< Ezekieli 31 >

1 Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa tatu, siku ya kwanza, neno la Bwana likanijia, kusema:
And it was don in the enleuenthe yeer, in the thridde moneth, in the firste dai of the monethe, the word of the Lord was maad to me,
2 “Mwanadamu, mwambie Farao mfalme wa Misri na makundi yake ya wajeuri: “‘Je, ni nani awezaye kulinganishwa na wewe katika fahari.
and he seide, Thou, sone of man, seie to Farao, kyng of Egipt, and to his puple, To whom art thou maad lijk in thi greetnesse?
3 Angalia Ashuru, wakati fulani ilikuwa mwerezi huko Lebanoni, ukiwa na matawi mazuri ukitia msitu kivuli; ulikuwa mrefu sana, kilele chake kilipita majani ya miti yote.
Lo! Assur as a cedre in Liban, fair in braunchis, and ful of boowis, and hiy bi hiynesse; and his heiyte was reisid among thicke bowis.
4 Maji mengi yaliustawisha, chemchemi zenye maji mengi ziliufanya urefuke; vijito vyake vilitiririka pale ulipoota pande zote na kupeleka mifereji yake kwenye miti yote ya shambani.
Watris nurschiden hym, the depthe of watris enhaunside him; hise floodis fletiden out in the cumpas of hise rootis, and he sente out hise strondis to alle the trees of the cuntrei.
5 Hivyo ukarefuka kupita miti yote ya shambani; vitawi vyake viliongezeka na matawi yake yakawa marefu, yakitanda kwa sababu ya wingi wa maji.
Therfor his hiynesse was enhaunsid ouer alle trees of the cuntrei, and hise trees weren multiplied, and hise braunchis weren reisid, for many watris.
6 Ndege wote wa angani wakaweka viota kwenye vitawi vyake, wanyama wote wa shambani wakazaana chini ya matawi yake, mataifa makubwa yote yaliishi chini ya kivuli chake.
And whanne he hadde stretchid forth his schadewe, alle the volatils of the eir maden nestis in hise braunchis; and alle the beestis of forestis gendriden vndur hise boowis, and the cumpeny of ful many folkis dwellide vndur the schadewynge place of hym.
7 Ulikuwa na fahari katika uzuri, ukiwa na matawi yaliyotanda, kwa kuwa mizizi yake ilikwenda chini mpaka kwenye maji mengi.
And he was ful fair in his greetnesse, and in alargyng of hise trees; for the roote of hym was bisidis many watris.
8 Mierezi katika bustani ya Mungu haikuweza kushindana nao, wala misunobari haikuweza kulingana na vitawi vyake, wala miaramoni haikulinganishwa na matawi yake, wala hakukuwa na mti katika bustani ya Mungu wa kulinganisha na uzuri wake.
Cedris in the paradijs of God weren not hiyere than he; fir trees atteyneden not euenli to the hiynesse of hym, and plane trees weren not euene with the boowis of hym. Ech tree of paradijs of God was not maad lic hym and his fairnesse.
9 Niliufanya kuwa mzuri ukiwa na matawi mengi, ulionewa wivu na miti yote ya Edeni katika bustani ya Mungu.
For Y made hym fair, and with many and thicke boowis; and alle the trees of lust, that weren in the paradijs of God, hadden enuye to hym.
10 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ulikuwa mrefu sana, kilele chake kikiwa juu ya majani manene ya miti na kwa sababu ulikuwa na kiburi cha urefu wake,
Therfor the Lord God seith these thingis, For that that he was reisid in hiynesse, and he yaf his hyynesse greene and thicke, and his herte was reisid in his hiynesse;
11 niliutia mikononi mwa mtawala wa mataifa, ili yeye aushughulikie sawasawa na uovu wake. Nikaukatilia mbali,
now Y haue youe hym in to the hondis of the strongeste man of hethene men. And he doynge schal do to that Assur; aftir the vnfeithfulnesse of hym Y castide hym out.
