< Ezekieli 30 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
Beseda Gospodova je ponovno prišla k meni, rekoč:
2 “Mwanadamu, toa unabii na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ombolezeni ninyi na mseme, “Ole wa siku ile!”
»Človeški sin, prerokuj in reci: ›Tako govori Gospod Bog: ›Tulite: ›Dan, vreden gorja!‹‹
3 Kwa kuwa siku ile imekaribia, siku ya Bwana imekaribia, siku ya mawingu, siku ya maangamizi kwa mataifa.
Kajti dan je blizu, celo Gospodov dan je blizu, oblačen dan; to bo čas poganov.
4 Upanga utakuja dhidi ya Misri, nayo maumivu makuu yataijia Ethiopia. Mauaji yatakapoangukia Misri, utajiri wake utachukuliwa na misingi yake itabomolewa.
Meč bo prišel nad Egipt in velika bolečina bo v Etiopiji, ko bodo umorjeni padli v Egiptu in bodo proč odpeljali njegovo množico in njegovi temelji bodo zrušeni.
5 Kushi na Putu, Ludi na Arabia yote, Libya na watu wa nchi ya Agano watauawa kwa upanga pamoja na Misri.
Etiopija, Libija in Ludéja in vsa pomešana ljudstva in Kub in možje dežele, ki je v zavezi, bodo z njimi padli pod mečem.‹
6 “‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Wale walioungana na Misri wataanguka na kiburi cha nguvu zake kitashindwa. Kutoka Migdoli hadi Aswani, watauawa ndani yake kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.
Tako govori Gospod: ›Tudi tisti, ki podpirajo Egipt, bodo padli; in ponos njegove oblasti se bo zrušil. Od siénskega stolpa bodo v njem padli pod mečem, ‹ govori Gospod Bog.
7 “‘Hizo nchi zitakua ukiwa miongoni mwa nchi zilizo ukiwa, nayo miji yao itakuwa magofu miongoni mwa miji iliyo magofu.
›In opustošeni bodo v sredi dežel, ki so opustošene in njegova mesta bodo v sredi mest, ki so opustošena.
8 Ndipo watakapojua kwamba mimi ndimi Bwana, nitakapoiwasha Misri moto na wote wamsaidiao watapondwa.
In spoznali bodo, da jaz sem Gospod, ko sem dal ogenj v Egipt in ko bodo vsi njegovi pomočniki uničeni.
9 “‘Siku hiyo wajumbe watatoka kwangu kwa merikebu, ili kuwatia hofu Ethiopia, wakiwa katika hali yao ya kuridhika. Maumivu makali yatawapata siku ya maangamizi ya Misri, kwa kuwa hakika itakuja.
Na tisti dan bodo poslanci šli pred menoj na ladjah, da prestrašijo brezskrbne Etiopijce in velika bolečina bo prišla nadnje kakor na dan Egipta, kajti, glej, ta prihaja.‹
10 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Nitakomesha makundi ya wajeuri ya Misri kwa mkono wa Nebukadneza mfalme wa Babeli.
Tako govori Gospod Bog: ›Tudi egiptovski množici bom storil, da odneha po roki babilonskega kralja Nebukadnezarja.
11 Yeye na jeshi lake, taifa lililo katili kuliko mataifa yote, litaletwa ili kuangamiza nchi. Watafuta panga zao dhidi ya Misri na kuijaza nchi kwa waliouawa.
On in njegovo ljudstvo z njim, strašni izmed narodov, bodo privedeni, da uničijo deželo in svoje meče bodo izvlekli zoper Egipt in deželo napolnili z umorjenimi.
12 Nitakausha vijito vya Naili na nitaiuza nchi kwa watu waovu, kwa mkono wa wageni, nitaifanya nchi ukiwa na kila kitu kilichomo ndani yake. Mimi Bwana nimenena haya.
Posušil bom reke in deželo prodal v roko zlobnega, in deželo in vse, kar je v njej, bom naredil opustošenje po roki tujcev. Jaz, Gospod sem to govoril.‹
13 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Nitaangamiza sanamu na kukomesha vinyago katika Memfisi Hapatakuwepo tena na mkuu katika nchi ya Misri, nami nitaeneza hofu katika nchi nzima.
