< Ezekieli 27 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
Et la parole du Seigneur me vint, disant:
2 “Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Tiro.
Et toi, fils de l'homme, chante sur Tyr une lamentation.
3 Umwambie Tiro, ulioko kwenye lango la bahari, ufanyao biashara na mataifa mengi ya pwani, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ee Tiro, wewe umesema, “Mimi ni mkamilifu katika uzuri.”
Et dis à cette Tyr, qui réside à l'entrée de la mer, dis à ce marché des peuples venant d'une multitude d'îles: Ainsi parle le Seigneur à Tyr: Tu as dit: C'est de moi-même que je tiens ma beauté.
4 Mipaka yako ilikuwa katika moyo wa bahari, wajenzi wako walikamilisha uzuri wako.
Au cœur de la mer, tes fils t'ont revêtue de beauté pour te consacrer à Baal.
5 Walizifanya mbao zako zote kwa misunobari itokayo Seniri; walichukua mierezi kutoka Lebanoni kukutengenezea mlingoti.
Le cèdre de Sénir a servi à construire tes vaisseaux; tes planches ont été prises en des poutres de cyprès du Liban, et pour faire tes mâts on a employé des sapins.
6 Walichukua mialoni toka Bashani wakakutengenezea makasia yako; kwa miti ya msanduku kutoka pwani ya Kitimu wakatengeneza sitaha yako na kuipamba kwa pembe za ndovu.
On a fait tes rames de bois de Basan; on a fait en ivoire tes choses saintes, et tes chambres ombragées d'arbres en bois des Iles de Cétim.
7 Kitani safi kilichotariziwa kutoka Misri kilikuwa tanga lako, nacho kilikuwa bendera yako; chandarua chako kilikuwa cha rangi ya buluu na ya zambarau kutoka visiwa vya Elisha.
Le fin lin d'Égypte avec des broderies a formé ta couche; il en a été l'ornement; tu as été vêtue d'hyacinthe et de la pourpre des îles d'Élisa; c'était là ton manteau.
8 Watu kutoka Sidoni na Arvadi walikuwa wapiga makasia yako; watu wako wenye ustadi, ee Tiro, walikuwa ndio mabaharia wako.
Et tes princes, ceux qui habitent Sidon, et ceux d'Arad, te servaient de rameurs; et tes sages, ô Tyr, ceux qui résidaient en toi, étaient là tes pilotes.
9 Wazee wa Gebali pamoja na mafundi stadi walikuwa mafundi wako melini. Meli zote za baharini na mabaharia wao walikuja kwako ili kubadilishana bidhaa zako.
Les anciens de Biblos et leurs sages, ceux qui étaient en toi, ceux-là fortifiaient ton conseil. Et tous les navires de la mer, et tous leurs rameurs trafiquaient pour toi, jusqu'aux confins de l'Occident.
10 “‘Watu wa Uajemi, Ludi na Putu walikuwa askari katika jeshi lako. Walitundika ngao zao na chapeo zao kwenye kuta zako, wakileta fahari yako.
Les Perses, les Lydiens, les Libyens étaient dans ton armée; tes hommes de guerre avaient suspendu chez toi leurs boucliers et leurs casques, pour servir à ta gloire.
11 Watu wa Arvadi na wa Heleki walikuwa juu ya kuta zako pande zote; watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walitundika ngao zao kuzizunguka kuta zako; wakaukamilisha uzuri wako.
Les fils d'Arad et ton armée étaient sur tes remparts; ils faisaient bonne garde sur tes tours; ils avaient suspendu leurs carquois autour de tes édifices; c'était l'achèvement de ta beauté.
12 “‘Tarshishi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mkubwa wa bidhaa, walibadilisha fedha, chuma, bati na risasi kwa mali zako.
Les Carthaginois, par leur trafic, t'apportaient une grande part de tes richesses; ils remplissaient ton marché d'argent, d'or, de fer, d'étain et de plomb.
13 “‘Uyunani, Tubali na Mesheki, walifanya biashara nawe, walibadilisha watumwa na vyombo vya shaba kwa bidhaa zako.
La Grèce tout entière et ses colons entraient chez toi avec des âmes d'hommes, et ils apportaient sur ton marché des vases d'airain.
14 “‘Watu wa Beth-Togarma walibadilisha farasi wa mizigo, farasi wa vita na nyumbu kwa mali zako.
Ils t'amenaient des chevaux de Thogarma et des cavaliers.
15 “‘Watu wa Dedani walifanya biashara nawe, watu wengi wa nchi za pwani walikuwa wachuuzi wako, walikulipa kwa pembe za ndovu na mpingo.
Les fils des Rhodiens trafiquaient avec toi; ils multipliaient sur ton marché ce qui provenait des îles; ils t'apportaient des dents d'éléphants; et à ceux qui entraient chez toi, tu donnais des marchandises en échange:
16 “‘Watu wa Aramu walifanya biashara nawe kwa ajili ya wingi wa kazi za mikono yako, wakibadilishana kwa almasi, vitambaa vya rangi ya zambarau, vitambaa vilivyotariziwa, kitani safi, matumbawe na akiki nyekundu.
Des esclaves pris dans la multitude de ceux que tu avais à vendre, de l'huile de myrrhe et des broderies de Tharsis; Rhamoth et Chorchor approvisionnaient aussi ton marché.
17 “‘Yuda na Israeli walifanya biashara nawe, walibadilishana kwa ngano kutoka Minithi, mtama, asali, mafuta na zeri ya kuponyeshea.
Juda et les fils d'Israël trafiquaient avec toi; ils te vendaient du blé, des parfums et de la cannelle; ils t'apportaient le meilleur miel, de l'huile et de la résine pour tes marchands.
