< Ezekieli 31 >
1 Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa tatu, siku ya kwanza, neno la Bwana likanijia, kusema:
La onzième année, au troisième mois, le premier du mois, la parole de Yahweh me fut adressée en ces termes:
2 “Mwanadamu, mwambie Farao mfalme wa Misri na makundi yake ya wajeuri: “‘Je, ni nani awezaye kulinganishwa na wewe katika fahari.
« Fils de l’homme, dis à Pharaon, roi d’Égypte, et à sa multitude: À qui ressembles-tu dans ta grandeur?
3 Angalia Ashuru, wakati fulani ilikuwa mwerezi huko Lebanoni, ukiwa na matawi mazuri ukitia msitu kivuli; ulikuwa mrefu sana, kilele chake kilipita majani ya miti yote.
Voilà qu’Assur était un cèdre sur le Liban, à la belle ramure, à l’ombrage épais, à la taille élevée, et ayant sa cime dans les nues.
4 Maji mengi yaliustawisha, chemchemi zenye maji mengi ziliufanya urefuke; vijito vyake vilitiririka pale ulipoota pande zote na kupeleka mifereji yake kwenye miti yote ya shambani.
Les eaux l’avaient fait croître, l’abîme l’avait fait grandir, en faisant couler ses fleuves autour du lieu où il était planté et en envoyant ses ruisseaux à tous les arbres des champs.
5 Hivyo ukarefuka kupita miti yote ya shambani; vitawi vyake viliongezeka na matawi yake yakawa marefu, yakitanda kwa sababu ya wingi wa maji.
C’est pourquoi sa taille s’élevait, plus haute que les arbres des champs; ses branches avaient grandi, ses rameaux s’étaient allongés, grâce aux eaux abondantes du temps de sa croissance.
6 Ndege wote wa angani wakaweka viota kwenye vitawi vyake, wanyama wote wa shambani wakazaana chini ya matawi yake, mataifa makubwa yote yaliishi chini ya kivuli chake.
Dans ses branches tous les oiseaux du ciel nichaient; sous ses rameaux mettaient bas tous les animaux des champs, et à son ombre étaient assises des nations nombreuses.
7 Ulikuwa na fahari katika uzuri, ukiwa na matawi yaliyotanda, kwa kuwa mizizi yake ilikwenda chini mpaka kwenye maji mengi.
Il était beau par sa grandeur, par la longueur de ses branches, car ses racines plongeaient dans des eaux abondantes.
8 Mierezi katika bustani ya Mungu haikuweza kushindana nao, wala misunobari haikuweza kulingana na vitawi vyake, wala miaramoni haikulinganishwa na matawi yake, wala hakukuwa na mti katika bustani ya Mungu wa kulinganisha na uzuri wake.
Les cèdres ne l’obscurcissaient pas dans le jardin de Dieu, les cyprès n’égalaient pas ses branches, et les platanes n’étaient pas comme ses rameaux; aucun arbre dans le jardin de Dieu ne l’égalait en beauté.
9 Niliufanya kuwa mzuri ukiwa na matawi mengi, ulionewa wivu na miti yote ya Edeni katika bustani ya Mungu.
Je l’avais rendu beau par la multitude de ses rameaux; tous les arbres d’Éden lui portaient envie, tous ceux qui sont dans le jardin de Dieu.
10 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ulikuwa mrefu sana, kilele chake kikiwa juu ya majani manene ya miti na kwa sababu ulikuwa na kiburi cha urefu wake,
C’est pourquoi ainsi parle le Seigneur Yahweh: Parce qu’il s’est élevé en hauteur, parce qu’il a porté sa cime jusque dans les nues; et que son cœur s’est enorgueilli de son élévation,
11 niliutia mikononi mwa mtawala wa mataifa, ili yeye aushughulikie sawasawa na uovu wake. Nikaukatilia mbali,
je l’ai livré aux mains du dieu des nations, qui le traitera à sa guise; à cause de sa méchanceté, je l’ai chassé.
