< Ezekieli 32 >

1 Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema:
And it came to pass in the twelfth year, in the twelfth month, in the first day of the month, that the word of the Lord came to me, saying:
2 “Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Farao mfalme wa Misri na umwambie: “‘Wewe ni kama simba miongoni mwa mataifa, wewe ni kama joka kubwa baharini, unayevuruga maji kwa miguu yako na kuchafua vijito.
Son of man, take up a lamentation for Pharao the king of Egypt, and say to him: Thou art like the lion of the nations, and the dragon that is in the sea: and thou didst push with the horn in thy rivers, and didst trouble the waters with thy feet, and didst trample upon their streams.
3 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Nikiwa pamoja na wingi mkubwa wa watu nitautupa wavu wangu juu yako, nao watakukokota katika wavu wangu.
Therefore, thus saith the Lord God: I will spread out my net over thee with the multitude of many people, and I will draw thee up in my net.
4 Nitakutupa nchi kavu na kukuvurumisha uwanjani. Nitawafanya ndege wote wa angani watue juu yako na wanyama wote wa nchi watajishibisha nyama yako.
And I will throw thee out on the land, I will cast thee away into the open field: and I will cause all the fowls of the air to dwell upon thee, and I will fill the beasts of all the earth with thee.
5 Nitatawanya nyama yako juu ya milima na kujaza mabonde kwa mabaki yako.
And I will lay thy flesh upon the mountains, and will fill thy hills with thy corruption,
6 Nitailowanisha nchi kwa damu yako inayotiririka njia yote hadi milimani, nayo mabonde yatajazwa na nyama yako.
And I will water the earth with thy stinking blood upon the mountains, and the valleys shall be filled with thee.
7 Nitakapokuzimisha, nitafunika mbingu na kuzitia nyota zake giza; nitalifunika jua kwa wingu, nao mwezi hautatoa nuru yake.
And I will cover the heavens, when thou shalt be put out, and I will make the stars thereof dark: I will cover the sun with a cloud, and the moon shall not give her light.
8 Mianga yote itoayo nuru angani nitaitia giza juu yako; nitaleta giza juu ya nchi yako, asema Bwana Mwenyezi.
I will make all the lights of heaven to mourn over thee: and I will cause darkness upon thy land, saith the Lord God, when thy wounded shall fall in the midst of the land, saith the Lord God.
9 Nitaifadhaisha mioyo ya mataifa mengi nitakapokuangamiza miongoni mwa mataifa, nikikuleta uhamishoni miongoni mwa nchi ambazo haujapata kuzijua.
And I shall provoke to anger the heart of many people, when I shall have brought in thy destruction among the nations upon the lands, which thou knowest not.
10 Nitayafanya mataifa mengi wakustaajabie, wafalme wao watatetemeka kwa hofu kwa ajili yako nitakapotikisa upanga wangu mbele yao. Siku ya anguko lako kila mmoja wao atatetemeka kila dakika kwa ajili ya maisha yake.
And I will make many people to be amazed at thee, and their kings shell be horribly afraid for thee, when my sword shall begin to fly upon their faces: and they shall be astonished on a sudden, every one for his own life, in the day of their ruin.
11 “‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Upanga wa mfalme wa Babeli utakuja dhidi yako.
For thus saith the Lord God: The sword of the king of Babylon shall come upon thee,
12 Nitafanya makundi yako ya wajeuri kuanguka kwa panga za watu mashujaa, taifa katili kuliko mataifa yote. Watakivunjavunja kiburi cha Misri, nayo makundi yake yote ya wajeuri yatashindwa.
By the swords of the mighty I will overthrow thy multitude: all these nations are invincible: and they shall waste the pride of Egypt, and the multitude thereof shall be destroyed.
13 Nitaangamiza mifugo yake yote wanaojilisha kando ya maji mengi, hayatavurugwa tena kwa mguu wa mwanadamu wala kwato za mnyama hazitayachafua tena.
I will destroy also all the beasts thereof that were beside the great waters: and the foot of man shall trouble them no more, neither shall the hoof of beasts trouble them.
14 Kisha nitafanya maji yake yatulie na kufanya vijito vyake vitiririke kama mafuta, asema Bwana Mwenyezi.
Then will I make their waters clear, and cause their rivers to run like oil, saith the Lord God:
15 Nitakapoifanya Misri kuwa ukiwa na kuiondolea nchi kila kitu kilichomo ndani yake, nitakapowapiga wote waishio humo, ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’
When I shall have made the land of Egypt desolate: and the land shall be destitute of her fulness, when I shall have struck all the inhabitants thereof: and they shall know that I am the Lord.
16 “Hili ndilo ombolezo watakalomwimbia. Binti za mataifa wataliimba, kwa kuwa Misri na makundi yake yote ya wajeuri wataliimba, asema Bwana Mwenyezi.”
This is the lamentation, and they shall lament therewith: the daughters of the nations shall lament therewith: for Egypt, and for the multitude thereof they shall lament therewith, saith the Lord God.
17 Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kwanza, siku ya kumi na tano ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
And it came to pass in the twelfth year, in the fifteenth day of the month that the word of the Lord came to me, saying:
18 “Mwanadamu, omboleza kwa ajili ya makundi ya wajeuri wa Misri na uwatupe kuzimu yeye na binti za mataifa yenye nguvu, waende huko pamoja nao washukao shimoni. (questioned)
Son of man, sing a mournful song for the multitude of Egypt: and cast her down, both her, and the daughters of the mighty nations to the lowest part of the earth, with them that go down into the pit.
