< Ezekieli 27 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
A palavra de Yahweh veio novamente a mim, dizendo:
2 “Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Tiro.
“Tu, filho do homem, faz uma lamentação sobre Tiro;
3 Umwambie Tiro, ulioko kwenye lango la bahari, ufanyao biashara na mataifa mengi ya pwani, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ee Tiro, wewe umesema, “Mimi ni mkamilifu katika uzuri.”
e diz a Tiro: 'Tu que habitas na entrada do mar, que és o mercador dos povos de muitas ilhas, diz o Senhor Yahweh: “Você, Tyre, disse, “Sou perfeito em beleza”.
4 Mipaka yako ilikuwa katika moyo wa bahari, wajenzi wako walikamilisha uzuri wako.
Suas fronteiras estão no coração dos mares. Seus construtores aperfeiçoaram sua beleza.
5 Walizifanya mbao zako zote kwa misunobari itokayo Seniri; walichukua mierezi kutoka Lebanoni kukutengenezea mlingoti.
Eles fizeram todas as suas tábuas de ciprestes de Senir. Eles pegaram um cedro do Líbano para fazer um mastro para você.
6 Walichukua mialoni toka Bashani wakakutengenezea makasia yako; kwa miti ya msanduku kutoka pwani ya Kitimu wakatengeneza sitaha yako na kuipamba kwa pembe za ndovu.
Eles fizeram seus remos dos carvalhos de Bashan. Eles fizeram suas bancadas de marfim incrustadas em madeira de cipreste proveniente das ilhas de Kittim.
7 Kitani safi kilichotariziwa kutoka Misri kilikuwa tanga lako, nacho kilikuwa bendera yako; chandarua chako kilikuwa cha rangi ya buluu na ya zambarau kutoka visiwa vya Elisha.
Sua vela era de linho fino com trabalho bordado do Egito, que poderia ser para você um banner. Azul e roxo das ilhas de Elishah era o seu toldo.
8 Watu kutoka Sidoni na Arvadi walikuwa wapiga makasia yako; watu wako wenye ustadi, ee Tiro, walikuwa ndio mabaharia wako.
Os habitantes de Sidon e Arvad eram seus remadores. Seus sábios, Tyre, estavam em você. Eles eram seus pilotos.
9 Wazee wa Gebali pamoja na mafundi stadi walikuwa mafundi wako melini. Meli zote za baharini na mabaharia wao walikuja kwako ili kubadilishana bidhaa zako.
Os homens velhos de Gebal e seus homens sábios foram seus reparadores de costuras de navios em você. Todos os navios do mar com seus marinheiros estavam em você para negociar em sua mercadoria.
10 “‘Watu wa Uajemi, Ludi na Putu walikuwa askari katika jeshi lako. Walitundika ngao zao na chapeo zao kwenye kuta zako, wakileta fahari yako.
“““Pérsia, Lud e Put estavam em seu exército, seus homens de guerra. Eles penduraram o escudo e o capacete em você. Eles mostraram sua beleza.
11 Watu wa Arvadi na wa Heleki walikuwa juu ya kuta zako pande zote; watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walitundika ngao zao kuzizunguka kuta zako; wakaukamilisha uzuri wako.
Os homens de Arvad com seu exército estavam em seus muros por toda parte, e homens corajosos estavam em suas torres. Eles penduraram seus escudos em suas paredes por toda parte. Eles aperfeiçoaram sua beleza.
12 “‘Tarshishi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mkubwa wa bidhaa, walibadilisha fedha, chuma, bati na risasi kwa mali zako.
“““Tarshish foi seu comerciante por causa da multidão de todos os tipos de riquezas. Eles trocavam por suas mercadorias com prata, ferro, estanho e chumbo.
13 “‘Uyunani, Tubali na Mesheki, walifanya biashara nawe, walibadilisha watumwa na vyombo vya shaba kwa bidhaa zako.
“““Javan, Tubal, e Meshech foram seus comerciantes. Eles negociavam as pessoas de homens e embarcações de bronze por sua mercadoria.
14 “‘Watu wa Beth-Togarma walibadilisha farasi wa mizigo, farasi wa vita na nyumbu kwa mali zako.
“““Eles da casa de Togarmah trocaram por suas mercadorias com cavalos, cavalos de guerra e mulas.
15 “‘Watu wa Dedani walifanya biashara nawe, watu wengi wa nchi za pwani walikuwa wachuuzi wako, walikulipa kwa pembe za ndovu na mpingo.
“““Os homens da Dedan negociaram com você. Muitas ilhas eram o mercado de sua mão. Eles trouxeram-lhe chifres de marfim e ébano em troca.
16 “‘Watu wa Aramu walifanya biashara nawe kwa ajili ya wingi wa kazi za mikono yako, wakibadilishana kwa almasi, vitambaa vya rangi ya zambarau, vitambaa vilivyotariziwa, kitani safi, matumbawe na akiki nyekundu.
“““A Síria foi seu comerciante por causa da multidão de suas obras. Eles trocavam por seus produtos com esmeraldas, roxo, bordados, linho fino, coral e rubis.
17 “‘Yuda na Israeli walifanya biashara nawe, walibadilishana kwa ngano kutoka Minithi, mtama, asali, mafuta na zeri ya kuponyeshea.
“““Judah e a terra de Israel eram seus comerciantes. Eles comercializavam trigo de Minnith, confeitos, mel, óleo e bálsamo para sua mercadoria.
18 “‘Dameski, kwa sababu ya wingi wa kazi za mikono yako na ukuu wa utajiri wa mali, walifanya biashara nawe wakibadilishana mvinyo kutoka Helboni na sufu kutoka Zahari.
“““Damasco foi seu comerciante pela multidão de suas obras em razão da multidão de todos os tipos de riquezas, com o vinho de Helbon, e a lã branca.
