< Ezekieli 22 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
И бысть слово Господне ко мне глаголя:
2 “Mwanadamu, je, wewe utauhukumu? Je, utauhukumu huu mji umwagao damu? Basi uujulishe juu ya matendo yake yote ya machukizo
и ты, сыне человечь, аще судити будеши граду кровей, и яви ему вся беззакония его,
3 uuambie: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee mji ule ujileteao maangamizi wenyewe kwa kumwaga damu ndani yake na kujinajisi wenyewe kwa kutengeneza sanamu,
и речеши: сия глаголет Адонаи Господь: о, граде проливаяй кровь среде себе, еже приити времени его, и творяй кумиры на себе, еже осквернитися самому:
4 umekuwa na hatia kwa sababu ya damu uliyomwaga na umetiwa unajisi kwa sanamu ulizotengeneza. Umejiletea mwisho wa siku zako na mwisho wa miaka yako umewadia. Kwa hiyo nitakufanya kitu cha kudharauliwa kwa mataifa na kitu cha mzaha kwa nchi zote.
в крови их, юже излиял еси, согрешил еси, и в кумирех твоих, яже творил, осквернился еси, и сократил еси дни твоя, и привед время лет твоих: сего ради дах тя на укоризну языком и на поругание всем странам,
5 Wale walio karibu na wale walio mbali watakudhihaki, Ewe mji wenye sifa mbaya, uliyejaa ghasia.
близ тебе и далече от тебе сущым, и поругаются тебе и возопиют на тя: о, нечистый, пресловутый и мног во беззакониих!
6 “‘Ona jinsi kila mkuu wa Israeli aliyeko ndani yako anavyotumia nguvu zake kumwaga damu.
Се, старейшины дому Израилева, кийждо ко своим ужикам смесишася в тебе, яко да пролиют кровь:
7 Ndani yako wamewadharau baba na mama, ndani yako wamewatendea wageni udhalimu na kuwaonea yatima na wajane.
отцу и матери злословяху в тебе и ко пришелцу обращахуся неправдами в тебе: сироту и вдовицу преобидяху в тебе:
8 Mmedharau vitu vyangu vitakatifu na kuzinajisi Sabato zangu.
и святая Моя уничижаху и субботы Моя оскверняху в тебе:
9 Ndani yako wako watu wasingiziaji, watu walio tayari kumwaga damu, ndani yako wako wale wanaokula vyakula vilivyotolewa mahali pa ibada za miungu kwenye milima, na kutenda matendo ya uasherati.
мужие разбойницы беша в тебе, яко да пролиют в тебе кровь, и на горах ядяху в тебе и скверны творяху в тебе:
10 Ndani yako wako wale wanaovunjia heshima vitanda vya baba zao, ndani yako wamo wale wanaowatendea wanawake jeuri wakiwa katika hedhi, wakati wakiwa si safi.
стыд отчий открыша в тебе, и в нечистоте седящую обругаша в тебе:
11 Ndani yako mtu hufanya mambo ya machukizo na mke wa jirani yake, mwingine kwa aibu kubwa hukutana kimwili na mke wa mwanawe, mwingine humtenda jeuri dada yake, binti wa baba yake hasa.
кийждо на жену подруга своего беззаконноваша, и кийждо невестку свою оскверняше в нечестии, и кийждо сестру свою, дщерь отца своего, обругаваше в тебе:
12 Ndani yako watu hupokea rushwa ili kumwaga damu, mnapokea riba na faida ya ziada na kupata faida isiyokuwa halali kutoka kwa jirani ili kupata faida kubwa kupita kiasi. Nawe umenisahau mimi, asema Bwana Mwenyezi.
мзды взимаху в тебе, яко да пролиют кровь, лихву и избыток взимаху в тебе: и скончал еси скончание злобы твоея яже в насилии, Мене же забыл еси, глаголет Адонаи Господь.
13 “‘Hakika nitapiga makofi kwa ajili ya faida isiyo halali uliyojipatia na kwa damu uliyoimwaga ndani yako.
Се убо, ударю рукою Моею о руку Мою на та, яже совершил еси и яже сотворил еси, и на крови твоя бывшыя посреде тебе:
14 Je, ujasiri wako utadumu au mikono yako itakuwa na nguvu siku hiyo nitakapokushughulikia? Mimi Bwana nimesema na nitalifanya.
аще устоит сердце твое, и аще преодолеют руце твои во днех, в няже Аз творю в тебе? Аз Господь глаголах, и сотворю.
15 Nitakutawanya miongoni mwa mataifa na kukutapanya katika nchi mbalimbali nami nitakomesha unajisi wako.
И разсыплю тя во языцех и разсею тя в странах, и оскудеет нечистота твоя из тебе,
16 Ukiisha kunajisika mbele ya mataifa, utajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”
и владети буду тобою пред очима языков, и познаеши, яко Аз Господь.
