< Ezekieli 29 >

1 Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya kumi na mbili, neno la Bwana likanijia kusema:
In the tenth year, in the tenth month, in the twelfth day of the month, the word of Jehovah came to me, saying:
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Farao mfalme wa Misri na utabiri dhidi yake na dhidi ya Misri yote.
Son of man, set thy face against Pharaoh, the king of Egypt, and prophesy against him, and against all Egypt;
3 Nena, nawe useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Mimi ni kinyume nawe, Farao, mfalme wa Misri, joka kubwa ulalaye katikati ya vijito vyako. Unasema, “Mto Naili ni wangu mwenyewe; niliufanya kwa ajili yangu mwenyewe.”
Speak, and say, Thus saith the Lord Jehovah: Behold, I am against thee, Pharaoh, king of Egypt, thou great dragon, that liest in the midst of thy rivers, and sayest, “My river is my own, and I have made it for myself.”
4 Lakini nitatia ndoana katika mataya yako nami nitawafanya samaki wa vijito vyako washikamane na magamba yako. Nitakutoa katikati ya vijito vyako, pamoja na samaki wote walioshikamana na magamba yako.
And I will put hooks in thy jaws, and I will cause the fish of thy rivers to cleave to thy scales, and I will draw thee forth from the midst of thy rivers, and all the fish of thy rivers which cleave to thy scales.
5 Nitakutupa jangwani, wewe pamoja na samaki wote wa vijito vyako. Utaanguka uwanjani, nawe hutakusanywa au kuchukuliwa. Nitakutoa uwe chakula kwa wanyama wa nchi na ndege wa angani.
And I will cast thee into the desert, thee and all the fish of thy rivers; thou shalt fall upon the open fields; thou shalt not be brought together, nor gathered; to the beasts of the field and the birds of heaven I have given thee for food.
6 Ndipo wale wote waishio Misri watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Umekuwa fimbo ya tete kwa nyumba ya Israeli.
And all the inhabitants of Egypt shall know that I am Jehovah; because they have been a staff of reed to the house of Israel.
7 Walipokushika kwa mikono yao, ulivunjika na kuchana mabega yao; walipokuegemea, ulivunjika na migongo yao ikateguka.
When they took hold of thee by thy handle, thou didst break and pierce their whole shoulder; and when they leaned upon thee, thou didst go to pieces, and madest all their loins to shake.
8 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaleta upanga juu yako na kuua watu wako na wanyama wao.
Therefore thus saith the Lord Jehovah: Behold, I will bring a sword upon thee, and cut off man and beast out of thee;
9 Misri itakuwa ukiwa na isiyolimwa wala kukaliwa na watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Kwa sababu ulisema, “Mto Naili ni wangu; mimi niliufanya,”
and the land of Egypt shall be desolate and waste; and they shall know that I am Jehovah, because he hath said, “The river is mine, and I have made it.”
10 kwa hiyo mimi ni kinyume nawe na kinyume na vijito vyako, nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa magofu na ukiwa isiyolimwa wala kukaliwa na watu kuanzia Migdoli hadi Aswani, hata kufikia mpakani wa Ethiopia.
Therefore, behold, I am against thee, and against thy rivers; and I will make the land of Egypt utterly waste and desolate, from Migdol even to Syene, and to the borders of Ethiopia.
11 Hakuna unyayo wa mtu au mnyama utakaopita ndani yake, wala hakuna yeyote atakayeishi humo kwa muda wa miaka arobaini.
There shall not pass through it the foot of man, and the foot of beast shall not pass through it, neither shall it be inhabited forty years.
12 Nitaifanya nchi ya Misri ukiwa, miongoni mwa nchi zilizo ukiwa, nayo miji yake itabaki ukiwa miaka arobaini miongoni mwa miji iliyo magofu. Nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi nyingine.
I will make the land of Egypt desolate amidst the lands that are desolate, and her cities, among the cities that are laid waste, shall be desolate forty years; and I will scatter the Egyptians among the nations, and will disperse them through the countries.
13 “‘Lakini hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mwishoni mwa hiyo miaka arobaini, nitawakusanya Wamisri kutoka mataifa walikotawanywa.
Yet thus saith the Lord Jehovah: At the end of forty years will I gather the Egyptians from the nations whither they are scattered;
14 Nitawarudisha hao Wamisri kutoka kwenye kutekwa kwao na kuwaweka katika Pathrosi, nchi ya baba zao. Huko watakuwa na ufalme usiokuwa na nguvu.
and I will bring back the captives of Egypt, and will cause them to return into the land of Pathros, into the land of their origin; and they shall be there a mean kingdom;
15 Utakuwa ufalme dhaifu kuliko zote na kamwe Misri haitajikweza tena juu ya mataifa mengine. Nitaufanya ufalme wake dhaifu sana kiasi kwamba kamwe hautatawala tena juu ya mataifa mengine.
it shall be the meanest of all kingdoms; it shall no more exalt itself above the nations; for I will diminish them, that they shall no more rule over the nations.
16 Misri haitakuwa tena tumaini la watu wa Israeli bali itakuwa kumbukumbu ya dhambi yao kwa kuigeukia kuomba msaada. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’”
And it shall be no more the confidence of the house of Israel, bringing to my remembrance their iniquity in looking to them for help; and they shall know that I am the Lord Jehovah.
17 Katika mwaka wa ishirini na saba, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza, neno la Bwana likanijia, kusema:
And it came to pass in the twenty-seventh year, in the first month, on the first day of the month, that the word of Jehovah came to me, saying:
18 “Mwanadamu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliongoza jeshi lake kufanya kazi ngumu dhidi ya Tiro; kila kichwa kilipata upaa na kila bega likachunika. Lakini yeye na jeshi lake hawakupata malipo yoyote kutokana na muda wote aliongoza hiyo vita dhidi ya Tiro.
Son of man, Nebuchadnezzar, the king of Babylon, caused his army to serve a great service against Tyre; every head was made bald, and every shoulder was peeled; yet neither he nor his army had wages from Tyre for the service which he served against it.
19 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaitia Misri mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atachukua utajiri wa Misri. Atateka mateka na kuchukua nyara mali za Misri kama ujira kwa ajili ya jeshi lake.
Therefore thus saith the Lord Jehovah: Behold, I will give the land of Egypt to Nebuchadnezzar, the king of Babylon, and he shall take her multitude, and take her spoil, and take her plunder; and it shall be wages for his army.
20 Nimempa mfalme wa Babeli nchi ya Misri kuwa ujira kwa juhudi zake kwa sababu yeye na jeshi lake walifanya kwa ajili yangu, asema Bwana Mwenyezi.
For his wages for his service I will give him the land of Egypt; for they wrought for me, saith the Lord Jehovah.
21 “Katika siku hiyo nitaifanya nyumba ya Israeli iwe na nguvu nami nitakifungua kinywa chako miongoni mwao. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.”
In that day will I cause a horn to grow forth to the house of Israel, and I will give thee to open the mouth in the midst of them; and they shall know that I am Jehovah.

< Ezekieli 29 >