< Ezekieli 29 >

1 Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya kumi na mbili, neno la Bwana likanijia kusema:
La dixième année, au dixième mois, le douzième jour du mois, la parole de l'Éternel me fut adressée en ces termes:
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Farao mfalme wa Misri na utabiri dhidi yake na dhidi ya Misri yote.
« Fils d'homme, tourne ta face vers Pharaon, roi d'Égypte, et prophétise contre lui et contre toute l'Égypte.
3 Nena, nawe useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Mimi ni kinyume nawe, Farao, mfalme wa Misri, joka kubwa ulalaye katikati ya vijito vyako. Unasema, “Mto Naili ni wangu mwenyewe; niliufanya kwa ajili yangu mwenyewe.”
Parle et dis: Le Seigneur Yahvé dit: « Voici, je suis contre toi, Pharaon, roi d'Égypte, le grand monstre qui se trouve au milieu de ses rivières, qui a dit: « Mon fleuve est à moi », et je l'ai fait pour moi.
4 Lakini nitatia ndoana katika mataya yako nami nitawafanya samaki wa vijito vyako washikamane na magamba yako. Nitakutoa katikati ya vijito vyako, pamoja na samaki wote walioshikamana na magamba yako.
Je mettrai des crochets dans vos mâchoires, et je ferai en sorte que les poissons de vos rivières se collent à vos écailles. Je vous ferai sortir du milieu de vos rivières, avec tous les poissons de vos rivières qui s'accrochent à vos écailles.
5 Nitakutupa jangwani, wewe pamoja na samaki wote wa vijito vyako. Utaanguka uwanjani, nawe hutakusanywa au kuchukuliwa. Nitakutoa uwe chakula kwa wanyama wa nchi na ndege wa angani.
Je te jetterai dans le désert, vous et tous les poissons de vos rivières. Tu vas tomber sur le champ libre. Vous ne serez pas réunis ou rassemblés. Je vous ai donné en nourriture aux animaux de la terre. et aux oiseaux du ciel.
6 Ndipo wale wote waishio Misri watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Umekuwa fimbo ya tete kwa nyumba ya Israeli.
"''Tous les habitants de l'Égypte sauront que je suis Yahvé, parce qu'ils ont été un bâton de roseau pour la maison d'Israël.
7 Walipokushika kwa mikono yao, ulivunjika na kuchana mabega yao; walipokuegemea, ulivunjika na migongo yao ikateguka.
Quand ils t'ont saisi par la main, tu as brisé et déchiré toutes leurs épaules. Quand ils se sont appuyés sur toi, tu as brisé et paralysé toutes leurs cuisses. »
8 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaleta upanga juu yako na kuua watu wako na wanyama wao.
"'C'est pourquoi le Seigneur Yahvé dit: « Voici que je fais venir sur vous l'épée, et j'extermine de vous hommes et bêtes.
9 Misri itakuwa ukiwa na isiyolimwa wala kukaliwa na watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Kwa sababu ulisema, “Mto Naili ni wangu; mimi niliufanya,”
Le pays d'Égypte sera une désolation et un désert. Alors ils sauront que je suis Yahvé. "" Parce qu'il a dit: Le fleuve est à moi, et c'est moi qui l'ai fait »,
10 kwa hiyo mimi ni kinyume nawe na kinyume na vijito vyako, nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa magofu na ukiwa isiyolimwa wala kukaliwa na watu kuanzia Migdoli hadi Aswani, hata kufikia mpakani wa Ethiopia.
voici que j'en veux à toi et à tes fleuves. Je ferai du pays d'Égypte un désert et une désolation totale, depuis la tour de Seveneh jusqu'à la frontière de l'Éthiopie.
11 Hakuna unyayo wa mtu au mnyama utakaopita ndani yake, wala hakuna yeyote atakayeishi humo kwa muda wa miaka arobaini.
Aucun pied d'homme n'y passera, aucun pied d'animal n'y passera. Il ne sera pas habité pendant quarante ans.