17 Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
И бысть слово Господне ко мне глаголя:
18 “Mwanadamu, nyumba ya Israeli imekuwa kwangu takataka ya chuma, wote kwangu wamekuwa shaba, bati, chuma na risasi iliyoachwa kalibuni. Wao ni taka ya madini ya fedha tu.
сыне человечь, се, быша Мне дом Израилев смешани вси с медию и железом, и со оловом чистым и со свинцем, среде пещи сребро смешено суть.
19 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa kuwa wote mmekuwa takataka ya chuma, nitawakusanya Yerusalemu.
Сего ради рцы: сия глаголет Адонаи Господь: понеже бысте вси во смешение едино, сего ради, се, Аз прииму вас во средину Иерусалима:
20 Kama vile watu wakusanyavyo fedha, shaba, chuma, risasi na bati kalibuni ili kuyeyusha kwa moto mkali, ndivyo nitakavyowakusanya katika hasira yangu na ghadhabu yangu kuwaweka ndani ya mji na kuwayeyusha.
якоже приемлется сребро и медь, и железо и свинец и олово чистое во средину пещи, еже дунути на ня огню, да слиются, тако прииму вас во гневе Моем и в ярости Моей, и соберу и слию вас,
21 Nitawakusanya na kupuliza juu yenu moto wa hasira yangu na ghadhabu yangu nanyi mtayeyushwa ndani ya huo mji.
и дуну на вы во огни гнева Моего, и слияни будете среде его:
22 Kama fedha iyeyukavyo kalibuni, ndivyo mtakavyoyeyuka ndani ya huo mji, nanyi mtajua kuwa Mimi Bwana nimemwaga ghadhabu yangu juu yenu.’”
якоже сливается сребро среде пещи, тако слиетеся посреде его и познаете, яко Аз Господь излиях ярость Мою на вас.
23 Neno la Bwana likanijia tena kusema:
И бысть слово Господне ко мне глаголя:
24 “Mwanadamu, iambie nchi, ‘Wewe ni nchi ambayo haijapata mvua wala manyunyu katika siku ya ghadhabu.’
сыне человечь, рцы ему: ты еси земля неодождимая, ниже дождь бысть на тя в день ярости.
25 Kuna hila mbaya ya wakuu ndani yake kama simba angurumaye akirarua mawindo yake, wanakula watu, wanachukua hazina na vitu vya thamani na kuongeza idadi ya wajane ndani yake.
Егоже старейшины среде его, яко львы рыкающе, восхищающе восхищения, душы изядающе насилием, богатство и честь приемлюще, и вдовицы твоя умножишася посреде тебе:
26 Makuhani wake wameihalifu sheria yangu na kunajisi vitu vyangu vitakatifu, hawatofautishi kati ya vitu vitakatifu na vitu vya kawaida. Wanafundisha kuwa hakuna tofauti kati ya vitu vilivyo najisi na visivyo najisi, nao wanafumba macho yao katika kutunza Sabato zangu, hivyo katikati yao nimetiwa unajisi.
и жерцы его отвергошася закона Моего и оскверниша святая Моя: между святым и сквернавым не разлучаху, и между нечистым и чистым не разделяху, и от суббот Моих покрываху очи свои, и оскверняху Мя посреде себе:
27 Maafisa wake walioko ndani yake ni kama mbwa mwitu wararuao mawindo yao, wanamwaga damu na kuua watu ili kupata faida ya udhalimu.
князи его среде его яко волцы восхищающе похищения, еже пролияти кровь и погубити душы, яко да лихоимством лихоимствуют:
28 Manabii wake wanapaka chokaa matendo haya kwa maono ya uongo na utabiri wa udanganyifu. Wanasema, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo,’ wakati Bwana hajasema.
и пророцы его помазующии их падут, видящии суетная, волхвующии ложная, глаголюще: сия глаголет Адонаи Господь: а Господь не глагола.
29 Watu wa nchi wanatoza kwa nguvu na kufanya unyangʼanyi, wanawatenda jeuri maskini na wahitaji na kuwaonea wageni, wakiwanyima haki.
Людий земли утесняюще неправдою и восхищающе восхищения, нища и убога насильствующе и со пришелцем не живуще судом.
30 “Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, ambaye angejenga ukuta na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka kwa ajili ya watu wa nchi ili nisije nikaiangamiza, lakini sikumwona mtu yeyote.
И исках от них мужа живуща право и стояща цело пред лицем Моим во время гнева Моего, еже бы не до конца погубити его, и не обретох.
31 Hivyo nitaimwaga ghadhabu yangu juu yao na kuwateketeza kwa moto wa hasira yangu, nikiyaleta juu ya vichwa vyao yale yote waliyotenda, asema Bwana Mwenyezi.”
И излиях нань ярость Мою во огни гнева Моего, еже скончати я: пути их на главы их дах, глаголет Адонаи Господь.

< Ezekieli 22 >