< Ezekieli 27 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
Beseda Gospodova je ponovno prišla k meni, rekoč:
2 “Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Tiro.
»Torej ti, človeški sin, vzdigni žalostinko za Tirom;
3 Umwambie Tiro, ulioko kwenye lango la bahari, ufanyao biashara na mataifa mengi ya pwani, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ee Tiro, wewe umesema, “Mimi ni mkamilifu katika uzuri.”
in reci Tiru: ›Oh ti, ki si postavljen na vhodu morja, ki si trgovec ljudstvom na številnih otokih: ›Tako govori Gospod Bog: ›O Tir, rekel si: ›Jaz sem popolne lepote.‹‹
4 Mipaka yako ilikuwa katika moyo wa bahari, wajenzi wako walikamilisha uzuri wako.
Tvoje meje so v sredi morij, tvoji graditelji so dovršili tvojo lepoto.
5 Walizifanya mbao zako zote kwa misunobari itokayo Seniri; walichukua mierezi kutoka Lebanoni kukutengenezea mlingoti.
Vse tvoje ladijske deske so naredili iz cipresovega lesa iz Senírja. Vzeli so libanonske cedre, da bi zate naredili jambore.
6 Walichukua mialoni toka Bashani wakakutengenezea makasia yako; kwa miti ya msanduku kutoka pwani ya Kitimu wakatengeneza sitaha yako na kuipamba kwa pembe za ndovu.
Iz bašánskih hrastov so naredili tvoja vesla; skupina Ašhúrcev je naredila tvoje klopi iz slonovine, pripeljane iz kitéjskih otokov.
7 Kitani safi kilichotariziwa kutoka Misri kilikuwa tanga lako, nacho kilikuwa bendera yako; chandarua chako kilikuwa cha rangi ya buluu na ya zambarau kutoka visiwa vya Elisha.
Tanko laneno platno z izvezenim delom iz Egipta je bilo to, kar si razširjala, da bi bilo tvoje jadro; modro in vijolično z otokov Elišája, je bilo to, kar te je pokrivalo.
8 Watu kutoka Sidoni na Arvadi walikuwa wapiga makasia yako; watu wako wenye ustadi, ee Tiro, walikuwa ndio mabaharia wako.
Prebivalci Sidóna in Arváda so bili tvoji mornarji. Tvoji modri možje, oh Tir, ki so bili v tebi, so bili tvoji krmarji.
9 Wazee wa Gebali pamoja na mafundi stadi walikuwa mafundi wako melini. Meli zote za baharini na mabaharia wao walikuja kwako ili kubadilishana bidhaa zako.
Gebálski starci in njegovi modri možje so bili v tebi tvoji popravljavci razpok. Vse morske ladje s svojimi mornarji so bile v tebi, da so prekupčevali tvoje trgovsko blago.
10 “‘Watu wa Uajemi, Ludi na Putu walikuwa askari katika jeshi lako. Walitundika ngao zao na chapeo zao kwenye kuta zako, wakileta fahari yako.
Tisti iz Perzije in iz Luda in iz Puta so bili v tvoji vojski, tvoji bojevniki. V tebi so obešali ščit in čelado; oni kažejo tvojo ljubkost.
11 Watu wa Arvadi na wa Heleki walikuwa juu ya kuta zako pande zote; watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walitundika ngao zao kuzizunguka kuta zako; wakaukamilisha uzuri wako.
Možje Arváda, s tvojo vojsko, so bili na tvojih zidovih naokoli in Gamádci so bili v tvojih stolpih. Svoje ščite so obešali naokoli po tvojih zidovih; tvojo lepoto so naredili popolno.
12 “‘Tarshishi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mkubwa wa bidhaa, walibadilisha fedha, chuma, bati na risasi kwa mali zako.
Taršíš je bil tvoj trgovec zaradi razloga množice vseh vrst bogastev; s srebrom, železom, kositrom in svincem so trgovali na tvojih sejmih.
13 “‘Uyunani, Tubali na Mesheki, walifanya biashara nawe, walibadilisha watumwa na vyombo vya shaba kwa bidhaa zako.
