< Ezekieli 31 >

1 Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa tatu, siku ya kwanza, neno la Bwana likanijia, kusema:
La onzième année, le premier jour du troisième mois, la parole de l'Éternel me fut adressée, en ces termes:
2 “Mwanadamu, mwambie Farao mfalme wa Misri na makundi yake ya wajeuri: “‘Je, ni nani awezaye kulinganishwa na wewe katika fahari.
Fils de l'homme, dis à Pharaon, roi d'Égypte, et à sa multitude: A qui ressembles-tu dans ta grandeur?
3 Angalia Ashuru, wakati fulani ilikuwa mwerezi huko Lebanoni, ukiwa na matawi mazuri ukitia msitu kivuli; ulikuwa mrefu sana, kilele chake kilipita majani ya miti yote.
Voici, l'Assyrie était un cèdre du Liban aux belles branches, au feuillage touffu, haut de taille et élevant sa cime jusqu'aux nues.
4 Maji mengi yaliustawisha, chemchemi zenye maji mengi ziliufanya urefuke; vijito vyake vilitiririka pale ulipoota pande zote na kupeleka mifereji yake kwenye miti yote ya shambani.
Les eaux l'avaient fait croître, l'abîme l'avait fait monter fort haut, en faisant couler ses fleuves autour du lieu où il était planté, et en envoyant ses canaux à tous les arbres des champs.
5 Hivyo ukarefuka kupita miti yote ya shambani; vitawi vyake viliongezeka na matawi yake yakawa marefu, yakitanda kwa sababu ya wingi wa maji.
C'est pourquoi sa hauteur dépassait tous les arbres des champs; ses branches avaient multiplié, et ses rameaux s'étendaient, grâce à l'abondance des eaux qui le faisaient croître.
6 Ndege wote wa angani wakaweka viota kwenye vitawi vyake, wanyama wote wa shambani wakazaana chini ya matawi yake, mataifa makubwa yote yaliishi chini ya kivuli chake.
Tous les oiseaux des cieux nichaient dans ses branches, et toutes les bêtes des champs faisaient leurs petits sous ses rameaux, et de nombreuses nations habitaient toutes à son ombre.
7 Ulikuwa na fahari katika uzuri, ukiwa na matawi yaliyotanda, kwa kuwa mizizi yake ilikwenda chini mpaka kwenye maji mengi.
Il était beau dans sa grandeur et par l'étendue de ses branches; car ses racines plongeaient dans des eaux abondantes.
8 Mierezi katika bustani ya Mungu haikuweza kushindana nao, wala misunobari haikuweza kulingana na vitawi vyake, wala miaramoni haikulinganishwa na matawi yake, wala hakukuwa na mti katika bustani ya Mungu wa kulinganisha na uzuri wake.
Les cèdres du jardin de Dieu ne lui ôtaient rien de son lustre; les cyprès n'égalaient point ses branches, et les platanes n'étaient point semblables à ses rameaux; aucun arbre du jardin de Dieu n'égalait sa beauté.
9 Niliufanya kuwa mzuri ukiwa na matawi mengi, ulionewa wivu na miti yote ya Edeni katika bustani ya Mungu.
Je l'avais rendu beau par la multitude de ses branches, et tous les arbres d'Éden, qui étaient au jardin de Dieu, lui portaient envie.
10 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ulikuwa mrefu sana, kilele chake kikiwa juu ya majani manene ya miti na kwa sababu ulikuwa na kiburi cha urefu wake,
C'est pourquoi, ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: Parce qu'il s'est élevé en hauteur, qu'il a produit une cime touffue, et que son cœur s'est enorgueilli de sa grandeur,
11 niliutia mikononi mwa mtawala wa mataifa, ili yeye aushughulikie sawasawa na uovu wake. Nikaukatilia mbali,
Je l'ai livré entre les mains du puissant des nations, qui les traitera comme il fallait: je l'ai chassé à cause de ses crimes.
12 nayo mataifa mageni yaliyo makatili sana yaliukata huo mti na kuuacha. Matawi yake yalianguka juu ya milima na kwenye mabonde yote, vitawi vyake vikavunjika na kusambaa katika makorongo yote ya nchi. Mataifa yote ya duniani yakaondoka kutoka kwenye kivuli chake na kuuacha.
