< Ezekieli 30 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
I doszło do mnie słowo PANA mówiące:
2 “Mwanadamu, toa unabii na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ombolezeni ninyi na mseme, “Ole wa siku ile!”
Synu człowieczy, prorokuj i mów: Tak mówi Pan BÓG: Zawódźcie, [mówiąc]: Ach, jakiż to dzień!
3 Kwa kuwa siku ile imekaribia, siku ya Bwana imekaribia, siku ya mawingu, siku ya maangamizi kwa mataifa.
Bliski bowiem jest dzień, bliski jest dzień PANA; będzie to dzień pochmurny i czas pogan.
4 Upanga utakuja dhidi ya Misri, nayo maumivu makuu yataijia Ethiopia. Mauaji yatakapoangukia Misri, utajiri wake utachukuliwa na misingi yake itabomolewa.
I spadnie miecz na Egipt, i będzie wielka trwoga w Etiopii, gdy polegną zabici w Egipcie, gdy zabiorą jego dostatek i jego fundamenty będą zburzone.
5 Kushi na Putu, Ludi na Arabia yote, Libya na watu wa nchi ya Agano watauawa kwa upanga pamoja na Misri.
Etiopia, Put i Lud, cała różnorodna ludność, Kub i mieszkańcy sprzymierzonej ziemi padną [razem] z nimi od miecza.
6 “‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Wale walioungana na Misri wataanguka na kiburi cha nguvu zake kitashindwa. Kutoka Migdoli hadi Aswani, watauawa ndani yake kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.
Tak mówi PAN: Upadną ci, którzy wspierają Egipt, i runie pycha jego mocy. Od wieży Sewene padną w niej od miecza, mówi Pan BÓG.
7 “‘Hizo nchi zitakua ukiwa miongoni mwa nchi zilizo ukiwa, nayo miji yao itakuwa magofu miongoni mwa miji iliyo magofu.
I będą spustoszeni wśród spustoszonych ziem, a ich miasta znajdą się wśród zburzonych miast.
8 Ndipo watakapojua kwamba mimi ndimi Bwana, nitakapoiwasha Misri moto na wote wamsaidiao watapondwa.
I poznają, że ja jestem PANEM, gdy rozpalę ogień w Egipcie, i wszyscy jego pomocnicy zostaną skruszeni.
9 “‘Siku hiyo wajumbe watatoka kwangu kwa merikebu, ili kuwatia hofu Ethiopia, wakiwa katika hali yao ya kuridhika. Maumivu makali yatawapata siku ya maangamizi ya Misri, kwa kuwa hakika itakuja.
W tym dniu posłańcy wyruszą ode mnie w okrętach na postrach spokojnej ziemi Etiopii; i ogarnie ich wielka trwoga, jaka była w dniu [porażki] Egiptu. Oto bowiem nadchodzi.
10 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Nitakomesha makundi ya wajeuri ya Misri kwa mkono wa Nebukadneza mfalme wa Babeli.
Tak mówi Pan BÓG: Położę kres mnóstwu Egiptu przez rękę Nabuchodonozora, króla Babilonu.
11 Yeye na jeshi lake, taifa lililo katili kuliko mataifa yote, litaletwa ili kuangamiza nchi. Watafuta panga zao dhidi ya Misri na kuijaza nchi kwa waliouawa.
On i z nim jego lud, najsrożsi z narodów, będą sprowadzeni, aby zniszczyć tę ziemię. Dobędą swe miecze przeciw Egiptowi i napełnią ziemię pobitymi.
12 Nitakausha vijito vya Naili na nitaiuza nchi kwa watu waovu, kwa mkono wa wageni, nitaifanya nchi ukiwa na kila kitu kilichomo ndani yake. Mimi Bwana nimenena haya.
Wysuszę rzeki i sprzedam ziemię w ręce niegodziwych. Ręką cudzoziemców spustoszę ziemię wraz ze wszystkim, co ją napełnia. Ja, PAN, [to] powiedziałem.
13 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Nitaangamiza sanamu na kukomesha vinyago katika Memfisi Hapatakuwepo tena na mkuu katika nchi ya Misri, nami nitaeneza hofu katika nchi nzima.
