< Ezekieli 24 >

1 Katika mwaka wa tisa, mwezi wa kumi, siku ya kumi, neno la Bwana likanijia kusema:
Or la parole du Seigneur me fut adressée en la neuvième année, au dixième mois, au dixième jour du mois, disant:
2 “Mwanadamu, weka kumbukumbu ya tarehe hii, tarehe hii hasa, kwa kuwa mfalme wa Babeli ameuzingira mji wa Yerusalemu kwa jeshi siku hii ya leo.
Fils d’un homme, écris pour toi le nom de ce jour, auquel le roi de Babylone s’est fortifié contre Jérusalem, le jour d’aujourd’hui.
3 Iambie nyumba hii ya kuasi fumbo, na uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Teleka sufuria jikoni; iteleke na umimine maji ndani yake,
Et tu proposeras en figure à la maison provocatrice une parabole, et tu leur diras: Voici ce que dit le Seigneur Dieu: Mets une marmite sur le feu; mets-la, dis-je, et verse de l’eau dedans.
4 Weka vipande vya nyama ndani yake, vipande vyote vizuri, vya paja na vya bega. Ijaze hiyo sufuria kwa mifupa hii mizuri;
Rassembles-y des morceaux de viande, toutes les bonnes parties, la cuisse et l’épaule, les endroits choisis et pleins d’os.
5 chagua yule aliye bora wa kundi la kondoo. Panga kuni chini ya sufuria kwa ajili ya mifupa; chochea mpaka ichemke na uitokose hiyo mifupa ndani yake.
Prends la bête la plus grasse, fais aussi au-dessous une pile de ses os; elle a bouilli à gros bouillons, et ses os ont cuit entièrement au milieu de la marmite.
6 “‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ole wa mji umwagao damu, ole wa sufuria ambayo sasa ina ukoko ndani yake, ambayo ukoko wake hautoki. Kipakue kipande baada ya kipande, bila kuvipigia kura.
À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur Dieu: Malheur à la cité de sang, à la marmite rouillée et dont la rouille ne s’est pas détachée; jettes-en toutes les pièces de viande les unes après les autres; on n’a pas jeté le sort sur elle.
7 “‘Kwa kuwa damu aliyoimwaga ipo katikati yake: huyo mwanamke aliimwaga juu ya mwamba ulio wazi; hakuimwaga kwenye ardhi, ambako vumbi lingeifunika.
Car son sang est au milieu d’elle; c’est sur une pierre très lisse qu’elle l’a répandu: elle ne l’a pas répandu sur la terre, parce qu’il aurait pu être couvert par la poussière.
8 Kuchochea ghadhabu na kulipiza kisasi, nimemwaga damu yake juu ya mwamba ulio wazi, ili isifunikwe.
Afin donc d’amener une indignation sur elle, et de tirer une vengeance complète, j’ai répandu son sang sur une pierre très lisse, pour qu’il ne fût pas couvert.
9 “‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ole wa mji umwagao damu! Mimi nami nitalundikia kuni nyingi.
À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur Dieu: Malheur à la cité de sang, dont je ferai moi-même un grand bûcher.
10 Kwa hiyo lundika kuni na uwashe moto. Pika hiyo nyama vizuri, changanya viungo ndani yake, na uiache mifupa iungue kwenye moto.
Entasse les os que je brûlerai par le feu; toutes les chairs seront consumées, et tout ce qui compose la marmite sera cuit, et les os se fondront.
11 Kisha teleka sufuria tupu kwenye makaa mpaka iwe na moto sana na shaba yake ingʼae, ili uchafu wake upate kuyeyuka na ukoko wake upate kuungua na kuondoka.
Mets-la aussi vide sur des charbons ardents, afin qu’elle s’échauffe et que son airain se liquéfie, que son ordure se fonde au milieu d’elle, et que sa rouille se consume.
12 Imezuia juhudi zote, ukoko wake mwingi haujaondoka, hata ikiwa ni kwa moto.
On a sué avec beaucoup de peine pour la nettoyer, mais sa rouille considérable n’a pas été enlevée même par le feu.
13 “‘Sasa uchafu wako ni uasherati wako. Kwa sababu nilijaribu kukutakasa lakini haikuwezekana kutakaswa kutoka kwenye huo uchafu wako, hutatakasika tena mpaka ghadhabu yangu dhidi yako iwe imepungua.
Ton impureté est exécrable; parce que j’ai voulu te purifier, et tu n’as pas été purifiée de tes ordures; aussi tu ne seras pas purifiée avant que je fasse reposer mon indignation sur toi.
14 “‘Mimi Bwana nimesema, wakati umewadia wa mimi kutenda. Mimi sitazuia, mimi sitaona huruma wala sitapunguza hasira yangu, Utahukumiwa sawasawa na mwenendo na matendo yako, asema Bwana Mwenyezi.’”