Javán, Tubál in Mešeh so bili tvoji trgovci. Trgovali so s človeškimi osebami in posodami iz brona na tvojem trgu.
14 “‘Watu wa Beth-Togarma walibadilisha farasi wa mizigo, farasi wa vita na nyumbu kwa mali zako.
Tisti iz hiše Togarmá so na tvojih sejmih trgovali s konji, konjeniki in mulami.
15 “‘Watu wa Dedani walifanya biashara nawe, watu wengi wa nchi za pwani walikuwa wachuuzi wako, walikulipa kwa pembe za ndovu na mpingo.
Možje iz Dedána so bili tvoji trgovci, številni otoki so bili trgovsko blago tvoje roke, za darilo so ti prinašali rogove iz slonovine in ebenovino.
16 “‘Watu wa Aramu walifanya biashara nawe kwa ajili ya wingi wa kazi za mikono yako, wakibadilishana kwa almasi, vitambaa vya rangi ya zambarau, vitambaa vilivyotariziwa, kitani safi, matumbawe na akiki nyekundu.
Sirija je bila tvoj trgovski partner zaradi razloga množičnosti stvari tvoje izdelave. Na tvojih sejmih so se zaposlovali s smaragdi, vijoličnim in izvezenim delom in tankim lanenim platnom in koraldo in ahatom.
17 “‘Yuda na Israeli walifanya biashara nawe, walibadilishana kwa ngano kutoka Minithi, mtama, asali, mafuta na zeri ya kuponyeshea.
Juda in Izraelova dežela so bili tvoji trgovci. Trgovali so na tvojem trgu s pšenico iz Miníta in Pannago in medom, oljem in balzamom.
18 “‘Dameski, kwa sababu ya wingi wa kazi za mikono yako na ukuu wa utajiri wa mali, walifanya biashara nawe wakibadilishana mvinyo kutoka Helboni na sufu kutoka Zahari.
Damask je bil tvoj trgovski partner v množici stvari tvoje izdelave zaradi množice vseh bogastev; z vinom iz Helbóna in belo volno.
19 “‘Wadani na Wayunani kutoka Uzali, walikuletea mali za biashara, nao wakabadilishana nawe chuma kilichofuliwa, mdalasini na mchaichai.
Tudi Dán in Javán, ki sta šla sem ter tja, sta se zaposlovala na tvojih sejmih. Svetlo železo, kasija in kolmež so bili na tvojem trgu.
20 “‘Dedani alifanya biashara nawe kwa matandiko ya farasi.
Dedán je bil tvoj trgovec v dragocenih oblačilih za bojne vozove.
21 “‘Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wanunuzi wako waliobadilishana bidhaa zako na wana-kondoo, kondoo dume na mbuzi.
Arabija in vsi princi Kedárja so se zaposlovali s teboj z jagnjeti, ovni in kozli; v teh so bili oni tvoji trgovci.
22 “‘Wafanyabiashara wa Sheba na wa Raama walifanya biashara nawe, wakabadilishana bidhaa zako na aina zote za vikolezi, vito vya thamani na dhahabu.
Trgovci iz Sabe in Ramája, oni so bili tvoji trgovci. Zaposlovali so se na tvojih sejmih z glavnino izmed vseh dišav in z vsemi dragocenimi kamni in z zlatom.
23 “‘Harani, Kane na Edeni na wafanyabiashara wa Sheba, Ashuru na Kilmadi walifanya biashara nawe.
Harán in Kané in Eden, trgovci iz Sabe, Asúrja in Kilmáda so bili tvoji trgovci.
24 Kwenye soko lako, walifanya biashara nawe kwa mavazi mazuri, vitambaa vya buluu, nguo za kutariziwa na mazulia ya rangi mbalimbali yenye kamba zilizosokotwa na kuwekwa mafundo imara.
To so bili tvoji trgovci v vseh vrstah stvari, v modrih oblačilih in izvezenem delu in v skrinjah bogatega videza, povezanih z vrvicami in narejenimi iz cedre, med tvojim trgovanjem.