Des étrangers, les plus terribles d'entre les nations, l'ont coupé et rejeté; ses branches sont tombées sur les montagnes et dans toutes les vallées, et ses rameaux se sont brisés dans tous les ravins du pays, et tous les peuples de la terre se sont retirés de dessous son ombre et l'ont abandonné.
13 Ndege wote wa angani wakakaa kwenye ule mti ulioanguka na wanyama pori wote wakakaa katikati ya vitawi vyake.
Tous les oiseaux des cieux se tiennent sur ses ruines, et toutes les bêtes des champs ont fait leur gîte de ses rameaux,
14 Kamwe hakutakuwa na miti mingine kando ya hayo maji itakayorefuka zaidi ya huo, vilele vyake vikiwa juu ya majani yote ya miti. Hakuna miti mingine, hata kama imekunywa maji vizuri namna gani, itakayofikia urefu huo. Yote mwisho wake ni kifo, na kuingia ardhini, kama vile ilivyo kwa wanadamu, pamoja na wale waendao shimoni.
Afin qu'aucun des arbres arrosés d'eau ne garde plus sa hauteur, et ne lance plus sa cime touffue, afin que tous ceux qui sont arrosés d'eau ne gardent plus leur élévation; car tous sont livrés à la mort dans les profondeurs de la terre, parmi les enfants des hommes, avec ceux qui descendent dans la fosse.
15 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mwerezi uliposhushwa chini kaburini nilizifunika chemchemi zenye maji mengi kwa maombolezo: Nilivizuia vijito vyake na wingi wa maji yake nikauzuia. Kwa sababu yake niliivika Lebanoni huzuni, nayo miti yote ya shambani ikanyauka. (Sheol h7585)
Ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: Au jour qu'il descendit dans le Sépulcre, j'ai fait mener deuil; à cause de lui, je couvris l'abîme, et empêchai ses fleuves de couler, et les grandes eaux furent retenues; j'ai mis le Liban en deuil à cause de lui, et tous les arbres des champs en défaillirent. (Sheol h7585)
16 Niliyafanya mataifa yatetemeke kwa kishindo cha kuanguka kwake wakati nilipoushusha chini kaburini pamoja na wale washukao shimoni. Ndipo miti yote ya Edeni, miti iliyo bora kuliko yote na iliyo mizuri sana ya Lebanoni, miti yote ile iliyokunywa maji vizuri, ilifarijika hapa duniani. (Sheol h7585)
J'ébranlai les nations par le bruit de sa chute, quand je l'ai précipité dans le Sépulcre, avec ceux qui descendent dans la fosse. Tous les arbres d'Éden, l'élite et le meilleur du Liban, tous arrosés d'eau, furent consolés dans les profondeurs de la terre. (Sheol h7585)
17 Wale walioishi katika kivuli chake, wale walioungana naye miongoni mwa mataifa, nao pia walikuwa wamezikwa pamoja naye, wakiungana na wale waliouawa kwa upanga. (Sheol h7585)
Eux aussi sont descendus avec lui dans le Sépulcre, vers ceux que l'épée blessa à mort; ils étaient son bras, et habitaient à son ombre au milieu des nations. (Sheol h7585)
18 “‘Ni miti ipi ya Edeni inayoweza kulinganishwa nawe kwa fahari na utukufu? Hata hivyo, wewe pia, utashushwa chini pamoja na miti ya Edeni mpaka kuzimu, utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga. “‘Huyu ni Farao pamoja na makundi yake yote ya wajeuri, asema Bwana Mwenyezi.’” (questioned)
A qui ressembles-tu ainsi, en gloire et en grandeur, parmi les arbres d'Éden? Tu seras jeté bas avec les arbres d'Éden dans les profondeurs de la terre; tu seras couché au milieu des incirconcis, avec ceux que l'épée a blessés à mort. Tel sera Pharaon et toute sa multitude, dit le Seigneur, l'Éternel.

< Ezekieli 31 >