12 nayo mataifa mageni yaliyo makatili sana yaliukata huo mti na kuuacha. Matawi yake yalianguka juu ya milima na kwenye mabonde yote, vitawi vyake vikavunjika na kusambaa katika makorongo yote ya nchi. Mataifa yote ya duniani yakaondoka kutoka kwenye kivuli chake na kuuacha.
And aliens, and the moost cruel men of naciouns, schulen kitte hym doun, and schulen caste hym forth on hillis. And hise braunchis schulen falle doun in alle grete valeis, and hise trees schulen be brokun in alle roochis of stoon of erthe. And alle the puplis of erthe schulen go awei fro his schadewing place, and schulen forsake hym.
13 Ndege wote wa angani wakakaa kwenye ule mti ulioanguka na wanyama pori wote wakakaa katikati ya vitawi vyake.
Alle volatils of the eir dwelliden in the fallyng of hym, and alle beestis of the cuntrei weren in the braunchis of hym.
14 Kamwe hakutakuwa na miti mingine kando ya hayo maji itakayorefuka zaidi ya huo, vilele vyake vikiwa juu ya majani yote ya miti. Hakuna miti mingine, hata kama imekunywa maji vizuri namna gani, itakayofikia urefu huo. Yote mwisho wake ni kifo, na kuingia ardhini, kama vile ilivyo kwa wanadamu, pamoja na wale waendao shimoni.
Wherfor alle the trees of watris schulen not be reisid in hir hiynesse, nether schulen sette hir hiynesse among places ful of woode, and ful of boowis, and alle trees that ben moistid of watris schulen not stonde in the hiynesse of tho. For alle thei ben youun in to deth, to the ferthest lond in the myddis of the sones of men, to hem that goon doun in to the lake.
15 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mwerezi uliposhushwa chini kaburini nilizifunika chemchemi zenye maji mengi kwa maombolezo: Nilivizuia vijito vyake na wingi wa maji yake nikauzuia. Kwa sababu yake niliivika Lebanoni huzuni, nayo miti yote ya shambani ikanyauka. (Sheol h7585)
The Lord God seith these thingis, In the dai whanne he yede doun to hellis, Y brouyte yn mourenyng; Y hilide hym with depthe of watris, and I forbede his flodis, and Y refreynede many watris. The Liban was sori on him, and alle the trees of the feeld (Sheol h7585)
16 Niliyafanya mataifa yatetemeke kwa kishindo cha kuanguka kwake wakati nilipoushusha chini kaburini pamoja na wale washukao shimoni. Ndipo miti yote ya Edeni, miti iliyo bora kuliko yote na iliyo mizuri sana ya Lebanoni, miti yote ile iliyokunywa maji vizuri, ilifarijika hapa duniani. (Sheol h7585)
weren shakun of the soun of his falling. I mouide togidere hethene men, whanne Y ledde hym doun to helle, with hem that yeden doun in to the lake. And alle trees of likyng, noble trees, and ful cleere in the Liban, alle that weren moistid with watris, weren coumfortid in the loweste lond. (Sheol h7585)
17 Wale walioishi katika kivuli chake, wale walioungana naye miongoni mwa mataifa, nao pia walikuwa wamezikwa pamoja naye, wakiungana na wale waliouawa kwa upanga. (Sheol h7585)
For whi also thei schulen go doun with hym to helle, to slayn men with swerd; and the arm of ech man schal sitte vndur the schadewyng place of hym, in the myddis of naciouns. (Sheol h7585)
18 “‘Ni miti ipi ya Edeni inayoweza kulinganishwa nawe kwa fahari na utukufu? Hata hivyo, wewe pia, utashushwa chini pamoja na miti ya Edeni mpaka kuzimu, utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga. “‘Huyu ni Farao pamoja na makundi yake yote ya wajeuri, asema Bwana Mwenyezi.’” (questioned)
To whom art thou licned, thou noble and hiy among the trees of likyng? Lo! thou art led doun with the trees of likyng to the fertheste lond. In the myddis of vncircumcidid men thou schalt slepe, with hem that ben slayn bi swerd. Thilke is Farao, and al the multitude of hym, seith the Lord God.

< Ezekieli 31 >