< Ezekieli 27 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
And the word of the Lord came to me, saying:
2 “Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Tiro.
“You, therefore, son of man, take up a lamentation over Tyre.
3 Umwambie Tiro, ulioko kwenye lango la bahari, ufanyao biashara na mataifa mengi ya pwani, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ee Tiro, wewe umesema, “Mimi ni mkamilifu katika uzuri.”
And you shall say to Tyre, which lives at the entrance to the sea, which is the marketplace of the peoples for the many islands: Thus says the Lord God: O Tyre, you have said, ‘I am of perfect beauty,
4 Mipaka yako ilikuwa katika moyo wa bahari, wajenzi wako walikamilisha uzuri wako.
for I have been positioned at the heart of the sea!’ Your neighbors, who built you, have filled up your beauty.
5 Walizifanya mbao zako zote kwa misunobari itokayo Seniri; walichukua mierezi kutoka Lebanoni kukutengenezea mlingoti.
They constructed you with spruce from Senir, with all the planks of the sea. They have taken cedars from Lebanon, so that they might make a mast for you.
6 Walichukua mialoni toka Bashani wakakutengenezea makasia yako; kwa miti ya msanduku kutoka pwani ya Kitimu wakatengeneza sitaha yako na kuipamba kwa pembe za ndovu.
They have formed your oars from the oaks of Bashan. And they have made your crossbeams from Indian ivory, and the pilothouse is from the islands of Italy.
7 Kitani safi kilichotariziwa kutoka Misri kilikuwa tanga lako, nacho kilikuwa bendera yako; chandarua chako kilikuwa cha rangi ya buluu na ya zambarau kutoka visiwa vya Elisha.
Colorful fine linen from Egypt was woven for you as a sail to be placed upon the mast; hyacinth and purple from the islands of Elishah were made into your covering.
8 Watu kutoka Sidoni na Arvadi walikuwa wapiga makasia yako; watu wako wenye ustadi, ee Tiro, walikuwa ndio mabaharia wako.
The inhabitants of Sidon and of Arwad were your rowers. Your wise ones, O Tyre, were your navigators.
9 Wazee wa Gebali pamoja na mafundi stadi walikuwa mafundi wako melini. Meli zote za baharini na mabaharia wao walikuja kwako ili kubadilishana bidhaa zako.
The elders of Gebal and its experts were considered as sailors making use of your diverse equipment. All the ships of the sea and their sailors were your merchants among the people.
10 “‘Watu wa Uajemi, Ludi na Putu walikuwa askari katika jeshi lako. Walitundika ngao zao na chapeo zao kwenye kuta zako, wakileta fahari yako.
The Persians, and the Lydians, and the Libyans were your men of war in your army. They suspended shield and helmet within you for your adornment.
11 Watu wa Arvadi na wa Heleki walikuwa juu ya kuta zako pande zote; watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walitundika ngao zao kuzizunguka kuta zako; wakaukamilisha uzuri wako.
The sons of Arwad were with your army upon your walls all around. And even the Gammadim, who were in your towers, suspended their quivers on your walls on all sides; they completed your beauty.
12 “‘Tarshishi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mkubwa wa bidhaa, walibadilisha fedha, chuma, bati na risasi kwa mali zako.
The Carthaginians, your merchants, supplied your festivals with a multitude of diverse riches, with silver, iron, tin, and lead.
13 “‘Uyunani, Tubali na Mesheki, walifanya biashara nawe, walibadilisha watumwa na vyombo vya shaba kwa bidhaa zako.
Greece, Tubal, and Meshech, these were your peddlers; they traveled to your people with slaves and with brass vessels.
14 “‘Watu wa Beth-Togarma walibadilisha farasi wa mizigo, farasi wa vita na nyumbu kwa mali zako.
From the house of Togarmah, they brought horses, and horsemen, and mules to your market.
15 “‘Watu wa Dedani walifanya biashara nawe, watu wengi wa nchi za pwani walikuwa wachuuzi wako, walikulipa kwa pembe za ndovu na mpingo.
The sons of Dedan were your merchants. The many islands were the marketplace of your hand. They traded teeth of ivory and of ebony for your price.
16 “‘Watu wa Aramu walifanya biashara nawe kwa ajili ya wingi wa kazi za mikono yako, wakibadilishana kwa almasi, vitambaa vya rangi ya zambarau, vitambaa vilivyotariziwa, kitani safi, matumbawe na akiki nyekundu.
The Syrian was your merchant. Because of the multitude of your works, they offered jewels, and purple, and patterned cloth, and fine linen, and silk, and other valuables in your market.
17 “‘Yuda na Israeli walifanya biashara nawe, walibadilishana kwa ngano kutoka Minithi, mtama, asali, mafuta na zeri ya kuponyeshea.
Judah and the land of Israel, these were your peddlers of the best grain; they offered balsam, and honey, and oil, and resins at your festivals.
18 “‘Dameski, kwa sababu ya wingi wa kazi za mikono yako na ukuu wa utajiri wa mali, walifanya biashara nawe wakibadilishana mvinyo kutoka Helboni na sufu kutoka Zahari.
The Damascene was your trader in the multitude of your works, in greatly diverse wealth, in rich wine, in wool with the finest coloring.
