< Ezekieli 24 >

1 Katika mwaka wa tisa, mwezi wa kumi, siku ya kumi, neno la Bwana likanijia kusema:
And the word of the LORD came unto me in the ninth year, in the tenth month, in the tenth day of the month, saying:
2 “Mwanadamu, weka kumbukumbu ya tarehe hii, tarehe hii hasa, kwa kuwa mfalme wa Babeli ameuzingira mji wa Yerusalemu kwa jeshi siku hii ya leo.
'Son of man, write thee the name of the day, even of this selfsame day; this selfsame day the king of Babylon hath invested Jerusalem.
3 Iambie nyumba hii ya kuasi fumbo, na uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Teleka sufuria jikoni; iteleke na umimine maji ndani yake,
And utter a parable concerning the rebellious house, and say unto them: Thus saith the Lord GOD: Set on the pot, set it on, and also pour water into it;
4 Weka vipande vya nyama ndani yake, vipande vyote vizuri, vya paja na vya bega. Ijaze hiyo sufuria kwa mifupa hii mizuri;
Gather into it the pieces belonging to it, even every good piece, the thigh, and the shoulder; fill it with the choice bones.
5 chagua yule aliye bora wa kundi la kondoo. Panga kuni chini ya sufuria kwa ajili ya mifupa; chochea mpaka ichemke na uitokose hiyo mifupa ndani yake.
Take the choice of the flock, and pile also the bones under it; make it boil well, that the bones thereof may also be seethed in the midst of it.
6 “‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ole wa mji umwagao damu, ole wa sufuria ambayo sasa ina ukoko ndani yake, ambayo ukoko wake hautoki. Kipakue kipande baada ya kipande, bila kuvipigia kura.
Wherefore thus saith the Lord GOD: Woe to the bloody city, to the pot whose filth is therein, and whose filth is not gone out of it! bring it out piece by piece; no lot is fallen upon it.
7 “‘Kwa kuwa damu aliyoimwaga ipo katikati yake: huyo mwanamke aliimwaga juu ya mwamba ulio wazi; hakuimwaga kwenye ardhi, ambako vumbi lingeifunika.
For her blood is in the midst of her; she set it upon the bare rock; she poured it not upon the ground, to cover it with dust;
8 Kuchochea ghadhabu na kulipiza kisasi, nimemwaga damu yake juu ya mwamba ulio wazi, ili isifunikwe.
that it might cause fury to come up, that vengeance might be taken, I have set her blood upon the bare rock, that it should not be covered.
9 “‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ole wa mji umwagao damu! Mimi nami nitalundikia kuni nyingi.
Therefore thus saith the Lord GOD: Woe to the bloody city! I also will make the pile great,
10 Kwa hiyo lundika kuni na uwashe moto. Pika hiyo nyama vizuri, changanya viungo ndani yake, na uiache mifupa iungue kwenye moto.
heaping on the wood, kindling the fire, that the flesh may be consumed; and preparing the mixture, that the bones also may be burned;
11 Kisha teleka sufuria tupu kwenye makaa mpaka iwe na moto sana na shaba yake ingʼae, ili uchafu wake upate kuyeyuka na ukoko wake upate kuungua na kuondoka.
then will I set it empty upon the coals thereof, that it may be hot, and the bottom thereof may burn, and that the impurity of it may be molten in it, that the filth of it may be consumed.
12 Imezuia juhudi zote, ukoko wake mwingi haujaondoka, hata ikiwa ni kwa moto.
It hath wearied itself with toil; yet its great filth goeth not forth out of it, yea, its noisome filth.
13 “‘Sasa uchafu wako ni uasherati wako. Kwa sababu nilijaribu kukutakasa lakini haikuwezekana kutakaswa kutoka kwenye huo uchafu wako, hutatakasika tena mpaka ghadhabu yangu dhidi yako iwe imepungua.
Because of thy filthy lewdness, because I have purged thee and thou wast not purged, thou shalt not be purged from thy filthiness any more, till I have satisfied My fury upon thee.
14 “‘Mimi Bwana nimesema, wakati umewadia wa mimi kutenda. Mimi sitazuia, mimi sitaona huruma wala sitapunguza hasira yangu, Utahukumiwa sawasawa na mwenendo na matendo yako, asema Bwana Mwenyezi.’”
