< Ezekieli 26 >

1 Mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
And it came to pass in the eleventh year, on the first day of the month, that the word bf Jehovah came to me, saying:
2 “Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema kuhusu Yerusalemu, ‘Aha! Lango la kwenda kwa mataifa limevunjika, nayo milango yake iko wazi mbele yangu, sasa kwa kuwa amekuwa magofu nitastawi.’
Son of man, because Tyre hath said against Jerusalem, “Aha! she is broken that was the gate of the nations; now is all transferred to me; I shall be full, now that she is desolate!”
3 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na wewe, ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi dhidi yako, kama bahari inayovurumisha mawimbi yake.
therefore thus saith the Lord Jehovah: Behold, I am against thee, O Tyre, and I will cause many nations to come up against thee, as the sea causeth his waves to come up.
4 Watavunja kuta za Tiro na kuibomoa minara yake, nitakwangua udongo wake na kuufanya mwamba mtupu.
And they shall destroy the walls of Tyre, and break down her towers; and I will scrape off her earth from her, and make her like a naked rock.
5 Itakuwa huko katikati ya bahari patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki, kwa maana nimenena, asema Bwana Mwenyezi. Atakuwa nyara kwa mataifa,
She shall be a place for the spreading of nets in the midst of the sea; for I have spoken it, saith the Lord Jehovah. And she shall be to the nations for a spoil;
6 nayo makao yake huko bara yataangamizwa kwa upanga. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.
and her daughters that are upon the land shall be slain by the sword; and they shall know that I am Jehovah.
7 “Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kutoka kaskazini nitamleta dhidi ya Tiro Mfalme Nebukadneza wa Babeli, mfalme wa wafalme, akiwa na farasi na magari ya vita, wapanda farasi na jeshi kubwa.
For thus saith the Lord Jehovah: Behold, I will bring against Tyre Nebuchadnezzar, the king of Babylon, a king of kings from the North, with horses, and with chariots, and with horsemen, and a vast multitude of people.
8 Atayaharibu makao yako huko bara kwa upanga, ataweka jeshi kukuzingira, atakuzingira mpaka kwenye kuta za ngome zako na kuinua ngao zake dhidi yako.
Thy daughters upon the land shall he slay with the sword; and he shall set a tower against thee, and cast up a mound against thee, and lift up the buckler against thee;
9 Ataelekeza mapigo ya vyombo vyake vya kubomolea dhidi ya kuta zako na kubomoa minara yako kwa silaha zake.
and his battering-rams shall be set against thy walls, and thy towers shall he break down with axes.
10 Farasi zake zitakuwa nyingi sana kiasi kwamba utafunikwa na mavumbi watakayotimua. Kuta zako zitatikisika kwa mshindo wa farasi wa vita, magari makubwa na magari ya vita wakati aingiapo malango yako kama watu waingiao mji ambao kuta zake zimebomolewa kote.
By reason of the great number of his horses, their dust shall cover thee; thy walls shall shake at the noise of the horsemen, and of the wheels, and of the chariots, when he entereth into thy gates, as men enter into a city that is broken through.
11 “Kwato za farasi zake zitakanyaga barabara zako zote, atawaua watu wako kwa upanga na nguzo zako zilizo imara zitaanguka chini.
With the hoofs of his horses shall he tread down all thy streets; thy people he shall slay with the sword; and the idols of thy strength shall fall to the ground.
12 Watateka utajiri wako na kuchukua nyara bidhaa zako, watazivunja kuta zako na kuzibomoa nyumba zako nzuri, watatupa baharini mawe yako, mbao zako na kifusi chako.
And they shall make a spoil of thy riches, and make a prey of thy merchandise; and they shall break down thy walls, and destroy thy beautiful houses; and thy stones and thy timber and thine earth shall they lay in the midst of the waters.
13 Nitakomesha kelele za nyimbo zako, na uimbaji wako wa kinubi kamwe hautasikika tena.
And I will cause the noise of thy songs to cease, and the sound of thy harps shall be no more heard.
14 Nitakufanya mwamba mtupu, nawe utakuwa mahali pa kutandazia nyavu za kuvulia samaki. Kamwe hutajengwa tena, kwa maana Mimi Bwana nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
And I will make thee like a naked rock; thou shalt be a place to spread nets upon; thou shalt be built no more; for I, Jehovah, have spoken it, saith the Lord Jehovah.
15 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa Tiro: ‘Je, nchi za pwani hazitatetemeka kwa kishindo cha anguko lako, wakati majeruhi wanapolia kwa maumivu makali na wakati mauaji yanaendelea ndani yako?
Thus saith the Lord Jehovah to Tyre: Behold, the isles shall shake at the sound of thy fall, at the groaning of the wounded, and at the slaughter which is made in the midst of thee.
16 Ndipo wakuu wote wa mataifa ya pwani watashuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuweka kando majoho yao na kuvua nguo zao zilizotariziwa. Wakiwa wamevikwa hofu kuu, wataketi chini ardhini, wakiwa wanatetemeka kila dakika na wakikustajabia.
And all the princes of the sea shall come down from their thrones, and lay aside their mantles, and put off their embroidered garments. They shall clothe themselves with trembling, and sit on the ground, and tremble every moment, and be astonished at thee.
17 Ndipo wao watakuombolezea na kukuambia: “‘Tazama jinsi ulivyoharibiwa, ee mji uliokuwa na sifa, wewe uliyekaliwa na mabaharia! Ulikuwa na nguvu kwenye bahari, wewe na watu wako; wote walioishi huko, uliwatia hofu kuu.
And they shall utter a lamentation over thee, and say to thee, “How art thou destroyed, thou that wast peopled from the seas, the renowned city, that wast mighty upon the sea, thou and thine inhabitants, causing terror to all that dwelt near thee!”
18 Sasa nchi za pwani zinatetemeka katika siku ya anguko lako; visiwa vilivyomo baharini vinaogopa kwa kuporomoka kwako.’
Now shall the isles tremble in the day of thy fall; yea, the isles that are in the sea shall quake at thy departure.
19 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitakapokufanya uwe mji wa ukiwa, kama miji isiyokaliwa tena na watu, nitakapoleta vilindi vya bahari juu yako na maji yake makuu yatakapokufunika,
For thus saith the Lord Jehovah: When I shall make thee a desolate city, like the cities that are not inhabited, when I shall bring up the deep upon thee, and great waters shall cover thee,
20 ndipo nitakapokushusha chini pamoja na wale washukao shimoni, kwa watu wa kale, nami nitakufanya uishi katika pande za chini za nchi kama katika magofu ya kale, pamoja na wale washukao shimoni, nawe hutarudi au kurejea kwenye makao yako katika nchi ya walio hai.
I will bring thee down to them that have gone down to the pit, to the people of old time, and I will cause thee to dwell in the lower parts of the earth, amid the ruins of ancient times, with them that have gone down to the pit, that thou be no more inhabited; but I will set glory in the land of the living.
21 Nitakufikisha mwisho wa kutisha wala hutakuwepo tena. Watu watakutafuta, lakini kamwe hutaonekana tena, asema Bwana Mwenyezi.”
I will make thee a desolation, and thou shalt be no more; though thou be sought for, thou shalt be found no more forever, saith the Lord Jehovah.

< Ezekieli 26 >