< Ezekieli 3 >

1 Naye akaniambia, “Mwanadamu, kula kile kilichoko mbele yako, kula huu ukurasa wa kitabu, kisha uende ukaseme na nyumba ya Israeli.”
Et l'esprit me dit: Fils de l'homme, mange ce rouleau et pars, et parle aux fils d'Israël.
2 Ndipo nikafungua kinywa changu, naye akanilisha ule ukurasa wa kitabu.
Et il m'ouvrit la bouche, et il me fit manger le rouleau.
3 Ndipo akaniambia, “Mwanadamu, kula ukurasa huu wa kitabu ninaokupa ujaze tumbo lako.” Kwa hiyo nikaula, ulikuwa mtamu kama asali kinywani mwangu.
Et il me dit: Fils de l'homme, ta bouche mangera, et tes entrailles seront rassasiées de ce rouleau qui t'est donné. Et je le mangeai, et il fut à ma bouche comme du miel le plus doux.
4 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, sasa nenda katika nyumba ya Israeli ukaseme nao maneno yangu.
Et l'esprit me dit: Fils de l'homme, pars et va trouver la maison d'Israël, et répète-leur mes paroles.
5 Hukutumwa kwa taifa lenye maneno ya kutatiza na lugha ngumu, bali kwa nyumba ya Israeli.
Car c'est à la maison d'Israël que je t'envoie, et non à un peuple qui parle une langue inconnue,
6 Sikukutuma kwa mataifa mengi yenye maneno ya kutatiza na lugha ngumu ambao maneno yao hutayaelewa. Hakika ningekutuma kwa watu hao, wangekusikiliza.
Ni à maintes nations parlant d'autres langues, des langues étrangères, difficiles, inintelligibles pour toi; et quand même je t'aurais envoyé à de tels peuples, ils t'écouteraient encore.
7 Lakini nyumba ya Israeli haitakusikiliza kwa kuwa hawako radhi kunisikiliza mimi, kwa kuwa nyumba yote ya Israeli ni wenye vipaji vya nyuso vigumu na mioyo ya ukaidi.
Mais la maison d'Israël ne voudra pas t'écouter; car ils ne veulent pas m'écouter moi-même, parce que toute la maison d'Israël est opiniâtre et a le cœur endurci.
8 Tazama nimefanya uso wako mgumu dhidi ya nyuso zao na kipaji cha uso wako kigumu dhidi ya vipaji vya nyuso zao.
Et voilà que j'ai fait ta face puissante devant leurs faces, et j'affermirai en toi un pouvoir plus fort que leur pouvoir,
9 Kama vile almasi ilivyo ngumu kuliko gumegume, ndivyo nilivyokifanya kipaji cha uso wako. Usiwaogope wala usiwahofu, ijapokuwa ni nyumba ya kuasi.”
Et qui sera toujours plus ferme qu'un rocher. Ne les crains pas, ne tremble pas devant leur visage; car c'est une maison qui m'irrite.
10 Naye akaniambia, “Mwanadamu, sikiliza kwa makini na uyatie moyoni mwako maneno yote nitakayosema nawe.
Et l'esprit me dit: Fils de l'homme, toutes les paroles que je t'ai dites, reçois-les dans ton cœur, entends-les de tes oreilles.
11 Kisha nenda kwa watu wa taifa lako walio uhamishoni, ukaseme nao. Waambie, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenyezi asemavyo,’ kwamba watasikiliza au hawatasikiliza.”
Et pars, va parmi les captifs près des fils de mon peuple; parle-leur et dis: Voici ce que dit le Seigneur; pour voir si par hasard ils t'écouteront, si par hasard ils rentreront en eux-mêmes.
12 Ndipo Roho akaniinua, nikasikia sauti kubwa nyuma yangu ya ngurumo. (Utukufu wa Bwana na utukuzwe katika mahali pa makao yake!)
Et l'esprit me saisit, et j'entendis derrière moi une voix, comme le bruit d'un grand tremblement de terre, disant: Bénie soit la gloire du Seigneur du lieu où il réside.
13 Ilikuwa ni sauti ya mabawa ya wale viumbe hai yakisuguana moja kwa jingine, sauti kama ya ngurumo.
Et je recueillis le bruit des ailes des quatre animaux ailés, battant l'une contre l'autre, et la voix semblable à un tremblement de terre.
14 Ndipo Roho aliponiinua na kunipeleka mbali. Nikaenda nikiwa na uchungu na hasira moyoni mwangu, nao mkono wa Bwana ukiwa juu yangu.
Et l'esprit me souleva, et il me ravit, et je m'en allai soulevé par l'impulsion de mon propre esprit, et la main puissante du Seigneur était sur moi.
15 Nikafika kwa wale watu waliokuwa uhamishoni huko Tel-Abibu karibu na Mto Kebari. Nikakaa miongoni mwao kwa muda wa siku saba, nikiwa nimejawa na mshangao.