I the LORD have spoken it; it shall come to pass, and I will do it; I will not go back, neither will I spare, neither will I repent; according to thy ways, and according to thy doings, shall they judge thee, saith the Lord GOD.'
15 Neno la Bwana likanijia kusema:
Also the word of the LORD came unto me, saying:
16 “Mwanadamu, kwa pigo moja nakaribia kukuondolea kile kilicho furaha ya macho yako. Lakini usiomboleze au kulia wala kudondosha machozi yoyote.
'Son of man, behold, I take away from thee the desire of thine eyes with a stroke; yet neither shalt thou make lamentation nor weep, neither shall thy tears run down.
17 Lia kwa uchungu kimya kimya usimwombolezee mtu aliyekufa. Jifunge kilemba chako na uvae viatu vyako miguuni mwako, usifunike sehemu ya chini ya uso wako, wala usile vyakula vya kawaida vya wakati wa matanga.”
Sigh in silence; make no mourning for the dead, bind thy headtire upon thee, and put thy shoes upon thy feet, and cover not thine upper lip, and eat not the bread of men.'
18 Hivyo nikanena na watu asubuhi na jioni mke wangu akafa. Asubuhi yake nilifanya kama nilivyoamriwa.
So I spoke unto the people in the morning, and at even my wife died; and I did in the morning as I was commanded.
19 Ndipo watu wakaniuliza, “Je, jambo hili unalofanya linamaanisha nini kwetu?”
And the people said unto me: 'Wilt thou not tell us what these things are to us, that thou doest so?'
20 Kwa hiyo nikawaambia, “Neno la Bwana lilinijia kusema:
Then I said unto them: 'The word of the LORD came unto me, saying:
21 ‘Sema na nyumba ya Israeli. Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninakaribia kupatia unajisi mahali pangu patakatifu, ngome ambayo ndani yake mnaona fahari, furaha ya macho yenu, kitu mnachokipenda. Wana wenu na binti zenu mliowaacha nyuma wataanguka kwa upanga.
Speak unto the house of Israel: Thus saith the Lord GOD: Behold, I will profane My sanctuary, the pride of your power, the desire of your eyes, and the longing of your soul; and your sons and your daughters whom ye have left behind shall fall by the sword.
22 Nanyi mtafanya kama nilivyofanya. Hamtafunika sehemu ya chini ya nyuso zenu wala hamtakula vyakula vya kawaida vya waombolezaji.
And ye shall do as I have done: ye shall not cover your upper lips, nor eat the bread of men;
23 Mtajifunga vilemba vichwani mwenu na kuvaa viatu vyenu miguuni mwenu. Hamtaomboleza au kulia, lakini mtadhoofika kwa sababu ya dhambi zenu na kulia kwa uchungu kila mtu na mwenzake.
and your tires shall be upon your heads, and your shoes upon your feet; ye shall not make lamentation nor weep; but ye shall pine away in your iniquities, and moan one toward another.
24 Ezekieli atakuwa ishara kwenu, mtafanya kama yeye alivyofanya. Wakati jambo hili litakapotokea, mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’
Thus shall Ezekiel be unto you a sign; according to all that he hath done shall ye do; when this cometh, then shall ye know that I am the Lord GOD.
25 “Nawe, mwanadamu, siku ile nitakapoondoa ngome yao iliyo furaha yao na utukufu wao, kitu cha kupendeza macho yao, kile kilicho shauku ya mioyo yao, wana wao na binti zao vilevile,
And thou, son of man, shall it not be in the day when I take from them their stronghold, the joy of their glory, the desire of their eyes, and the yearning of their soul, their sons and their daughters,
26 siku hiyo atakayetoroka atakuja kuwapasha habari.
that in that day he that escapeth shall come unto thee, to cause thee to hear it with thine ears?
27 Katika siku ile kinywa chako kitamfumbukia yeye aliyenusurika, nawe utaongea wala hutanyamaza tena. Hivyo wewe utakuwa ishara kwao, nao watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
In that day shall thy mouth be opened together with him that is escaped, and thou shalt speak, and be no more dumb; so shalt thou be a sign unto them; and they shall know that I am the LORD.'

< Ezekieli 24 >