< Ezekieli 26 >

1 Mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
La onzième année, le premier du mois, la parole de Yahweh me fut adressée en ces termes:
2 “Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema kuhusu Yerusalemu, ‘Aha! Lango la kwenda kwa mataifa limevunjika, nayo milango yake iko wazi mbele yangu, sasa kwa kuwa amekuwa magofu nitastawi.’
" Fils de l'homme, parce que Tyr a dit de Jérusalem: Ha! Ha! elle est brisée, la porte des peuples! on se tourne vers moi; je vais me remplir! elle est devenue un désert! —
3 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na wewe, ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi dhidi yako, kama bahari inayovurumisha mawimbi yake.
à cause de cela ainsi parle le Seigneur Yahweh: Voici que je viens contre toi, Tyr! Je vais faire monter contre toi des nations nombreuses, comme la mer fait monter ses flots.
4 Watavunja kuta za Tiro na kuibomoa minara yake, nitakwangua udongo wake na kuufanya mwamba mtupu.
Elles détruiront les murs de Tyr, et abattront ses tours; je balaierai loin d'elle sa poussière, et je ferai d'elle un rocher nu.
5 Itakuwa huko katikati ya bahari patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki, kwa maana nimenena, asema Bwana Mwenyezi. Atakuwa nyara kwa mataifa,
Elle sera, au milieu de la mer, un lieu où l'on étend les filets; car moi j'ai parlé, — oracle du Seigneur Yahweh; elle sera la proie des nations.
6 nayo makao yake huko bara yataangamizwa kwa upanga. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.
Ses filles qui sont sur la terre ferme seront tuées par l'épée, et on saura que je suis Yahweh.
7 “Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kutoka kaskazini nitamleta dhidi ya Tiro Mfalme Nebukadneza wa Babeli, mfalme wa wafalme, akiwa na farasi na magari ya vita, wapanda farasi na jeshi kubwa.
Car ainsi parle le Seigneur Yahweh: Voici que je vais amener du septentrion contre Tyr, Nabuchodonosor, roi de Babylone, le roi des rois, avec des chevaux, des chars, des cavaliers, et une multitude de troupes et un peuple nombreux.
8 Atayaharibu makao yako huko bara kwa upanga, ataweka jeshi kukuzingira, atakuzingira mpaka kwenye kuta za ngome zako na kuinua ngao zake dhidi yako.
Il tuera par l'épée tes filles sur la terre ferme, il construira contre toi des murs, il élèvera contre toi des terrasses, et dressera contre toi la tortue.
9 Ataelekeza mapigo ya vyombo vyake vya kubomolea dhidi ya kuta zako na kubomoa minara yako kwa silaha zake.
Il dirigera contre tes murs le choc de ses béliers, et démolira tes tours avec ses crochets.
10 Farasi zake zitakuwa nyingi sana kiasi kwamba utafunikwa na mavumbi watakayotimua. Kuta zako zitatikisika kwa mshindo wa farasi wa vita, magari makubwa na magari ya vita wakati aingiapo malango yako kama watu waingiao mji ambao kuta zake zimebomolewa kote.
Telle sera la multitude de ses chevaux que leur poussière te couvrira; au bruit des cavaliers, des roues et des chars, tes murs trembleront, quand il entrera dans tes portes, comme on entre dans une ville forcée.
11 “Kwato za farasi zake zitakanyaga barabara zako zote, atawaua watu wako kwa upanga na nguzo zako zilizo imara zitaanguka chini.
Du sabot de ses chevaux, il foulera toutes les rues; il tuera ton peuple par l'épée, et tes puissantes colonnes seront jetées par terre.
12 Watateka utajiri wako na kuchukua nyara bidhaa zako, watazivunja kuta zako na kuzibomoa nyumba zako nzuri, watatupa baharini mawe yako, mbao zako na kifusi chako.
Ils enlèveront tes richesses, pilleront tes marchandises, abattront tes murailles, renverseront tes beaux palais, et jetteront au milieu des eaux tes pierres, ton bois et ta poussière.
