< Ezekieli 21 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
In k meni je prišla Gospodova beseda, rekoč:
2 “Mwanadamu, uelekeze uso wako juu ya Yerusalemu na uhubiri dhidi ya mahali patakatifu. Tabiri dhidi ya nchi ya Israeli
»Človeški sin, naravnaj svoj obraz proti Jeruzalemu in spusti svojo besedo proti svetim krajem in prerokuj zoper Izraelovo deželo
3 uiambie: ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Mimi niko kinyume nawe. Nitautoa upanga wangu kwenye ala yake na kumkatilia mbali mwenye haki na mwovu.
in reci Izraelovi deželi: ›Tako govori Gospod: ›Glej, jaz sem zoper tebe in izvlekel bom svoj meč iz nožnice in iz tebe bom iztrebil pravičnega in zlobnega.
4 Kwa sababu nitamkatilia mbali mwenye haki na mwovu, upanga wangu utakuwa wazi dhidi ya kila mmoja kuanzia kusini mpaka kaskazini.
Ker bom iz tebe iztrebil pravičnega in zlobnega, bo zato moj meč šel iz nožnice zoper vse meso od juga do severa,
5 Ndipo watu wote watajua ya kuwa Mimi Bwana nimeutoa upanga wangu kwenye ala yake, nao hautarudi humo tena.’
da bo lahko vse meso vedelo, da sem jaz, Gospod, izvlekel svoj meč iz nožnice. Ta se ne bo več vrnil.
6 “Kwa hiyo lia kwa uchungu, mwanadamu! Lia kwa uchungu mbele yao kwa moyo uliopondeka na kwa huzuni nyingi.
Zdihuj torej, ti, človeški sin, s trganjem svojih ledij; in z grenkim vzdihom pred njihovimi očmi.
7 Nao watakapokuuliza, ‘Kwa nini unalia kwa uchungu?’ Utasema hivi, ‘Kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila moyo utayeyuka na kila mkono utalegea, kila roho itazimia na kila goti litalegea kama maji.’ Habari hizo zinakuja! Hakika zitatokea, asema Bwana Mwenyezi.”
In zgodilo se bo, ko ti bodo rekli: ›Zakaj vzdihuješ?‹ da boš odgovoril: ›Zaradi novic, ker le-te prihajajo.‹ In vsako srce se bo stopilo in vse roke bodo slabotne in vsak duh bo medlel in vsa kolena bodo šibka kakor voda. Glej, to prihaja in se bo zgodilo, ‹ govori Gospod Bog.«
8 Neno la Bwana likanijia, kusema:
Ponovno je prišla k meni Gospodova beseda, rekoč:
9 “Mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Upanga, upanga, ulionolewa na kusuguliwa:
»Človeški sin, prerokuj in reci: ›Tako govori Gospod: ›Reci: ›Meč, meč je nabrušen in tudi zglajen.
10 umenolewa kwa ajili ya mauaji, umesuguliwa ili ungʼae kama umeme wa radi! “‘Je, tuifurahie fimbo ya utawala ya mwanangu Yuda? Upanga unaidharau kila fimbo ya namna hiyo.
Nabrušen je, da naredi boleč pokol; zglajen je, da se lahko lesketa. Naj bi se mi potem razveseljevali? Ta zaničuje palico mojega sina kakor vsako drevo.
11 “‘Upanga umewekwa tayari ili kusuguliwa, ili upate kushikwa mkononi, umenolewa na kusuguliwa, umewekwa tayari kwa mkono wa muuaji.
In on ga je dal zgladiti, da bi lahko z njim rokoval. Ta meč je nabrušen in zglajen, da ga da v roko ubijalca.
12 Piga kelele na uomboleze, ee mwanadamu, kwa kuwa upanga u dhidi ya watu wangu; u dhidi ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa wauawe kwa upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo pigapiga kifua chako.
Jokaj in tuli, človeški sin, kajti ta bo nad mojim ljudstvom, ta bo nad Izraelovimi princi. Strahote zaradi meča bodo nad mojim ljudstvom. Udari torej na svoje stegno.
