< Ezekieli 28 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
HERRENS Ord kom til mig saaledes:
2 “Mwanadamu, mwambie mfalme wa Tiro, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Kwa sababu moyo wako umejivuna na umesema, “Mimi ni mungu; nami ninaketi katika kiti cha enzi cha mungu katika moyo wa bahari.” Lakini wewe ni mwanadamu, wala si mungu, ingawa unafikiri kuwa una hekima kama mungu.
Menneskesøn, sig til Tyrus's Fyrste: Saa siger den Herre HERREN: Fordi dit Hjerte hovmoder sig og du siger: »Jeg er en Gud, paa et Gudesæde sidder jeg midt ude i Havet!« skønt du er et Menneske og ingen Gud, og fordi du føler dig i Hjertet som en Gud;
3 Je, wewe una hekima kuliko Danieli? Je, hakuna siri iliyofichika kwako?
se, du er visere end Daniel, ingen Vismand maaler sig med dig;
4 Kwa hekima yako na ufahamu wako, umejipatia utajiri, nawe umejikusanyia dhahabu na fedha katika hazina zako.
ved din Visdom og indsigt vandt du dig Rigdom og samlede dig Guld og Sølv i dine Skatkamre;
5 Kwa werevu wako mwingi katika biashara, umeongeza utajiri wako na kwa sababu ya utajiri wako moyo wako umekuwa na kiburi.
ved dit store Handelssnilde øgede du din Rigdom, saa dit Hjerte hovmodede sig over den —
6 “‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Kwa sababu unafikiri una hekima, mwenye hekima kama mungu,
derfor, saa siger den Herre HERREN: Fordi du i dit Hjerte føler dig som en Gud,
7 mimi nitawaleta wageni dhidi yako, taifa katili kuliko yote; watafuta panga zao dhidi ya uzuri wa hekima yako, na kuchafua fahari yako inayongʼaa.
se, derfor bringer jeg fremmede over dig, de grummeste Folk, og de skal drage deres Sværd mod din skønne Visdom og vanhellige din Glans.
8 Watakushusha chini shimoni, nawe utakufa kifo cha kikatili katika moyo wa bahari.
De skal styrte dig i Graven, og du skal dø de ihjelslagnes Død i Havets Dyb.
9 Je, wakati huo utasema, “Mimi ni mungu,” mbele ya wale wanaokuua? Utakuwa mwanadamu tu, wala si mungu, mikononi mwa hao wanaokuua.
Mon du da Ansigt til Ansigt med dem, der dræber dig, vil sige: »Jeg er en Gud!« du, som i deres Haand, der slaar dig ihjel, er et Menneske og ikke en Gud.
10 Utakufa kifo cha wasiotahiriwa kwa mkono wa wageni. Kwa kuwa mimi nimenena, asema Bwana Mwenyezi.’”
De uomskaarnes Død skal du dø for fremmedes Haand, saa sandt jeg har talet, lyder det fra den Herre HERREN.
11 Neno la Bwana likanijia kusema:
Og HERRENS Ord kom til mig saaledes:
12 “Mwanadamu, mfanyie maombolezo mfalme wa Tiro, nawe umwambie: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ulikuwa kipeo cha ukamilifu, ukiwa umejaa hekima na mkamilifu katika uzuri.
Menneskesøn, istem en Klagesang over Kongen af Tyrus og sig til ham: Saa siger den Herre HERREN: Du var Indsigtens Segl, fuld af Visdom og fuldkommen i Skønhed.
13 Ulikuwa ndani ya Edeni, bustani ya Mungu; kila kito cha thamani kilikupamba: akiki nyekundu, yakuti manjano na zumaridi, krisolitho, shohamu na yaspi, yakuti samawi, almasi na zabarajadi. Kuwekwa kwa hayo mapambo na kushikizwa kwake kulifanywa kwa dhahabu; siku ile ulipoumbwa yaliandaliwa tayari.
I Eden, Guds Have, var du; alle Slags Ædelsten var din Klædning, Karneol, Topas, Jaspis, Krysolit, Sjoham, Onyks, Safir, Rubin, Smaragd og Guld var paa dig i indfattet og indlagt Arbejde; det var til Rede, den Dag du skabtes.
14 Ulitiwa mafuta kuwa kerubi mlinzi, kwa kuwa hivyo ndivyo nilivyokuweka wakfu. Ulikuwa kwenye mlima mtakatifu wa Mungu; ulitembea katikati ya vito vya moto.
Du var en salvet, skærmende Kerub; jeg gjorde dig dertil; paa det hellige Gudebjerg var du; du vandrede imellem Guds Sønner.
