< Ezekieli 27 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
I stało się słowo Pańskie do mnie, mówiąc:
2 “Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Tiro.
A ty, synu człowieczy! podnieś nad Tyrem lament,
3 Umwambie Tiro, ulioko kwenye lango la bahari, ufanyao biashara na mataifa mengi ya pwani, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ee Tiro, wewe umesema, “Mimi ni mkamilifu katika uzuri.”
A rzecz do Tyru, który leży nad portami morskiemi i handluje z narodami na wielu wyspach: Tak mówi panujący Pan: O Tyrze! tyś mówił: Jam jest doskonały w piękności.
4 Mipaka yako ilikuwa katika moyo wa bahari, wajenzi wako walikamilisha uzuri wako.
W pośrodku morza były granice twoje, budownicy twoi doskonałą uczynili piękność twoję.
5 Walizifanya mbao zako zote kwa misunobari itokayo Seniri; walichukua mierezi kutoka Lebanoni kukutengenezea mlingoti.
Z jedliny z Sanir pobudowalić wszystkie piętra twoje, cedry z Libanu brali, aby czynili maszty twoje.
6 Walichukua mialoni toka Bashani wakakutengenezea makasia yako; kwa miti ya msanduku kutoka pwani ya Kitimu wakatengeneza sitaha yako na kuipamba kwa pembe za ndovu.
Z dębów Basańskich czynili wiosła twoje, ławy twoje urobili z kości słoniowych i z bukszpanu z wysep Cytymskich.
7 Kitani safi kilichotariziwa kutoka Misri kilikuwa tanga lako, nacho kilikuwa bendera yako; chandarua chako kilikuwa cha rangi ya buluu na ya zambarau kutoka visiwa vya Elisha.
Bisior haftowany egipski bywał płótnem twojem, z któregoś żagle miewał; hijacynt i szarłat z wysep Elisa był nakryciem twojem.
8 Watu kutoka Sidoni na Arvadi walikuwa wapiga makasia yako; watu wako wenye ustadi, ee Tiro, walikuwa ndio mabaharia wako.
Obywatele Sydonu, i Arwadczycy bywali żeglarzami twymi; mędrcy twoi, Tyrze! którzy bywali w tobie, ci byli sternikami twymi.
9 Wazee wa Gebali pamoja na mafundi stadi walikuwa mafundi wako melini. Meli zote za baharini na mabaharia wao walikuja kwako ili kubadilishana bidhaa zako.
Starcy z Giebal, i mędrcy jego oprawiali w tobie rozpadliny twoje; wszystkie okręty morskie i żeglarze ich bywali w tobie, handlując z tobą.
10 “‘Watu wa Uajemi, Ludi na Putu walikuwa askari katika jeshi lako. Walitundika ngao zao na chapeo zao kwenye kuta zako, wakileta fahari yako.
Persowie, i Ludczycy, i Putejczycy bywali w wojsku twojem, mężowie waleczni twoi; tarcz i przyłbicę zawieszali w tobie, ci przydawali tobie ozdoby.
11 Watu wa Arvadi na wa Heleki walikuwa juu ya kuta zako pande zote; watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walitundika ngao zao kuzizunguka kuta zako; wakaukamilisha uzuri wako.
Synowie Arwad z wojskiem twojem na murach twoich w około, także Gamadczycy na wieżach twoich bywali, tarcze twoje zawieszali na murach twoich w około; cić są, którzy doskonałą uczynili piękność twoję.
12 “‘Tarshishi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mkubwa wa bidhaa, walibadilisha fedha, chuma, bati na risasi kwa mali zako.
Zamorscy kupcy twoi dla wielkości wszelakich dostatków, srebrem, żelazem, cyną i ołowiem kupczyli na jarmarkach twoich.
13 “‘Uyunani, Tubali na Mesheki, walifanya biashara nawe, walibadilisha watumwa na vyombo vya shaba kwa bidhaa zako.
Jawan, Tubal, i Mesech, kupcy twoi, ludzi i naczynie miedziane dawali na zamianę tobie.