Tako govori Gospod Bog: ›Prav tako bom uničil malike in njihovim podobam bom povzročil, da bodo izginile iz Nofa; in tam ne bo nič več princa iz egiptovske dežele, in na egiptovsko deželo bom položil strah.
14 Nitaifanya Pathrosi kuwa ukiwa na kuitia moto Soani, nami nitaipiga kwa adhabu Thebesi
Patrós bom naredil zapuščen in prižgal bom ogenj na Coanu in izvršil bom sodbe v Noju.
15 Nitaimwaga ghadhabu yangu juu ya Pelusiumu, ngome ya Misri, nami nitakatilia mbali makundi ya wajeuri wa Thebesi.
In svojo razjarjenost bom izlil nad Sin, moč Egipta; in iztrebil bom množico iz Noja.
16 Nitaitia moto nchi ya Misri; Pelusiumu itagaagaa kwa maumivu makuu. Thebesi itachukuliwa na tufani, Memfisi itakuwa katika taabu daima.
Zanetil bom ogenj v Egiptu. Sin bo imel veliko bolečino in No bo raztrgan in Nof bo imel dnevne tegobe.
17 Wanaume vijana wa Oni na wa Pi-Besethi wataanguka kwa upanga nayo hiyo miji itatekwa.
Mladeniči iz Avena in iz Pi Beseta bodo padli pod mečem, in ta mesta bodo šla v ujetništvo.
18 Huko Tahpanhesi mchana utatiwa giza nitakapovunja kongwa la Misri; hapo kiburi cha nguvu zake kitakoma. Atafunikwa na mawingu na vijiji vyake vitatekwa.
Tudi v Tahpanhésu bo dan otemnel, ko bom tam zlomil egiptovske jarme, in pomp njegove moči bo prenehal v njem. Kar se tiče njega, oblak ga bo pokril in njegove hčere bodo šle v ujetništvo.
19 Kwa hiyo nitaipiga Misri kwa adhabu, nao watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
Tako bom izvršil sodbe v Egiptu, in spoznali bodo, da jaz sem Gospod.‹«
20 Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa kwanza, siku ya saba, neno la Bwana likanijia kusema:
In pripetilo se je v enajstem letu, v prvem mesecu, na sedmi dan meseca, da je prišla k meni Gospodova beseda, rekoč:
21 “Mwanadamu, nimevunja mkono wa Farao mfalme wa Misri. Haukufungwa ili upone au kuwekewa kipande cha ubao ili upate nguvu za kuweza kuchukua upanga.
»Človeški sin zlomil sem laket faraonu, egiptovskemu kralju; in glej, ta ne bo obvezan, da bi bil ozdravljen, da položi povoj, da ga poveže, da ga naredi močnega za držanje meča.
22 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume na Farao mfalme wa Misri. Nitavunja mikono yake yote miwili, ule mkono ulio mzima pia na ule uliovunjika na kuufanya upanga uanguke toka mkononi mwake.
Zato tako govori Gospod Bog: ›Glej jaz sem zoper faraona, egiptovskega kralja in zlomil bom njegova lakta, zdravega in tistega, ki je bil zlomljen; in storil bom, da iz njegove roke pade meč.
23 Nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi zote.
Egipčane bom razkropil med narode in jih razpodil po deželah.
24 Nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babeli na kuutia upanga wangu mkononi mwake, lakini nitavunja mikono ya Farao, naye atalia kwa huzuni mbele yake kama mtu aliyetiwa jeraha la kumfisha.
Okrepil pa bom lakte babilonskega kralja in v njegovo roko položim svoj meč. Toda faraonova lakta bom zlomil in pred njim bo stokal s stokanjem smrtno ranjenega moža.
25 Nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babeli, lakini mikono ya Farao italegea. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, nitakapoutia upanga wangu mkononi mwa mfalme wa Babeli, naye ataunyoosha dhidi ya Misri.
Toda okrepil bom lakta babilonskega kralja, faraonova lakta pa bosta upadla in spoznali bodo, da jaz sem Gospod, ko bom svoj meč položil v roko babilonskega kralja in iztegnil ga bo nad egiptovsko deželo.
26 Nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi mbalimbali. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.”
In Egipčane bom razkropil med narode in jih razpodil med dežele; in spoznali bodo, da jaz sem Gospod.‹«