19 “‘Wadani na Wayunani kutoka Uzali, walikuletea mali za biashara, nao wakabadilishana nawe chuma kilichofuliwa, mdalasini na mchaichai.
Dan, and Greece, and Mosel have offered works made of iron at your festivals. Storax ointment and sweet flag were in your marketplace.
20 “‘Dedani alifanya biashara nawe kwa matandiko ya farasi.
The men of Dedan were your peddlers of tapestries used as seats.
21 “‘Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wanunuzi wako waliobadilishana bidhaa zako na wana-kondoo, kondoo dume na mbuzi.
Arabia and all the leaders of Kedar, these were the merchants at your hand. Your merchants came to you with lambs, and rams, and young goats.
22 “‘Wafanyabiashara wa Sheba na wa Raama walifanya biashara nawe, wakabadilishana bidhaa zako na aina zote za vikolezi, vito vya thamani na dhahabu.
The vendors of Sheba and Raamah, these were your merchants, with all the finest aromatics, and precious stones, and gold, which they offered in your marketplace.
23 “‘Harani, Kane na Edeni na wafanyabiashara wa Sheba, Ashuru na Kilmadi walifanya biashara nawe.
Haran, and Canneh, and Eden were your merchants. Sheba, Assur, and Chilmad were your sellers.
24 Kwenye soko lako, walifanya biashara nawe kwa mavazi mazuri, vitambaa vya buluu, nguo za kutariziwa na mazulia ya rangi mbalimbali yenye kamba zilizosokotwa na kuwekwa mafundo imara.
These were your merchants in many places, with windings of hyacinth and of colorful weavings, and with precious treasures, which were wrapped and bound with cords. Also, they had works of cedar among your merchandise.
25 “‘Merikebu za Tarshishi ndizo zinazokusafirishia bidhaa zako. Umejazwa shehena kubwa katika moyo wa bahari.
The ships of the sea were important to your business dealings. For you were replenished and exceedingly glorified in the heart of the sea.
26 Wapiga makasia wako wanakupeleka mpaka kwenye maji makavu. Lakini upepo wa mashariki umekuvunja vipande vipande katika moyo wa bahari.
Your rowers have brought you into many waters. The south wind has worn you down in the heart of the sea.
27 Utajiri wako, bidhaa zako na mali zako, mabaharia wako, manahodha wako, mafundi wako wa meli, wafanyabiashara wako na askari wako wote, na kila mmoja aliyeko melini atazama kwenye moyo wa bahari siku ile ya kuvunjika kwa meli yako.
Your riches, and your treasures, and your versatile equipment, your sailors and your navigators, who handle your goods and who were first among your people, likewise your men of war, who were among you, and your entire multitude that is in your midst: they will fall in the heart of the sea on the day of your ruin.
28 Nchi za pwani zitatetemeka wakati mabaharia wako watakapopiga kelele.
Your fleets will be disturbed by the sound of an outcry from your navigators.
29 Wote wapigao makasia wataacha meli zao, mabaharia wote na wanamaji wote watasimama pwani.
And all who were handling the oar will descend from their ships; the sailors and all the navigators of the sea will stand upon the land.
30 Watapaza sauti zao na kulia sana kwa ajili yako; watajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao na kujivingirisha kwenye majivu.
And they will howl over you with a great voice, and they will cry out with bitterness. And they will cast dust upon their heads, and they will be sprinkled with ashes.
31 Watanyoa nywele zao kwa ajili yako, nao watavaa nguo za magunia. Watakulilia kwa uchungu wa moyo na kwa maombolezo makuu.
And they will shave their heads because of you, and they will be wrapped in haircloth. And they will weep for you with bitterness of soul, with a very bitter weeping.
32 Watakapokuwa wanalia na kuomboleza juu yako, watafanya maombolezo kukuhusu wakisema: “Ni nani aliyepata kuangamizwa kama Tiro, katika moyo wa bahari?”
And they will take up a mournful verse over you, and they will lament you: ‘What city is like Tyre, which has become mute in the midst of the sea?’
33 Wakati bidhaa zako zilipotoka baharini, ulitosheleza mataifa mengi; kwa wingi wa utajiri wako na bidhaa zako ulitajirisha wafalme wa dunia.
For by the going forth of your merchandise by sea, you supplied many peoples; by the multitude of your riches and of your people, you enriched the kings of the earth.
34 Sasa umevunjavunjwa na bahari, katika vilindi vya maji, bidhaa zako na kundi lako lote vimezama pamoja nawe.
Now you have been worn away by the sea, your opulence is in the depths of the waters, and your entire multitude that was in your midst has fallen.
35 Wote waishio katika nchi za pwani wanakustaajabia; wafalme wao wanatetemeka kwa hofu kuu, nazo nyuso zao zimekunjamana kwa woga.
All the inhabitants of the islands have been stupefied over you; and all their kings, having been struck by the tempest, have changed their expression.
36 Wafanyabiashara miongoni mwa mataifa wanakucheka; umefikia mwisho wa kutisha nawe hutakuwepo tena.’”
The merchants of the peoples have hissed over you. You have been reduced to nothing, and you shall not be again, even forever.”