19 “‘Wadani na Wayunani kutoka Uzali, walikuletea mali za biashara, nao wakabadilishana nawe chuma kilichofuliwa, mdalasini na mchaichai.
“““Vedan e Javan negociaram com fios para suas mercadorias; ferro forjado, cássia e calamus estavam entre suas mercadorias.
20 “‘Dedani alifanya biashara nawe kwa matandiko ya farasi.
“““Dedan foi seu comerciante em preciosos cobertores de sela para montar.
21 “‘Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wanunuzi wako waliobadilishana bidhaa zako na wana-kondoo, kondoo dume na mbuzi.
“““A Arábia e todos os príncipes de Kedar eram seus comerciantes favoritos de cordeiros, carneiros e caprinos. Nesses, eles eram seus comerciantes.
22 “‘Wafanyabiashara wa Sheba na wa Raama walifanya biashara nawe, wakabadilishana bidhaa zako na aina zote za vikolezi, vito vya thamani na dhahabu.
“““Os comerciantes de Sheba e Raamah eram seus comerciantes. Eles negociaram por suas mercadorias com o melhor de todas as especiarias, todas as pedras preciosas e ouro.
23 “‘Harani, Kane na Edeni na wafanyabiashara wa Sheba, Ashuru na Kilmadi walifanya biashara nawe.
“““Haran, Canneh, Eden, os comerciantes de Sheba, Asshur e Chilmad, foram seus comerciantes.
24 Kwenye soko lako, walifanya biashara nawe kwa mavazi mazuri, vitambaa vya buluu, nguo za kutariziwa na mazulia ya rangi mbalimbali yenye kamba zilizosokotwa na kuwekwa mafundo imara.
Estes foram seus comerciantes em artigos de escolha, em envoltórios de trabalho azul e bordados, e em arcas de cedro de roupas ricas atadas com cordas, entre suas mercadorias.
25 “‘Merikebu za Tarshishi ndizo zinazokusafirishia bidhaa zako. Umejazwa shehena kubwa katika moyo wa bahari.
“““Os navios de Tarshish foram suas caravanas para suas mercadorias. Você foi reabastecido e se tornaram muito gloriosos no coração dos mares.
26 Wapiga makasia wako wanakupeleka mpaka kwenye maji makavu. Lakini upepo wa mashariki umekuvunja vipande vipande katika moyo wa bahari.
Seus remadores o trouxeram para grandes águas. O vento leste o quebrou no coração dos mares.
27 Utajiri wako, bidhaa zako na mali zako, mabaharia wako, manahodha wako, mafundi wako wa meli, wafanyabiashara wako na askari wako wote, na kila mmoja aliyeko melini atazama kwenye moyo wa bahari siku ile ya kuvunjika kwa meli yako.
Suas riquezas, seus bens, suas mercadorias, seus marinheiros, seus pilotos, seus reparadores de costuras de navios, os revendedores em sua mercadoria, e todos os seus homens de guerra que estão em você, com toda a sua empresa que está entre vocês, cairá no coração dos mares no dia de sua ruína.
28 Nchi za pwani zitatetemeka wakati mabaharia wako watakapopiga kelele.
Ao som do grito de seus pilotos, as terras de pasto vão tremer.
29 Wote wapigao makasia wataacha meli zao, mabaharia wote na wanamaji wote watasimama pwani.
Todos que lidam com os remos, os marinheiros e todos os pilotos do mar, descerão de seus navios. Eles ficarão na terra,
30 Watapaza sauti zao na kulia sana kwa ajili yako; watajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao na kujivingirisha kwenye majivu.
e fará com que sua voz seja ouvida sobre você, e vai chorar amargamente. Eles vão jogar pó na cabeça. Eles vão chafurdar nas cinzas.
31 Watanyoa nywele zao kwa ajili yako, nao watavaa nguo za magunia. Watakulilia kwa uchungu wa moyo na kwa maombolezo makuu.
Eles se tornarão carecas para você, e se vestirem com pano de saco. Eles chorarão por você em amargura de alma, com um luto amargo.
32 Watakapokuwa wanalia na kuomboleza juu yako, watafanya maombolezo kukuhusu wakisema: “Ni nani aliyepata kuangamizwa kama Tiro, katika moyo wa bahari?”
Em seus lamentos, eles aceitarão uma lamentação para você, e lamentar sobre você, dizendo, “Quem está lá como Tyre”, como ela que é levada ao silêncio no meio do mar...
33 Wakati bidhaa zako zilipotoka baharini, ulitosheleza mataifa mengi; kwa wingi wa utajiri wako na bidhaa zako ulitajirisha wafalme wa dunia.
Quando suas mercadorias vieram dos mares, você encheu muitas pessoas. Vocês enriqueceram os reis da terra com a multidão de suas riquezas e de suas mercadorias.
34 Sasa umevunjavunjwa na bahari, katika vilindi vya maji, bidhaa zako na kundi lako lote vimezama pamoja nawe.
No tempo em que você estava quebrado pelos mares, nas profundezas das águas, sua mercadoria e toda a sua empresa caíram dentro de você.
35 Wote waishio katika nchi za pwani wanakustaajabia; wafalme wao wanatetemeka kwa hofu kuu, nazo nyuso zao zimekunjamana kwa woga.
Todos os habitantes das ilhas estão surpresos com você, e seus reis estão horrivelmente assustados. Eles estão com problemas na cara.
36 Wafanyabiashara miongoni mwa mataifa wanakucheka; umefikia mwisho wa kutisha nawe hutakuwepo tena.’”
Os mercadores entre os povos assobiam para você. Você chegou a um fim terrível, e você não será mais”'”.

< Ezekieli 27 >