14 “‘Watu wa Beth-Togarma walibadilisha farasi wa mizigo, farasi wa vita na nyumbu kwa mali zako.
Z domu Togorma końmi, i jezdnymi, i mułami kupczyli na jarmarkach twoich.
15 “‘Watu wa Dedani walifanya biashara nawe, watu wengi wa nchi za pwani walikuwa wachuuzi wako, walikulipa kwa pembe za ndovu na mpingo.
Synowie Dedanowi, kupcy twoi, i wiele wysep przekupowali towary ręki twojej, rogi, kości słoniowe, i drzewo hebanowe dawali na zamianę za zapłatę twoję.
16 “‘Watu wa Aramu walifanya biashara nawe kwa ajili ya wingi wa kazi za mikono yako, wakibadilishana kwa almasi, vitambaa vya rangi ya zambarau, vitambaa vilivyotariziwa, kitani safi, matumbawe na akiki nyekundu.
Syryjczycy kupcy twoi dla mnóstwa przemyślnych robót twoich, karbunkułami, szarłatem, i haftarskiemi rzeczami, płótnem subtelnem, i koralami, i kryształami handlowali na jarmarkach twoich.
17 “‘Yuda na Israeli walifanya biashara nawe, walibadilishana kwa ngano kutoka Minithi, mtama, asali, mafuta na zeri ya kuponyeshea.
Juda i ziemia Izraelska, i ci kupcy twoi, pszenicę z Minnit i z Pannag, i miód, i oliwę. i kadzidło na zamianęć dawali.
18 “‘Dameski, kwa sababu ya wingi wa kazi za mikono yako na ukuu wa utajiri wa mali, walifanya biashara nawe wakibadilishana mvinyo kutoka Helboni na sufu kutoka Zahari.
Damaszczanie, kupcy twoi dla mnóstwa przemyślnych robót twoich, i dla mnóstwa wszelkich dostatków, winem z Helbonu i wełnę białą kupczyli.
19 “‘Wadani na Wayunani kutoka Uzali, walikuletea mali za biashara, nao wakabadilishana nawe chuma kilichofuliwa, mdalasini na mchaichai.
Także Dan i Jawan, kramarze na jarmarkach twoich, sprzedawali żelazo polerowane, kassyję, i Tatarskie ziela na zamianęć dawali.
20 “‘Dedani alifanya biashara nawe kwa matandiko ya farasi.
Dedan kupczył w tobie suknami kosztownemi na wozy.
21 “‘Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wanunuzi wako waliobadilishana bidhaa zako na wana-kondoo, kondoo dume na mbuzi.
Arabczycy, i wszyscy książęta Kedarscy, i ci kupczyli z tobą skopami i baranami, i kozłami, tem handlowali w tobie.
22 “‘Wafanyabiashara wa Sheba na wa Raama walifanya biashara nawe, wakabadilishana bidhaa zako na aina zote za vikolezi, vito vya thamani na dhahabu.
Kupcy Sabejscy i z Ramy kupczyli z tobą wszelakiemi przedniejszemi wonnemi rzeczami, i wszelakim kamieniem drogim i złotem kupczyli na jarmarkach twoich;
23 “‘Harani, Kane na Edeni na wafanyabiashara wa Sheba, Ashuru na Kilmadi walifanya biashara nawe.
Haran, i Kanne, i Eden kupcy z Saby; Assur i Kilmad kupczył w tobie.
24 Kwenye soko lako, walifanya biashara nawe kwa mavazi mazuri, vitambaa vya buluu, nguo za kutariziwa na mazulia ya rangi mbalimbali yenye kamba zilizosokotwa na kuwekwa mafundo imara.
Ci kupcy twoi, sztukami hijacyntu, i rzeczami haftowanemi, i skrzyniami dla kosztownych szat, także towarami, które powrozami obwiązują albo w skrzyniach cedrowych zawierają, kupczyli w tobie.