18 “‘Dameski, kwa sababu ya wingi wa kazi za mikono yako na ukuu wa utajiri wa mali, walifanya biashara nawe wakibadilishana mvinyo kutoka Helboni na sufu kutoka Zahari.
Damas trafiquait avec toi; ils t'achetaient une part de la multitude de tes marchandises, du vin de Chelbon, des laines de Milet.
19 “‘Wadani na Wayunani kutoka Uzali, walikuletea mali za biashara, nao wakabadilishana nawe chuma kilichofuliwa, mdalasini na mchaichai.
Et ils apportaient du vin sur ton marché. D'Asel venaient chez tes marchands du fer travaillé et des roues.
20 “‘Dedani alifanya biashara nawe kwa matandiko ya farasi.
Dédan trafiquait avec toi; elle t'amenait des bêtes de somme, choisies pour les chars.
21 “‘Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wanunuzi wako waliobadilishana bidhaa zako na wana-kondoo, kondoo dume na mbuzi.
L'Arabie et tous les princes de Cédar trafiquaient avec toi; ils venaient chez toi avec des chameaux, des agneaux et des béliers.
22 “‘Wafanyabiashara wa Sheba na wa Raama walifanya biashara nawe, wakabadilishana bidhaa zako na aina zote za vikolezi, vito vya thamani na dhahabu.
Les marchands de Saba et de Rhamma trafiquaient avec toi; ils apportaient à ton marché les épices les plus recherchées, des pierres précieuses et de l'or.
23 “‘Harani, Kane na Edeni na wafanyabiashara wa Sheba, Ashuru na Kilmadi walifanya biashara nawe.
Charrha et Chanaa trafiquaient avec toi; Assur et Charman trafiquaient avec toi.
24 Kwenye soko lako, walifanya biashara nawe kwa mavazi mazuri, vitambaa vya buluu, nguo za kutariziwa na mazulia ya rangi mbalimbali yenye kamba zilizosokotwa na kuwekwa mafundo imara.
Ils t'apportaient de l'hyacinthe et des ballots de marchandises précieuses, attachés avec des cordes, et des bois de cyprès
25 “‘Merikebu za Tarshishi ndizo zinazokusafirishia bidhaa zako. Umejazwa shehena kubwa katika moyo wa bahari.
Pour en faire des navires. Ceux qui trafiquaient avec toi se mêlaient à la multitude de tes marchands, et tu étais remplie et pesamment chargée au cœur de la mer.
26 Wapiga makasia wako wanakupeleka mpaka kwenye maji makavu. Lakini upepo wa mashariki umekuvunja vipande vipande katika moyo wa bahari.
Tes rameurs t'ont conduite dans les grandes eaux; et le souffle du midi t'a brisée au cœur de la mer.
27 Utajiri wako, bidhaa zako na mali zako, mabaharia wako, manahodha wako, mafundi wako wa meli, wafanyabiashara wako na askari wako wote, na kila mmoja aliyeko melini atazama kwenye moyo wa bahari siku ile ya kuvunjika kwa meli yako.
Tes richesses, tes trésors, ceux de tes marchands; tes rameurs, tes pilotes, tes conseillers; ces hommes qui trafiquent avec toi, ces guerriers qui sont chez toi, toute la multitude rassemblée en toi, tomberont au cœur de la mer le jour de ta ruine.
28 Nchi za pwani zitatetemeka wakati mabaharia wako watakapopiga kelele.
Au cri de ta voix, tes pilotes seront frappés d'épouvante.
29 Wote wapigao makasia wataacha meli zao, mabaharia wote na wanamaji wote watasimama pwani.
Tous tes rameurs, tous tes matelots descendront des navires; tous les pilotes de la mer resteront sur le rivage.
30 Watapaza sauti zao na kulia sana kwa ajili yako; watajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao na kujivingirisha kwenye majivu.
Et ils te plaindront à haute voix, et ils crieront amèrement, et ils mettront de la poussière sur leurs têtes, et ils se couvriront de cendre.
31 Watanyoa nywele zao kwa ajili yako, nao watavaa nguo za magunia. Watakulilia kwa uchungu wa moyo na kwa maombolezo makuu.
Et leurs fils feront sur toi une lamentation, une complainte sur Tyr, disant:
32 Watakapokuwa wanalia na kuomboleza juu yako, watafanya maombolezo kukuhusu wakisema: “Ni nani aliyepata kuangamizwa kama Tiro, katika moyo wa bahari?”
Et leurs fils feront sur toi une lamentation, une complainte sur Tyr, disant:
33 Wakati bidhaa zako zilipotoka baharini, ulitosheleza mataifa mengi; kwa wingi wa utajiri wako na bidhaa zako ulitajirisha wafalme wa dunia.
Quel profit as-tu retiré de la mer? Tu avais rempli de ton abondance toutes les nations; tu avais enrichi par ton trafic tous les rois de la terre.
34 Sasa umevunjavunjwa na bahari, katika vilindi vya maji, bidhaa zako na kundi lako lote vimezama pamoja nawe.
Maintenant tu es brisée dans la mer; tes trafiquants sont au fond de l'abîme, avec toute la multitude assemblée en toi.
35 Wote waishio katika nchi za pwani wanakustaajabia; wafalme wao wanatetemeka kwa hofu kuu, nazo nyuso zao zimekunjamana kwa woga.
Tous tes rameurs sont tombés; tous les habitants des îles se sont affligés sur toi; leurs rois ont été saisis de stupeur, et leur visage s'est couvert de larme.
36 Wafanyabiashara miongoni mwa mataifa wanakucheka; umefikia mwisho wa kutisha nawe hutakuwepo tena.’”
Les marchands des nations t'ont sifflée; tu es perdue, et tu ne seras plus dans les siècles.