12 nayo mataifa mageni yaliyo makatili sana yaliukata huo mti na kuuacha. Matawi yake yalianguka juu ya milima na kwenye mabonde yote, vitawi vyake vikavunjika na kusambaa katika makorongo yote ya nchi. Mataifa yote ya duniani yakaondoka kutoka kwenye kivuli chake na kuuacha.
Des étrangers l’ont coupé, — nation féroce entre toutes, — et laissé là; sur les montagnes et dans toutes les vallées; ses branches sont tombées; ses rameaux brisés gisent dans tous les ravins du pays; tous les peuples de la terre se sont éloignés de son ombre et l’ont abandonné.
13 Ndege wote wa angani wakakaa kwenye ule mti ulioanguka na wanyama pori wote wakakaa katikati ya vitawi vyake.
Sur ses débris tous les oiseaux du ciel viennent se poser, et dans ses rameaux se sont retirés tous les animaux des champs:
14 Kamwe hakutakuwa na miti mingine kando ya hayo maji itakayorefuka zaidi ya huo, vilele vyake vikiwa juu ya majani yote ya miti. Hakuna miti mingine, hata kama imekunywa maji vizuri namna gani, itakayofikia urefu huo. Yote mwisho wake ni kifo, na kuingia ardhini, kama vile ilivyo kwa wanadamu, pamoja na wale waendao shimoni.
afin qu’aucun arbre planté sur les eaux ne s’élève en hauteur et ne porte sa cime jusque dans les nues, et qu’aucun de ceux qui s’abreuvent d’eau ne s’appuie sur lui-même dans son orgueil. Car ils sont tous voués à la mort, aux profondeurs de la terre, mêlés aux enfants des hommes; à ceux qui descendent dans la fosse.
15 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mwerezi uliposhushwa chini kaburini nilizifunika chemchemi zenye maji mengi kwa maombolezo: Nilivizuia vijito vyake na wingi wa maji yake nikauzuia. Kwa sababu yake niliivika Lebanoni huzuni, nayo miti yote ya shambani ikanyauka. (Sheol )
Ainsi parle le Seigneur Yahweh: Le jour où il descendit au schéol, j’ai fait mener le deuil; à cause de lui j’ai voilé l’abîme, j’ai retenu le cours de ses fleuves, et les grandes eaux se sont arrêtées; à cause de lui, j’ai assombri le Liban, et à cause de lui, tous les arbres des champs ont langui. (Sheol )
16 Niliyafanya mataifa yatetemeke kwa kishindo cha kuanguka kwake wakati nilipoushusha chini kaburini pamoja na wale washukao shimoni. Ndipo miti yote ya Edeni, miti iliyo bora kuliko yote na iliyo mizuri sana ya Lebanoni, miti yote ile iliyokunywa maji vizuri, ilifarijika hapa duniani. (Sheol )
Au bruit de sa chute, j’ai fait trembler les nations, quand je l’ai fait descendre au schéol, avec ceux qui descendent dans la fosse. Ils se sont consolés dans les profondeurs de la terre, tous les arbres d’Éden, les plus beaux et les plus magnifiques du Liban, tous ceux que les eaux abreuvaient. (Sheol )
17 Wale walioishi katika kivuli chake, wale walioungana naye miongoni mwa mataifa, nao pia walikuwa wamezikwa pamoja naye, wakiungana na wale waliouawa kwa upanga. (Sheol )
Ceux-là aussi sont descendus avec lui au schéol, vers les victimes de l’épée, qui étaient son bras et étaient assises à son ombre au milieu des nations. (Sheol )
18 “‘Ni miti ipi ya Edeni inayoweza kulinganishwa nawe kwa fahari na utukufu? Hata hivyo, wewe pia, utashushwa chini pamoja na miti ya Edeni mpaka kuzimu, utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga. “‘Huyu ni Farao pamoja na makundi yake yote ya wajeuri, asema Bwana Mwenyezi.’” ()
Ainsi à qui ressembles-tu en gloire et en grandeur, parmi les arbres d’Éden? Tu seras précipité avec les arbres d’Éden, dans les profondeurs de la terre, pour être couché au milieu d’incirconcis, avec ceux que l’épée a transpercés. Tel sera le sort de Pharaon et de toute sa multitude; — oracle du Seigneur Yahweh. »