< Ezekieli 26 >

1 Mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
No décimo primeiro ano, no primeiro do mês, a palavra de Javé veio até mim, dizendo:
2 “Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema kuhusu Yerusalemu, ‘Aha! Lango la kwenda kwa mataifa limevunjika, nayo milango yake iko wazi mbele yangu, sasa kwa kuwa amekuwa magofu nitastawi.’
“Filho do homem, porque Tiro disse contra Jerusalém: 'Aha! Ela está quebrada! Ela, que era a porta de entrada dos povos, voltou para mim. Eu serei reabastecido, agora que ela está devastada;
3 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na wewe, ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi dhidi yako, kama bahari inayovurumisha mawimbi yake.
portanto, o Senhor Javé diz: 'Eis que eu estou contra ti, Tiro, e farei com que muitas nações se aproximem de ti, pois o mar faz subir suas ondas.
4 Watavunja kuta za Tiro na kuibomoa minara yake, nitakwangua udongo wake na kuufanya mwamba mtupu.
They destruirá as paredes de Tyre, e derrubará suas torres. Também lhe arrancarei o pó e farei dela uma rocha nua.
5 Itakuwa huko katikati ya bahari patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki, kwa maana nimenena, asema Bwana Mwenyezi. Atakuwa nyara kwa mataifa,
Ela será um lugar para a propagação de redes no meio do mar; pois eu o falei”, diz o Senhor Javé. Ela se tornará um saque para as nações”.
6 nayo makao yake huko bara yataangamizwa kwa upanga. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.
Suas filhas que estão no campo serão mortas com a espada. Então elas saberão que eu sou Yahweh'.
7 “Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kutoka kaskazini nitamleta dhidi ya Tiro Mfalme Nebukadneza wa Babeli, mfalme wa wafalme, akiwa na farasi na magari ya vita, wapanda farasi na jeshi kubwa.
“Pois o Senhor Javé diz: “Eis que trarei sobre Tiro Nabucodonosor rei da Babilônia, rei dos reis, do norte, com cavalos, com carros, com cavaleiros, e um exército com muita gente.
8 Atayaharibu makao yako huko bara kwa upanga, ataweka jeshi kukuzingira, atakuzingira mpaka kwenye kuta za ngome zako na kuinua ngao zake dhidi yako.
Ele matará suas filhas no campo com a espada. Ele fará fortes contra vocês, levantará um montículo contra vocês e levantará o balde contra vocês.
9 Ataelekeza mapigo ya vyombo vyake vya kubomolea dhidi ya kuta zako na kubomoa minara yako kwa silaha zake.
Ele encostará seus motores de aríete contra suas paredes e com seus eixos derrubará suas torres.
10 Farasi zake zitakuwa nyingi sana kiasi kwamba utafunikwa na mavumbi watakayotimua. Kuta zako zitatikisika kwa mshindo wa farasi wa vita, magari makubwa na magari ya vita wakati aingiapo malango yako kama watu waingiao mji ambao kuta zake zimebomolewa kote.
Em razão da abundância de seus cavalos, a poeira deles o cobrirá. Seus muros tremerão com o barulho dos cavaleiros, das carroças e das carruagens, quando ele entrar em seus portões, quando os homens entrarem em uma cidade que está aberta.
11 “Kwato za farasi zake zitakanyaga barabara zako zote, atawaua watu wako kwa upanga na nguzo zako zilizo imara zitaanguka chini.
Ele pisará todas as suas ruas com os cascos de seus cavalos. Ele matará seu povo com a espada. Os pilares de sua força descerão até o chão.
12 Watateka utajiri wako na kuchukua nyara bidhaa zako, watazivunja kuta zako na kuzibomoa nyumba zako nzuri, watatupa baharini mawe yako, mbao zako na kifusi chako.