Et je traversai l'air, et j'arrivai parmi les captifs, et je parcourus les demeures de ceux qui étaient sur le fleuve Chobar. Et je restai là sept jours, allant et venant au milieu d'eux.
16 Mwishoni mwa hizo siku saba neno la Bwana likanijia kusema:
Et après sept jours la parole du Seigneur me vint, disant:
17 “Mwanadamu, nimekufanya uwe mlinzi wa nyumba ya Israeli, kwa hiyo sikia neno nisemalo, ukawape onyo litokalo kwangu.
Fils de l'homme, je t'ai mis en sentinelle parmi la maison d'Israël, et tu entendras la parole de ma bouche, et tu les menaceras en mon nom.
18 Nimwambiapo mtu mwovu, ‘Hakika utakufa,’ na wewe usipomwonya mtu huyo au kumshauri aache njia zake mbaya ili kuokoa maisha yake, huyo mtu mwovu atakufa katika dhambi yake na damu yake nitaidai mkononi mwako.
Quand tu diras de ma part à l'impie: Tu mourras de mort; si tu ne lui enjoins pas de faire effort sur lui-même pour se détourner de ses voies afin qu'il vive, cet impie mourra dans son iniquité, et je réclamerai son sang de ta main.
19 Lakini ukimwonya mtu mwovu naye akakataa kuacha uovu wake na njia zake mbaya, atakufa katika dhambi yake, lakini wewe utakuwa umejiokoa nafsi yako.
Mais si tu as averti l'impie, et qu'il ne se soit détourné ni de son impiété ni de sa voie, cet impie mourra dans son iniquité, et toi tu auras sauvé ton âme.
20 “Tena, mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda maovu, nami nikaweka kikwazo mbele yake mtu huyo atakufa. Kwa kuwa hukumwonya, atakufa katika dhambi yake. Mambo ya haki aliyotenda, hayatakumbukwa, damu yake nitaidai mkononi mwako.
Et quand le juste se détournera de la justice et fera une faute, je lui mettrai le châtiment devant la face; et il mourra parce que tu ne l'auras point averti; et il mourra dans ses péchés; car je ne garderai plus la mémoire de ses actes de justice, et je réclamerai son sang de ta main.
21 Lakini ukimwonya mwenye haki asitende dhambi na akaacha kutenda dhambi, hakika ataishi kwa sababu alipokea maonyo na utakuwa umejiokoa nafsi yako.”
Mais si tu as enjoint au juste de ne pas pécher, et s'il ne pèche plus, le juste vivra, parce que tu l'auras averti, et toi tu auras sauvé ton âme.
22 Mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu huko, naye akaniambia, “Simama uende mpaka sehemu tambarare, nami nitasema nawe huko.”
Et la main du Seigneur vint sur moi, et il me dit: Lève-toi, et sors dans la plaine, et là il te sera parlé.
23 Kwa hiyo niliinuka nikaenda mpaka mahali pa tambarare. Utukufu wa Bwana ulikuwa umesimama huko, kama utukufu ule niliouona kando ya Mto Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
Et je me levai et je sortis dans la plaine, et voilà que la gloire du Seigneur s'y tenait, pareille à la vision et à la gloire du Seigneur que j'avais vue sur le fleuve Chobar. Et je tombai la face contre terre.
24 Ndipo Roho akaja ndani yangu akanisimamisha kwa miguu yangu. Akasema nami akaniambia: “Nenda ukajifungie ndani ya nyumba yako.
Et un esprit vint en moi, et il me remit sur mes pieds, et il parla et me dit: Rentre, et enferme-toi au milieu de ta maison.
25 Nawe, ee mwanadamu, watakufunga kwa kamba, watakufunga ili usiweze kutoka na kuwaendea watu.
Et toi, fils de l'homme, voilà que des chaînes sont préparées pour toi, et ils te chargeront de ces chaînes, et tu n'en sortiras point.
26 Nitaufanya ulimi wako ushikamane kwenye kaa la kinywa chako, ili uwe kimya usiweze kuwakemea, wajapokuwa ni nyumba ya kuasi.
Et je te nouerai la langue, et tu seras muet, et tu ne seras plus pour eux un reproche vivant; car c'est une maison qui m'irrite.
27 Lakini nitakaposema nawe, nitafungua kinywa chako nawe utawaambia, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo.’ Yeyote atakayesikiliza na asikilize, na yeyote atakayekataa na akatae; kwa kuwa wao ni nyumba ya kuasi.
Mais quand je t'aurai parlé, je t'ouvrirai la bouche et tu leur diras: Voilà ce que dit le Seigneur: Que celui qui vaut écouter écoute; que celui qui veut désobéir désobéisse; car c'est une maison qui m'irrite.

< Ezekieli 3 >