Tak mówi Pan BÓG: Zniszczę bożki i usunę posągi z Nof, i nie będzie już księcia w ziemi Egiptu. Ześlę strach na ziemię Egiptu.
14 Nitaifanya Pathrosi kuwa ukiwa na kuitia moto Soani, nami nitaipiga kwa adhabu Thebesi
Spustoszę Patros, rozniecę ogień w Soan i wykonam sąd w No.
15 Nitaimwaga ghadhabu yangu juu ya Pelusiumu, ngome ya Misri, nami nitakatilia mbali makundi ya wajeuri wa Thebesi.
Wyleję swoją zapalczywość na Sin, twierdzę Egiptu, i wytracę tłumy z No.
16 Nitaitia moto nchi ya Misri; Pelusiumu itagaagaa kwa maumivu makuu. Thebesi itachukuliwa na tufani, Memfisi itakuwa katika taabu daima.
Rozniecę ogień w Egipcie, Sin będzie cierpieć z bólu, No zostanie zniszczone i Nof będzie codziennie dręczone.
17 Wanaume vijana wa Oni na wa Pi-Besethi wataanguka kwa upanga nayo hiyo miji itatekwa.
Młodzieńcy z Awen i Pibeset polegną od miecza, te [miasta] pójdą do niewoli.
18 Huko Tahpanhesi mchana utatiwa giza nitakapovunja kongwa la Misri; hapo kiburi cha nguvu zake kitakoma. Atafunikwa na mawingu na vijiji vyake vitatekwa.
W Tachpanches dzień ogarną ciemności, gdy złamię tam jarzma Egiptu, i ustanie w nim pycha jego mocy. Okryje go chmura i jego córki pójdą do niewoli.
19 Kwa hiyo nitaipiga Misri kwa adhabu, nao watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
Tak wykonam sądy nad Egiptem. I poznają, że ja jestem PANEM.
20 Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa kwanza, siku ya saba, neno la Bwana likanijia kusema:
W roku jedenastym, w pierwszym miesiącu, siódmego [dnia miesiąca], doszło do mnie słowo PANA mówiące:
21 “Mwanadamu, nimevunja mkono wa Farao mfalme wa Misri. Haukufungwa ili upone au kuwekewa kipande cha ubao ili upate nguvu za kuweza kuchukua upanga.
Synu człowieczy, złamałem ramię faraona, króla Egiptu, i oto nie będzie ono obwiązane w celu uleczenia ani nie zostanie owinięte bandażami, ani nie będzie związane, by je wzmocnić, aby mogło trzymać miecz.
22 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume na Farao mfalme wa Misri. Nitavunja mikono yake yote miwili, ule mkono ulio mzima pia na ule uliovunjika na kuufanya upanga uanguke toka mkononi mwake.
Dlatego tak mówi Pan BÓG: Oto jestem przeciwko faraonowi, królowi Egiptu, skruszę mu ramiona, zarówno to mocne, jak i to złamane, i wytrącę miecz z jego ręki.
23 Nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi zote.
I rozproszę Egipcjan między narodami, i rozrzucę ich po ziemiach.
24 Nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babeli na kuutia upanga wangu mkononi mwake, lakini nitavunja mikono ya Farao, naye atalia kwa huzuni mbele yake kama mtu aliyetiwa jeraha la kumfisha.
Wzmocnię ramiona króla Babilonu i włożę swój miecz w jego ręce, a ramiona faraona złamię i będzie przed nim stękał, jak stęka śmiertelnie zraniony.
25 Nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babeli, lakini mikono ya Farao italegea. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, nitakapoutia upanga wangu mkononi mwa mfalme wa Babeli, naye ataunyoosha dhidi ya Misri.
Wzmocnię – mówię – ramiona króla Babilonu, a ramiona faraona upadną; i poznają, że ja jestem PANEM, gdy włożę swój miecz w ręce króla Babilonu, aby go wyciągnął na ziemię Egiptu.
26 Nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi mbalimbali. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.”
I rozproszę Egipcjan między narodami, i rozrzucę ich po ziemiach. I poznają, że jestem PANEM.