Eles farão um saque de suas riquezas e farão de sua mercadoria uma presa. Eles derrubarão suas paredes e destruirão suas casas agradáveis. Colocarão suas pedras, sua madeira e seu pó no meio das águas.
13 Nitakomesha kelele za nyimbo zako, na uimbaji wako wa kinubi kamwe hautasikika tena.
Farei cessar o barulho de suas canções. O som de suas harpas não será mais ouvido.
14 Nitakufanya mwamba mtupu, nawe utakuwa mahali pa kutandazia nyavu za kuvulia samaki. Kamwe hutajengwa tena, kwa maana Mimi Bwana nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
Vou fazer de vocês uma pedra nua. Vocês serão um lugar para a propagação das redes. Vocês não serão mais construídos; pois eu, Yahweh, o falei”, diz o Senhor Yahweh.
15 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa Tiro: ‘Je, nchi za pwani hazitatetemeka kwa kishindo cha anguko lako, wakati majeruhi wanapolia kwa maumivu makali na wakati mauaji yanaendelea ndani yako?
“O Senhor Javé diz a Tyre: 'Será que as ilhas não tremerão ao som de sua queda, quando o gemido dos feridos, quando o abate for feito dentro de você?
16 Ndipo wakuu wote wa mataifa ya pwani watashuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuweka kando majoho yao na kuvua nguo zao zilizotariziwa. Wakiwa wamevikwa hofu kuu, wataketi chini ardhini, wakiwa wanatetemeka kila dakika na wakikustajabia.
Então todos os príncipes do mar descerão de seus tronos, colocarão suas vestes de lado e despirão suas vestes bordadas. Eles se vestirão de tremores. Sentar-se-ão no chão, e tremerão a cada momento, e ficarão surpresos com você.
17 Ndipo wao watakuombolezea na kukuambia: “‘Tazama jinsi ulivyoharibiwa, ee mji uliokuwa na sifa, wewe uliyekaliwa na mabaharia! Ulikuwa na nguvu kwenye bahari, wewe na watu wako; wote walioishi huko, uliwatia hofu kuu.
Eles vão se lamentar de você, e lhe dirão, “Como você é destruído”, que eram habitados por marinheiros, a famosa cidade, que era forte no mar, ela e seus habitantes, que causaram seu terror em todos os que lá viviam”!
18 Sasa nchi za pwani zinatetemeka katika siku ya anguko lako; visiwa vilivyomo baharini vinaogopa kwa kuporomoka kwako.’
Agora as ilhas vão tremer no dia de sua queda. Sim, as ilhas que estão no mar ficarão consternadas com a sua partida”.
19 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitakapokufanya uwe mji wa ukiwa, kama miji isiyokaliwa tena na watu, nitakapoleta vilindi vya bahari juu yako na maji yake makuu yatakapokufunika,
“Pois o Senhor Javé diz: 'Quando eu fizer de ti uma cidade desolada, como as cidades que não são habitadas, quando eu fizer subir o abismo sobre ti, e as grandes águas te cobrirem,
20 ndipo nitakapokushusha chini pamoja na wale washukao shimoni, kwa watu wa kale, nami nitakufanya uishi katika pande za chini za nchi kama katika magofu ya kale, pamoja na wale washukao shimoni, nawe hutarudi au kurejea kwenye makao yako katika nchi ya walio hai.
então eu te farei descer com aqueles que descem ao poço, ao povo dos velhos tempos, e te farei habitar nas partes mais baixas da terra, nos lugares desolados de outrora, com aqueles que descem ao poço, para que não sejas habitado; e colocarei a glória na terra dos vivos'.
21 Nitakufikisha mwisho wa kutisha wala hutakuwepo tena. Watu watakutafuta, lakini kamwe hutaonekana tena, asema Bwana Mwenyezi.”
Farei de vocês um terror, e não terão mais nenhum ser. Embora vocês sejam procurados, nunca mais serão encontrados”, diz o Senhor Yahweh”.

< Ezekieli 26 >