25 “‘Merikebu za Tarshishi ndizo zinazokusafirishia bidhaa zako. Umejazwa shehena kubwa katika moyo wa bahari.
Ladje iz Taršíša so pele o tebi na tvojem trgu in ti si bil na novo napolnjen in zelo veličastno narejen v sredi morij.
26 Wapiga makasia wako wanakupeleka mpaka kwenye maji makavu. Lakini upepo wa mashariki umekuvunja vipande vipande katika moyo wa bahari.
Tvoji veslači so te privedli v velike vode. Vzhodni veter te je zlomil v sredi morij.
27 Utajiri wako, bidhaa zako na mali zako, mabaharia wako, manahodha wako, mafundi wako wa meli, wafanyabiashara wako na askari wako wote, na kila mmoja aliyeko melini atazama kwenye moyo wa bahari siku ile ya kuvunjika kwa meli yako.
Tvoja bogastva, tvoji sejmi, tvoji trgovci, tvoji mornarji in tvoji krmarji, tvoji popravljavci razpok, zaposlovalci tvojega trgovanja in vsi tvoji bojevniki, ki so v tebi in v vsej tvoji skupini, ki je v tvoji sredi, bodo padli v sredo morij na dan tvojega propada.
28 Nchi za pwani zitatetemeka wakati mabaharia wako watakapopiga kelele.
Predmestja se bodo tresla ob zvoku krika tvojih krmarjev.
29 Wote wapigao makasia wataacha meli zao, mabaharia wote na wanamaji wote watasimama pwani.
In vsi, ki prijemajo veslo, mornarji in vsi krmarji morja bodo prišli dol iz svojih ladij, stali bodo na kopnem;
30 Watapaza sauti zao na kulia sana kwa ajili yako; watajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao na kujivingirisha kwenye majivu.
in svojemu glasu bodo povzročili, da bo slišan zoper tebe in grenko bodo jokali in metali prah na svoje glave in se valjali v pepelu,
31 Watanyoa nywele zao kwa ajili yako, nao watavaa nguo za magunia. Watakulilia kwa uchungu wa moyo na kwa maombolezo makuu.
in zate se bodo naredili popolnoma plešaste in se prepasali z vrečevino in jokali bodo zaradi tebe s srčno grenkobo in grenko tarnali.
32 Watakapokuwa wanalia na kuomboleza juu yako, watafanya maombolezo kukuhusu wakisema: “Ni nani aliyepata kuangamizwa kama Tiro, katika moyo wa bahari?”
In v svojem tarnanju bodo vzdignili žalostinko za teboj in žalovali nad teboj, rekoč: ›Katero mesto je podobno Tiru, podobno uničenemu v sredi morja?
33 Wakati bidhaa zako zilipotoka baharini, ulitosheleza mataifa mengi; kwa wingi wa utajiri wako na bidhaa zako ulitajirisha wafalme wa dunia.
Ko so tvoje stvari šle naprej iz morij, si sitil mnoga ljudstva, kralje zemlje si obogatil z množico svojih bogastev in od svojega trgovanja.
34 Sasa umevunjavunjwa na bahari, katika vilindi vya maji, bidhaa zako na kundi lako lote vimezama pamoja nawe.
V času, ko boš zlomljen z morji, v globinah voda, bo tvoje trgovsko blago in vsa tvoja druščina padla v tvoji sredi.
35 Wote waishio katika nchi za pwani wanakustaajabia; wafalme wao wanatetemeka kwa hofu kuu, nazo nyuso zao zimekunjamana kwa woga.
Vsi prebivalci otokov bodo osupli nad teboj in njihovi kralji bodo boleče prestrašeni, vznemirjeni bodo na svojem obličju.
36 Wafanyabiashara miongoni mwa mataifa wanakucheka; umefikia mwisho wa kutisha nawe hutakuwepo tena.’”
Trgovci med ljudstvom bodo sikali nad teboj; strahota boš in nikoli več te ne bo.‹«

< Ezekieli 27 >