Moi le Seigneur j’ai parlé: Le temps viendra et j’agirai; je ne passerai pas outre, et je n’épargnerai pas, et je ne m’apaiserai pas, mais selon Les voies et selon tes inventions je te jugerai, dit le Seigneur.
15 Neno la Bwana likanijia kusema:
Et la parole du Seigneur me fut adressée, disant:
16 “Mwanadamu, kwa pigo moja nakaribia kukuondolea kile kilicho furaha ya macho yako. Lakini usiomboleze au kulia wala kudondosha machozi yoyote.
Fils d’un homme, voici que moi je t’enlève ce qui est désirable à tes yeux, en le frappant d’une plaie, et tu ne te lamenteras pas, et tes larmes ne couleront pas.
17 Lia kwa uchungu kimya kimya usimwombolezee mtu aliyekufa. Jifunge kilemba chako na uvae viatu vyako miguuni mwako, usifunike sehemu ya chini ya uso wako, wala usile vyakula vya kawaida vya wakati wa matanga.”
Gémis en silence, tu ne feras pas le deuil des morts: que ta couronne soit liée sur ta tête, et ta chaussure sera à tes pieds, et tu ne couvriras pas d’un voile ton visage, et tu ne mangeras pas les mets de ceux qui sont dans le deuil.
18 Hivyo nikanena na watu asubuhi na jioni mke wangu akafa. Asubuhi yake nilifanya kama nilivyoamriwa.
Je parlai donc au peuple le matin, et ma femme mourut le soir; et je fis le matin comme Dieu m’avait ordonné.
19 Ndipo watu wakaniuliza, “Je, jambo hili unalofanya linamaanisha nini kwetu?”
Et le peuple me dit; Pourquoi ne nous indiquez-vous pas ce que signifie ce que vous faites?
20 Kwa hiyo nikawaambia, “Neno la Bwana lilinijia kusema:
Et je leur répondis: La parole du Seigneur m’a été adressée, disant:
21 ‘Sema na nyumba ya Israeli. Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninakaribia kupatia unajisi mahali pangu patakatifu, ngome ambayo ndani yake mnaona fahari, furaha ya macho yenu, kitu mnachokipenda. Wana wenu na binti zenu mliowaacha nyuma wataanguka kwa upanga.
Dis à la maison d’Israël: Voici ce que dit le Seigneur Dieu: Voilà que moi je souillerai mon sanctuaire, l’orgueil de votre empire, et le désir de vos yeux, et l’objet de la frayeur de votre âme; vos fils et vos filles que vous avez laissés tomberont sous le glaive.
22 Nanyi mtafanya kama nilivyofanya. Hamtafunika sehemu ya chini ya nyuso zenu wala hamtakula vyakula vya kawaida vya waombolezaji.
Et vous ferez comme j’ai fait: vous ne couvrirez pas d’un voile votre visage, et vous ne mangerez pas les mets de ceux qui sont dans le deuil.
23 Mtajifunga vilemba vichwani mwenu na kuvaa viatu vyenu miguuni mwenu. Hamtaomboleza au kulia, lakini mtadhoofika kwa sababu ya dhambi zenu na kulia kwa uchungu kila mtu na mwenzake.
Vous aurez des couronnes sur vos têtes, et une chaussure à vos pieds; vous ne vous lamenterez pas et vous ne pleurerez pas; mais vous sécherez dans vos iniquités, et chacun gémira sur son frère.
24 Ezekieli atakuwa ishara kwenu, mtafanya kama yeye alivyofanya. Wakati jambo hili litakapotokea, mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’
Et Ezéchiel sera pour vous un signe; selon tout ce que j’ai fait, vous ferez, lorsque sera venu le temps; et vous saurez que je suis le Seigneur Dieu.
25 “Nawe, mwanadamu, siku ile nitakapoondoa ngome yao iliyo furaha yao na utukufu wao, kitu cha kupendeza macho yao, kile kilicho shauku ya mioyo yao, wana wao na binti zao vilevile,
Et loi, fils d’un homme, voici qu’au jour où je leur ôterai leur force, et la gloire de leur dignité, et le désir de leurs yeux, et ce sur quoi se reposent leurs âmes, leurs fils et leurs filles;
26 siku hiyo atakayetoroka atakuja kuwapasha habari.
En ce jour-là viendra un fuyard vers toi, pour te donner des nouvelles;
27 Katika siku ile kinywa chako kitamfumbukia yeye aliyenusurika, nawe utaongea wala hutanyamaza tena. Hivyo wewe utakuwa ishara kwao, nao watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
En ce jour-là, dis-je, ta bouche s’ouvrira avec celui qui a fui; et tu lui parleras, et tu ne demeureras plus dans le silence; tu seras pour eux un signe; et vous saurez que je suis le Seigneur.

< Ezekieli 24 >