25 “‘Merikebu za Tarshishi ndizo zinazokusafirishia bidhaa zako. Umejazwa shehena kubwa katika moyo wa bahari.
Okręty morskie przodkowały w kupiectwie twojem; i byłoś napełnione i uwielbione bardzo w pośród morza.
26 Wapiga makasia wako wanakupeleka mpaka kwenye maji makavu. Lakini upepo wa mashariki umekuvunja vipande vipande katika moyo wa bahari.
Na wody wielkie zaprowadzili cię żeglarze twoi; wiatr wschodni rozbije cię w pośród morza.
27 Utajiri wako, bidhaa zako na mali zako, mabaharia wako, manahodha wako, mafundi wako wa meli, wafanyabiashara wako na askari wako wote, na kila mmoja aliyeko melini atazama kwenye moyo wa bahari siku ile ya kuvunjika kwa meli yako.
Bogactwa twoje, i jarmarki twoje, kupiectwo twoje, żeglarze twoi, i sternicy twoi, i ci, którzy zaprawiali rozpadliny twoje, i kupcy towarów twoich, i wszyscy mężowie waleczni twoi, którzy byli w tobie, i wszystko mnóstwo twoje, które jest w pośród ciebie, wpadną w pośród morza w dzień upadku twego.
28 Nchi za pwani zitatetemeka wakati mabaharia wako watakapopiga kelele.
Na głos krzyku sterników twoich zadrżą wały morskie;
29 Wote wapigao makasia wataacha meli zao, mabaharia wote na wanamaji wote watasimama pwani.
I wystąpią z okrętów swoich wszyscy robiący wiosłem, żeglarze, i wszyscy sternicy morscy na ziemi staną.
30 Watapaza sauti zao na kulia sana kwa ajili yako; watajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao na kujivingirisha kwenye majivu.
I będą narzekali nad tobą głosem wielkim, i będą gorzko wołali, a sypiąc proch na głowy swoje, w popiele się walać będą.
31 Watanyoa nywele zao kwa ajili yako, nao watavaa nguo za magunia. Watakulilia kwa uchungu wa moyo na kwa maombolezo makuu.
Nadto poczynią sobie dla ciebie łysiny, a opaszą się worami; i będą płakać nad tobą w gorzkości duszy swej płaczem gorzkim.
32 Watakapokuwa wanalia na kuomboleza juu yako, watafanya maombolezo kukuhusu wakisema: “Ni nani aliyepata kuangamizwa kama Tiro, katika moyo wa bahari?”
Uczynią, mówię, nad tobą lament żałośny, a będą narzekali nad tobą, mówiąc: Któreż miasto podobne jest Tyrowi, wyciętemu w pośrodku morza?
33 Wakati bidhaa zako zilipotoka baharini, ulitosheleza mataifa mengi; kwa wingi wa utajiri wako na bidhaa zako ulitajirisha wafalme wa dunia.
Gdy wychodziły towary twoje z morza, nasycałoś wiele narodów; mnóstwem bogactw twoich i handlów twoich bogaciłoś królów ziemskich.
34 Sasa umevunjavunjwa na bahari, katika vilindi vya maji, bidhaa zako na kundi lako lote vimezama pamoja nawe.
Ale gdy będziesz podruzgotane od morza w głębokościach wód, kupiectwo twoje i wszystko mnóstwo twoje w pośrodku ciebie upadnie.
35 Wote waishio katika nchi za pwani wanakustaajabia; wafalme wao wanatetemeka kwa hofu kuu, nazo nyuso zao zimekunjamana kwa woga.
Wszyscy na wyspach mieszkający zdumieją się nad tobą, a królowie ich strachem zdjęci będąc, bardzo się zatrwożą.
36 Wafanyabiashara miongoni mwa mataifa wanakucheka; umefikia mwisho wa kutisha nawe hutakuwepo tena.’”
Kupcy między narodami zaświsną nad tobą; na postrach im będziesz, a nie będzie cię na wieki.

< Ezekieli 27 >