< Ezekieli 29 >
1 Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya kumi na mbili, neno la Bwana likanijia kusema:
In the tenth year, in the tenth month, on the eleventh day of the month, the word of the Lord came to me, saying:
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Farao mfalme wa Misri na utabiri dhidi yake na dhidi ya Misri yote.
“Son of man, set your face against Pharaoh, the king of Egypt, and you shall prophesy about him and about all of Egypt.
3 Nena, nawe useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Mimi ni kinyume nawe, Farao, mfalme wa Misri, joka kubwa ulalaye katikati ya vijito vyako. Unasema, “Mto Naili ni wangu mwenyewe; niliufanya kwa ajili yangu mwenyewe.”
Speak, and you shall say: Thus says the Lord God: Behold, I am against you, Pharaoh, king of Egypt, you great dragon, who rests in the midst of your rivers. And you say: ‘Mine is the river, and I have made myself.’
4 Lakini nitatia ndoana katika mataya yako nami nitawafanya samaki wa vijito vyako washikamane na magamba yako. Nitakutoa katikati ya vijito vyako, pamoja na samaki wote walioshikamana na magamba yako.
But I will place a bridle in your jaws. And I will adhere the fish of your rivers to your scales. And I will draw you out of the midst of your rivers, and all your fish will adhere to your scales.
5 Nitakutupa jangwani, wewe pamoja na samaki wote wa vijito vyako. Utaanguka uwanjani, nawe hutakusanywa au kuchukuliwa. Nitakutoa uwe chakula kwa wanyama wa nchi na ndege wa angani.
And I will cast you into the desert, with all the fish of your river. You will fall upon the surface of the earth; you will not be taken up, nor gathered together. I have given you to the beasts of the earth and to the birds of the air, to be devoured.
6 Ndipo wale wote waishio Misri watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Umekuwa fimbo ya tete kwa nyumba ya Israeli.
And all the inhabitants of Egypt shall know that I am the Lord. For you have been a staff made of reed to the house of Israel.
7 Walipokushika kwa mikono yao, ulivunjika na kuchana mabega yao; walipokuegemea, ulivunjika na migongo yao ikateguka.
When they took hold of you with the hand, you broke, and so you wounded all of their shoulders. And when they leaned on you, you shattered, and so you injured all of their lower backs.
8 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaleta upanga juu yako na kuua watu wako na wanyama wao.
Because of this, thus says the Lord God: Behold, I will lead the sword over you, and I will destroy both man and beast from among you.
9 Misri itakuwa ukiwa na isiyolimwa wala kukaliwa na watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Kwa sababu ulisema, “Mto Naili ni wangu; mimi niliufanya,”
And the land of Egypt will be a desert and a wilderness. And they shall know that I am the Lord. For you have said, ‘The river is mine, and I have made it.’
10 kwa hiyo mimi ni kinyume nawe na kinyume na vijito vyako, nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa magofu na ukiwa isiyolimwa wala kukaliwa na watu kuanzia Migdoli hadi Aswani, hata kufikia mpakani wa Ethiopia.
Therefore, behold, I am against you and against your rivers. And I will make the land of Egypt into a wilderness, destroyed by the sword from the tower of Syene all the way to the borders of Ethiopia.
11 Hakuna unyayo wa mtu au mnyama utakaopita ndani yake, wala hakuna yeyote atakayeishi humo kwa muda wa miaka arobaini.
The foot of man will not pass through it, and the foot of cattle will not walk in it. And it will be uninhabited for forty years.
12 Nitaifanya nchi ya Misri ukiwa, miongoni mwa nchi zilizo ukiwa, nayo miji yake itabaki ukiwa miaka arobaini miongoni mwa miji iliyo magofu. Nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi nyingine.
And I will set the land of Egypt in desolation, in the midst of desolate lands, and its cities in the midst of overturned cites. And they will be desolate for forty years. And I will scatter the Egyptians among the nations, and I will disperse them among the lands.
13 “‘Lakini hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mwishoni mwa hiyo miaka arobaini, nitawakusanya Wamisri kutoka mataifa walikotawanywa.
For thus says the Lord God: After the end of forty years, I will gather the Egyptians from the peoples among whom they had been scattered.
14 Nitawarudisha hao Wamisri kutoka kwenye kutekwa kwao na kuwaweka katika Pathrosi, nchi ya baba zao. Huko watakuwa na ufalme usiokuwa na nguvu.
And I will lead back the captivity of Egypt, and I will collect them in the land of Pathros, in the land of their nativity. And in that place, they will be a lowly kingdom.
15 Utakuwa ufalme dhaifu kuliko zote na kamwe Misri haitajikweza tena juu ya mataifa mengine. Nitaufanya ufalme wake dhaifu sana kiasi kwamba kamwe hautatawala tena juu ya mataifa mengine.
It will be the lowest among the other kingdoms, and it will no longer be exalted above the nations. And I will diminish them, lest they rule over the Gentiles.
16 Misri haitakuwa tena tumaini la watu wa Israeli bali itakuwa kumbukumbu ya dhambi yao kwa kuigeukia kuomba msaada. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’”
And they will no longer be the confidence of the house of Israel, teaching iniquity, so that they may flee and follow them. And they shall know that I am the Lord God.”
17 Katika mwaka wa ishirini na saba, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza, neno la Bwana likanijia, kusema:
And it happened that, in the twenty-seventh year, in the first month, on the first of the month, the word of the Lord came to me, saying:
18 “Mwanadamu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliongoza jeshi lake kufanya kazi ngumu dhidi ya Tiro; kila kichwa kilipata upaa na kila bega likachunika. Lakini yeye na jeshi lake hawakupata malipo yoyote kutokana na muda wote aliongoza hiyo vita dhidi ya Tiro.
“Son of man, Nebuchadnezzar, the king of Babylon, has caused his army to serve with great servility against Tyre. Every head was shaven, and every shoulder was stripped of hair. And wages have not been paid to him, nor to his army, for Tyre, for the service by which he served for me against it.
19 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaitia Misri mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atachukua utajiri wa Misri. Atateka mateka na kuchukua nyara mali za Misri kama ujira kwa ajili ya jeshi lake.
Because of this, thus says the Lord God: Behold, I will station Nebuchadnezzar, the king of Babylon, in the land of Egypt. And he will take its multitude, and he will prey upon its profits, and he will plunder its spoils. And this shall be the wages for his army
20 Nimempa mfalme wa Babeli nchi ya Misri kuwa ujira kwa juhudi zake kwa sababu yeye na jeshi lake walifanya kwa ajili yangu, asema Bwana Mwenyezi.
and for the work by which he has served against it. I have given to him the land of Egypt, because he has labored for me, says the Lord God.
21 “Katika siku hiyo nitaifanya nyumba ya Israeli iwe na nguvu nami nitakifungua kinywa chako miongoni mwao. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.”
In that day, a horn will spring forth for the house of Israel, and I will give to you an open mouth in their midst. And they shall know that I am the Lord.”