15 Ulikuwa mnyofu katika njia zako tangu siku ile ya kuumbwa kwako, hadi uovu ulipoonekana ndani yako.
Fuldkommen var du i din Færd, fra den Dag du skabtes, indtil der fandtes Brøde hos dig.
16 Kutokana na biashara yako iliyoenea, ulijazwa na dhuluma, nawe ukatenda dhambi. Hivyo nilikuondoa kwa aibu kutoka mlima wa Mungu, nami nikakufukuza, ee kerubi mlinzi, kutoka katikati ya vito vya moto.
Ved din megen Handel fyldte du dit Indre med Uret og forbrød dig; da vanhelligede jeg dig og viste dig bort fra Gudebjerget og tilintetgjorde dig, skærmende Kerub, saa du ikke blev mellem Guds Sønner.
17 Moyo wako ukawa na kiburi kwa ajili ya uzuri wako, nawe ukaiharibu hekima yako kwa sababu ya fahari yako. Kwa hiyo nikakutupa chini; nimekufanya kioja mbele ya wafalme.
Dit Hjerte hovmodede sig over din Skønhed, du satte din Visdom til paa Grund af din Glans. Jeg, slængte dig til Jorden og overgav dig til Konger, at de skulde nyde Skuet af dig.
18 Kwa dhambi zako nyingi na biashara yako ya dhuluma, umenajisi mahali pako patakatifu. Kwa hiyo nilifanya moto utoke ndani yako, nao ukakuteketeza, nami nikakufanya majivu juu ya nchi, machoni pa wote waliokuwa wakitazama.
Med dine mange Misgerninger, ved din uredelige Handel vanhelligede du dine Helligdomme. Da lod jeg Ild bryde løs i din Midte, og den fortærede dig; jeg gjorde dig til Støv paa Jorden for alle, som saa dig.
19 Mataifa yote yaliyokujua yanakustajabia; umefikia mwisho wa kutisha na hutakuwepo tena milele.’”
Alle blandt Folkeslagene, der kendte dig, stivnede af Skræk over dig; du blev en Rædsel, og borte er du for evigt.
20 Neno la Bwana likanijia kusema:
HERRENS Ord kom til mig saaledes:
21 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Sidoni, ukatabiri dhidi yake,
Menneskesøn, vend dit Ansigt mod Zidon og profeter imod det
22 nawe useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Mimi ni kinyume chako, ee Sidoni, nami nitapata utukufu ndani yako. Nao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana, nitakapotekeleza hukumu zangu na kuonyesha utakatifu wangu ndani yake.
og sig: Saa siger den Herre HERREN: Se, jeg kommer over dig, Zidon, og herliggør mig paa dig; og du skal kende, at jeg er HERREN, naar jeg holder Dom over dig og viser min Hellighed paa dig.
23 Nitapeleka tauni ndani yake na kufanya damu itiririke katika barabara zake. Waliochinjwa wataanguka ndani yake, kwa upanga dhidi yake kila upande. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.
Jeg sender Pest over dig og Blod i dine Gader; ihjelslagne Mænd skal segne i din Midte for Sværd, der er rettet imod dig fra alle Sider; og du skal kende, at jeg er HERREN.
24 “‘Nyumba ya Israeli hawatakuwa tena na majirani wenye nia ya kuwadhuru wanaoumiza kama michongoma na miiba mikali. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.
Fremtidig skal der ikke være nogen Tidsel til at saare eller Torn til at stikke Israels Hus blandt alle dets Naboer, som nu haaner dem; og de skal kende, at jeg er den Herre HERREN.
25 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitakapoikusanya nyumba ya Israeli kutoka mataifa ambako wametawanyika, nitajionyesha kuwa mtakatifu miongoni mwao machoni pa mataifa. Ndipo watakapoishi katika nchi yao wenyewe, niliyompa mtumishi wangu Yakobo.
Saa siger den Herre HERREN: Naar jeg samler Israels Slægt fra de Folkeslag, de er spredt iblandt, vil jeg hellige mig paa dem for Folkenes Øjne, og de skal bo i deres Land, som jeg gav min Tjener Jakob;
26 Wataishi humo kwa salama na watajenga nyumba na kupanda mashamba ya mizabibu, wataishi kwa salama nitakapowaadhibu majirani zao wote ambao waliwafanyia uovu. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, Mungu wao.’”
de skal bo trygt deri, bygge Huse og plante Vingaarde, ja bo trygt, medens jeg holder Dom over alle dem, der haaner dem fra alle Sider; og de skal kende, at jeg er HERREN deres Gud.

< Ezekieli 28 >