12 Nitaifanya nchi ya Misri ukiwa, miongoni mwa nchi zilizo ukiwa, nayo miji yake itabaki ukiwa miaka arobaini miongoni mwa miji iliyo magofu. Nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi nyingine.
Je ferai du pays d'Égypte une désolation au milieu des pays qui sont désolés. Ses villes au milieu des villes dévastées seront une désolation pendant quarante ans. Je disperserai les Égyptiens parmi les nations, je les disperserai à travers les pays. »
13 “‘Lakini hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mwishoni mwa hiyo miaka arobaini, nitawakusanya Wamisri kutoka mataifa walikotawanywa.
"'Car le Seigneur Yahvé dit: « Au bout de quarante ans, je rassemblerai les Égyptiens des peuples où ils ont été dispersés.
14 Nitawarudisha hao Wamisri kutoka kwenye kutekwa kwao na kuwaweka katika Pathrosi, nchi ya baba zao. Huko watakuwa na ufalme usiokuwa na nguvu.
Je renverserai la captivité de l'Égypte et je les ferai retourner dans le pays de Pathros, dans le pays de leur naissance. Là, ils formeront un royaume modeste.
15 Utakuwa ufalme dhaifu kuliko zote na kamwe Misri haitajikweza tena juu ya mataifa mengine. Nitaufanya ufalme wake dhaifu sana kiasi kwamba kamwe hautatawala tena juu ya mataifa mengine.
Il sera le plus bas des royaumes. Il ne s'élèvera plus au-dessus des nations. Je les diminuerai au point qu'ils ne domineront plus sur les nations.
16 Misri haitakuwa tena tumaini la watu wa Israeli bali itakuwa kumbukumbu ya dhambi yao kwa kuigeukia kuomba msaada. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’”
Il ne sera plus l'assurance de la maison d'Israël, rappelant l'iniquité, quand on se tourne vers lui. Alors ils sauront que je suis le Seigneur Yahvé. »'"
17 Katika mwaka wa ishirini na saba, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza, neno la Bwana likanijia, kusema:
La vingt-septième année, le premier jour du mois, la parole de l'Éternel me fut adressée, en ces mots:
18 “Mwanadamu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliongoza jeshi lake kufanya kazi ngumu dhidi ya Tiro; kila kichwa kilipata upaa na kila bega likachunika. Lakini yeye na jeshi lake hawakupata malipo yoyote kutokana na muda wote aliongoza hiyo vita dhidi ya Tiro.
« Fils d'homme, Nebucadnetsar, roi de Babylone, a fait faire à son armée un grand service contre Tyr. Toutes les têtes étaient chauves, et toutes les épaules étaient usées; mais il n'a pas reçu de salaire, ni son armée de Tyr, pour le service qu'il a fait contre elle.
19 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaitia Misri mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atachukua utajiri wa Misri. Atateka mateka na kuchukua nyara mali za Misri kama ujira kwa ajili ya jeshi lake.
C'est pourquoi le Seigneur Yahvé dit: « Voici que je donne le pays d'Égypte à Nabuchodonosor, roi de Babylone. Il enlèvera sa multitude, prendra son pillage et son butin. Ce sera le salaire de son armée.
20 Nimempa mfalme wa Babeli nchi ya Misri kuwa ujira kwa juhudi zake kwa sababu yeye na jeshi lake walifanya kwa ajili yangu, asema Bwana Mwenyezi.
Je lui ai donné le pays d'Égypte en paiement de son service, parce qu'ils ont travaillé pour moi, dit le Seigneur Yahvé.
21 “Katika siku hiyo nitaifanya nyumba ya Israeli iwe na nguvu nami nitakifungua kinywa chako miongoni mwao. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.”
« En ce jour-là, je ferai germer une corne pour la maison d'Israël, et j'ouvrirai ta bouche au milieu d'eux. Alors ils sauront que je suis Yahvé. »

< Ezekieli 29 >