19 Je, ninyi mnamzidi nani kwa uzuri? Shukeni chini! Nanyi mkalazwe pamoja na hao wasiotahiriwa!
Whom dost thou excel in beauty? go down and sleep with the uncircumcised.
20 Wataanguka miongoni mwa wale waliouawa kwa upanga. Upanga umefutwa, mwache aburutwe mbali pamoja na hao wajeuri wake wote.
They shall fall in the midst of them that are slain with the sword: the sword is given, they have drawn her down, and all her people.
21 Kutoka kuzimu viongozi hodari watanena kuhusu Misri pamoja na wale walioungana nao, ‘Wameshuka chini, nao wamelala kimya pamoja na hao wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.’ (Sheol h7585)
The most mighty among the strong ones shall speak to him from the midst of hell, they that went down with his helpers, and slept uncircumcised, slain by the sword. (Sheol h7585)
22 “Ashuru yuko huko pamoja na jeshi lake lote, amezungukwa na makaburi ya watu wake wote waliouawa, wale wote walioanguka kwa upanga.
Assur is there, and all his multitude: their graves are round about him, all of them slain, and that fell by the sword.
23 Makaburi yao yako kwenye kina cha chini cha shimo na jeshi lake limelala kulizunguka kaburi lake. Wote waliokuwa wameeneza hofu kuu katika nchi ya walio hai wameuawa, wameanguka kwa upanga.
Whose graves are set in the lowest parts of the pit: and his multitude lay round about his grave: all of them slain, and fallen by the sword, they that heretofore spread terror in the land of the living.
24 “Elamu yuko huko, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote wameuawa, wameanguka kwa upanga. Wote waliokuwa wameeneza hofu katika nchi ya walio hai walishuka kuzimu bila kutahiriwa. Wanaichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni. (questioned)
There is Elam and all his multitude round about his grave, all of them slain, and fallen by the sword; that went down uncircumcised to the lowest parts of the earth: that caused their terror in the land of the living, and they have borne their shame with them that go down into the pit.
25 Kitanda kimetandikwa kwa ajili yake miongoni mwa waliouawa, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote ni watu wasiotahiriwa, wameuawa kwa upanga. Kwa sababu vitisho vyao vilienea katika nchi ya walio hai, wameichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni, nao wamewekwa miongoni mwa waliouawa.
In the midst of the slain they have set him a bed among all his people: their graves are round about him: all these are uncircumcised, and slain by the sword: for they spread their terror in the land of the living, and have borne their shame with them that descend into the pit: they are laid in the midst of the slain.
26 “Mesheki na Tubali wako humo, pamoja na makundi yao ya wajeuri wakiwa wameyazunguka makaburi yao. Wote hawakutahiriwa, wameuawa kwa upanga kwa sababu walieneza vitisho vyao katika nchi ya walio hai.
There is Mosoch, and Thubal, and all their multitude: their graves are round about him: all of them uncircumcised and slain, and fallen by the sword: though they spread their terror in the land of the living.
27 Je, hawakulala na mashujaa wengine wasiotahiriwa waliouawa, ambao wameshuka kaburini wakiwa na silaha zao za vita, ambao panga zao ziliwekwa chini ya vichwa vyao na uovu wao juu ya mifupa yao? Adhabu kwa ajili ya dhambi zao ilikuwa juu ya mifupa yao, ingawa vitisho vya mashujaa hawa vilikuwa vimeenea hadi kwenye nchi ya walio hai. (Sheol h7585)
And they shall not sleep with the brave, and with them that fell uncircumcised, that went down to hell with their weapons, and laid their swords under their heads, and their iniquities were in their bones, because they were the terror of the mighty in the land of the living. (Sheol h7585)
28 “Wewe pia, ee Farao, utavunjwa nawe utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.
So thou also shalt be broken in the midst of the uncircumcised, and shalt sleep with them that are slain by the sword.
29 “Edomu yuko humo, wafalme wake wote na wakuu wake wote, ambao ijapokuwa wana nguvu, wamelazwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga. Wamelala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale washukao shimoni.
There is Edom, and her kings, and all her princes, who with their army are joined with them that are slain by the sword: and have slept with the uncircumcised, and with them that go down into the pit.
30 “Wakuu wote wa kaskazini na Wasidoni wote wako huko, wameshuka chini pamoja na waliouawa kwa aibu ijapokuwa kuna vitisho vilivyosababishwa na nguvu zao. Wamelala bila kutahiriwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga na kuchukua aibu yao pamoja na wale washukao chini shimoni.
There are all the princes of the north, and all the hunters: who were brought down with the slain, fearing, and confounded in their strength: who slept uncircumcised with them that are slain by the sword, and have borne their shame with them that go down into the pit.
31 “Farao, yeye pamoja na jeshi lake lote, atakapowaona atafarijiwa kwa ajili ya makundi yake yote ya wajeuri, wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.
Pharao saw them, and he was comforted concerning all his multitude, which was slain by the sword: Pharao, and all his army, saith the Lord God:
32 Ingawa nilimfanya Farao aeneze vitisho vyake katika nchi ya walio hai, Farao pamoja na makundi yake yote ya wajeuri watalazwa miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.”
Because I have spread my terror in the land of the living, and he hath slept in the midst of the uncircumcised with them that are slain by the sword: Pharao and all his multitude, saith the Lord God.

< Ezekieli 32 >