pada tanggal lima belas bulan satu dalam tahun kedua belas masa pembuangan kami, TUHAN berkata lagi kepadaku,
18 “Mwanadamu, omboleza kwa ajili ya makundi ya wajeuri wa Misri na uwatupe kuzimu yeye na binti za mataifa yenye nguvu, waende huko pamoja nao washukao shimoni. (questioned)
"Hai manusia fana, berkabunglah bagi rakyat di Mesir. Kirimlah mereka ke dunia orang mati bersama-sama dengan negeri-negeri kuat lainnya.
19 Je, ninyi mnamzidi nani kwa uzuri? Shukeni chini! Nanyi mkalazwe pamoja na hao wasiotahiriwa!
Katakanlah kepada mereka, 'Sangkamu kamukah yang paling jelita? Kamu akan turun ke dunia orang mati, dan dibaringkan di antara orang-orang yang tidak mengenal Allah.'
20 Wataanguka miongoni mwa wale waliouawa kwa upanga. Upanga umefutwa, mwache aburutwe mbali pamoja na hao wajeuri wake wote.
Bangsa Mesir akan mati bersama dengan mereka yang tewas dalam pertempuran. Sebuah pedang sudah siap untuk membunuh mereka semua.
21 Kutoka kuzimu viongozi hodari watanena kuhusu Misri pamoja na wale walioungana nao, ‘Wameshuka chini, nao wamelala kimya pamoja na hao wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.’ (Sheol h7585)
Pahlawan-pahlawan yang gagah berani dan orang-orang yang berperang di pihak Mesir menyambut dengan gembira kedatangan orang Mesir ke dunia orang mati. Mereka bersorak begini, 'Orang-orang yang tidak mengenal Allah itu telah tewas dalam pertempuran. Sekarang mereka datang ke mari dan berbaring di sini!' (Sheol h7585)
22 “Ashuru yuko huko pamoja na jeshi lake lote, amezungukwa na makaburi ya watu wake wote waliouawa, wale wote walioanguka kwa upanga.
Asyur berbaring di sana, dikelilingi oleh kuburan prajurit-prajuritnya. Mereka semua telah tewas dalam pertempuran. Kuburan mereka ada di bagian yang paling dalam di dunia orang mati. Ketika masih hidup, mereka menimbulkan ketakutan di dunia.
23 Makaburi yao yako kwenye kina cha chini cha shimo na jeshi lake limelala kulizunguka kaburi lake. Wote waliokuwa wameeneza hofu kuu katika nchi ya walio hai wameuawa, wameanguka kwa upanga.
24 “Elamu yuko huko, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote wameuawa, wameanguka kwa upanga. Wote waliokuwa wameeneza hofu katika nchi ya walio hai walishuka kuzimu bila kutahiriwa. Wanaichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni. (questioned)
Elam ada di sana dengan kuburan prajuritnya di sekelilingnya. Tanpa disunat, mereka semua tewas dalam pertempuran, lalu turun ke dunia orang mati. Ketika hidup, mereka menimbulkan ketakutan, tetapi sekarang mereka telah mati dan harus menanggung malu bersama orang-orang yang telah tewas dalam pertempuran.
25 Kitanda kimetandikwa kwa ajili yake miongoni mwa waliouawa, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote ni watu wasiotahiriwa, wameuawa kwa upanga. Kwa sababu vitisho vyao vilienea katika nchi ya walio hai, wameichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni, nao wamewekwa miongoni mwa waliouawa.
26 “Mesheki na Tubali wako humo, pamoja na makundi yao ya wajeuri wakiwa wameyazunguka makaburi yao. Wote hawakutahiriwa, wameuawa kwa upanga kwa sababu walieneza vitisho vyao katika nchi ya walio hai.
Mesekh dan Tubal ada di situ, dikelilingi oleh kuburan prajurit-prajurit mereka. Tanpa disunat, mereka semua tewas dalam pertempuran. Ketika hidup, mereka menimbulkan ketakutan di dunia.
27 Je, hawakulala na mashujaa wengine wasiotahiriwa waliouawa, ambao wameshuka kaburini wakiwa na silaha zao za vita, ambao panga zao ziliwekwa chini ya vichwa vyao na uovu wao juu ya mifupa yao? Adhabu kwa ajili ya dhambi zao ilikuwa juu ya mifupa yao, ingawa vitisho vya mashujaa hawa vilikuwa vimeenea hadi kwenye nchi ya walio hai. (Sheol h7585)
Mereka tidak mendapat penguburan secara terhormat seperti pahlawan di zaman dahulu yang turun ke dunia orang mati dengan bersenjata lengkap. Pahlawan-pahlawan itu dikuburkan dengan pedang di bawah kepala dan perisai di atas dada. Waktu masih hidup, pahlawan-pahlawan sungguh perkasa sehingga membuat takut semua orang. (Sheol h7585)
28 “Wewe pia, ee Farao, utavunjwa nawe utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.
Demikianlah orang Mesir akan dikuburkan dan dibaringkan di tengah orang-orang yang tidak mengenal Allah dan tewas dalam pertempuran.
29 “Edomu yuko humo, wafalme wake wote na wakuu wake wote, ambao ijapokuwa wana nguvu, wamelazwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga. Wamelala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale washukao shimoni.
Edom ada di sana dengan semua raja dan penguasanya. Dahulu mereka adalah prajurit-prajurit yang kuat, tetapi sekarang mereka terbaring di dunia orang mati bersama dengan orang-orang mati lainnya yang tidak mengenal Allah.
30 “Wakuu wote wa kaskazini na Wasidoni wote wako huko, wameshuka chini pamoja na waliouawa kwa aibu ijapokuwa kuna vitisho vilivyosababishwa na nguvu zao. Wamelala bila kutahiriwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga na kuchukua aibu yao pamoja na wale washukao chini shimoni.
Semua pangeran dari utara ada di sana, demikian juga orang-orang Sidon. Dahulu kekuasaan mereka menimbulkan ketakutan, tetapi sekarang mereka dipermalukan dan tanpa disunat turun ke dunia orang mati bersama orang-orang yang tewas dalam pertempuran. Di sana mereka berbaring dan menanggung noda bersama orang-orang yang turun ke dunia orang mati.
31 “Farao, yeye pamoja na jeshi lake lote, atakapowaona atafarijiwa kwa ajili ya makundi yake yote ya wajeuri, wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.
Bilamana raja Mesir dan tentaranya tiba di dunia orang mati dan melihat semua orang itu yang telah tewas dalam pertempuran, mereka akan merasa terhibur. Aku TUHAN Yang Mahatinggi telah berbicara.
32 Ingawa nilimfanya Farao aeneze vitisho vyake katika nchi ya walio hai, Farao pamoja na makundi yake yote ya wajeuri watalazwa miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.”
Akulah yang menyebabkan raja Mesir menimbulkan ketakutan pada orang-orang yang hidup, tetapi dia dan tentaranya akan tewas dan dibaringkan bersama semua orang yang tidak mengenal Allah dan gugur dalam pertempuran. Aku TUHAN Yang Mahatinggi telah berbicara."

< Ezekieli 32 >