13 Nitakomesha kelele za nyimbo zako, na uimbaji wako wa kinubi kamwe hautasikika tena.
Je ferai cesser le bruit de tes chansons, et le son de tes cithares ne se fera plus entendre.
14 Nitakufanya mwamba mtupu, nawe utakuwa mahali pa kutandazia nyavu za kuvulia samaki. Kamwe hutajengwa tena, kwa maana Mimi Bwana nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
Je ferai de toi un rocher nu, tu seras un lieu où l'on étend les filets; tu ne seras plus rebâtie; car moi, Yahweh, j'ai parlé, — oracle du Seigneur Yahweh.
15 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa Tiro: ‘Je, nchi za pwani hazitatetemeka kwa kishindo cha anguko lako, wakati majeruhi wanapolia kwa maumivu makali na wakati mauaji yanaendelea ndani yako?
Ainsi parle à Tyr le Seigneur Yahweh: Au bruit de ta chute, quand tes blessés pousseront des gémissements, quand le carnage sévira au milieu de toi, les îles ne trembleront-elles pas?
16 Ndipo wakuu wote wa mataifa ya pwani watashuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuweka kando majoho yao na kuvua nguo zao zilizotariziwa. Wakiwa wamevikwa hofu kuu, wataketi chini ardhini, wakiwa wanatetemeka kila dakika na wakikustajabia.
Et ils descendront de leurs trônes, tous les princes de la mer; ils quitteront leurs manteaux, et déposeront leurs vêtements brodés; ils se vêtiront d'épouvante, ils s'assoieront sur la terre; ils trembleront à chaque moment, et seront dans la stupeur à cause de toi.
17 Ndipo wao watakuombolezea na kukuambia: “‘Tazama jinsi ulivyoharibiwa, ee mji uliokuwa na sifa, wewe uliyekaliwa na mabaharia! Ulikuwa na nguvu kwenye bahari, wewe na watu wako; wote walioishi huko, uliwatia hofu kuu.
Et ils prononceront sur toi une complainte, et ils te diront: " Comment as-tu péri, toi qui te dressais au sein des mers, ô toi ville célèbre, qui étais puissante sur la mer, toi et tes habitants, alors qu'ils inspiraient la terreur à tous les habitants de la mer. "
18 Sasa nchi za pwani zinatetemeka katika siku ya anguko lako; visiwa vilivyomo baharini vinaogopa kwa kuporomoka kwako.’
Maintenant les îles trembleront au jour de ta chute, et les îles qui sont dans la mer seront épouvantées de ta fin.
19 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitakapokufanya uwe mji wa ukiwa, kama miji isiyokaliwa tena na watu, nitakapoleta vilindi vya bahari juu yako na maji yake makuu yatakapokufunika,
Car ainsi parle le Seigneur Yahweh: Quand j'aurai fait de toi une ville déserte, comme les villes qui n'ont point d'habitants; quand j'aurai fait monter sur toi l'abîme, et que les grandes eaux t'auront couverte,
20 ndipo nitakapokushusha chini pamoja na wale washukao shimoni, kwa watu wa kale, nami nitakufanya uishi katika pande za chini za nchi kama katika magofu ya kale, pamoja na wale washukao shimoni, nawe hutarudi au kurejea kwenye makao yako katika nchi ya walio hai.
je te ferai descendre avec ceux qui sont descendus dans la fosse, vers les peuples d'autrefois; je te ferai habiter dans les profondeurs de la terre, dans les solitudes éternelles, avec ceux qui sont descendus dans la fosse, pour que tu ne sois plus habitée; et je mettrai un ornement sur la terre des vivants.
21 Nitakufikisha mwisho wa kutisha wala hutakuwepo tena. Watu watakutafuta, lakini kamwe hutaonekana tena, asema Bwana Mwenyezi.”
Je ferai de toi un objet d'épouvante, et tu ne seras plus; on te cherchera, et on ne te trouvera plus jamais, — oracle du Seigneur Yahweh. "

< Ezekieli 26 >