13 “‘Kwa maana upanga huu umejaribiwa na kuhakikishwa, itakuwaje basi fimbo ya ufalme ya Yuda inayoudharau kama haitakuwepo tena, bali itakuwa imeondolewa kabisa? asema Bwana Mwenyezi.’
Ker je to preizkušnja in kaj če meč zaničuje celo palico? To ne bo več, ‹ govori Gospod Bog.
14 “Hivyo basi, mwanadamu, tabiri na ukapige makofi. Upanga wako na upige mara mbili, naam, hata mara tatu. Ni upanga wa kuchinja, upanga wa mauaji makuu, ukiwashambulia kutoka kila upande.
›Ti torej, človeški sin, prerokuj in zaploskaj s svojima rokama in naj bo meč tretjič podvojen, meč umorjenih. To je meč velikih ljudi, ki so umorjeni, ki vstopa v njihove skrivne sobe.
15 Ili mioyo ipate kuyeyuka na wanaouawa wawe wengi, nimeweka upanga wa kuchinja kwenye malango yao yote. Lo! Umetengenezwa umetemete kama umeme wa radi, umeshikwa kwa ajili ya kuua.
Konico meča sem naravnal zoper vsa njihova velika vrata, da bo njihovo srce lahko slabelo in [bodo] njihovi propadi pomnoženi. Ah! Narejen je [da se] lesketa, zavit je za pokol.
16 Ee upanga, kata upande wa kuume, kisha upande wa kushoto, mahali popote makali yako yatakapoelekezwa.
Pojdi eno pot ali drugo, ali na desno ali na levo, kamor je naravnan tvoj obraz.
17 Mimi nami nitapiga makofi, nayo ghadhabu yangu itapungua. Mimi Bwana nimesema.”
Tudi jaz bom plosknil s svojima rokama in bom umiril svojo razjarjenost. Jaz, Gospod, sem to govoril.‹«
18 Neno la Bwana likanijia kusema:
Ponovno je prišla k meni Gospodova beseda, rekoč:
19 “Mwanadamu, weka alama njia mbili ambazo upanga wa mfalme wa Babeli utapitia, njia hizo zikianzia katika nchi hiyo hiyo. Weka kibao pale ambapo njia zinagawanyika kuelekea mjini.
»Tudi ti, človeški sin, si določi dve poti, da bo lahko prišel meč babilonskega kralja. Obe bosta izšli iz ene dežele in izberi kraj, izberi ga ob začetku poti v mesto.
20 Weka alama njia moja kwa ajili ya upanga upate kuja dhidi ya Raba ya Waamoni na nyingine upate kuja dhidi ya Yuda na Yerusalemu iliyozungushiwa ngome.
Določi pot, da lahko pride meč v Rabo Amóncev in v Juda in zaščiteno [prestolnico] Jeruzalem.
21 Kwa kuwa mfalme wa Babeli sasa amesimama katika njia panda, katika makutano ya njia mbili, akipiga ramli: anapiga kura kwa kutumia mishale, anataka shauri kwa sanamu zake, anachunguza maini ya wanyama.
Kajti babilonski kralj je stal pri razpotju poti, ob začetku dveh poti, da uporabi vedeževanje. Svoje puščice je posvetlil, posvetoval se je z družinskimi maliki, gledal je v jetra.
22 Upande wake wa kuume inakuja kura ya Yerusalemu, ambapo ataweka vyombo vya kuvunjia boma, ili kuamrisha mauaji, kupiga ukelele wa vita, kuweka vyombo vya kuvunjia boma kwenye malango, kuweka jeshi kuzunguka na kufanya uzingiraji.
Pri njegovi desni roki je bilo vedeževanje za [prestolnico] Jeruzalem, da določi častnike, da odpre usta v pokol, da povzdigne glas s kričanjem, da določi oblegovalne ovne proti velikim vratom, da nasuje nasip in da zgradi utrdbo.
23 Itakuwa kama kupiga ramli kwa uongo kwa wale watu ambao wameapa kumtii yeye. Lakini mfalme wa Babeli atawakumbusha juu ya uovu wao na kuwachukua mateka.
In to jim bo kakor napačno vedeževanje v njihovem pogledu, tistim, ki so prisegli prisege, toda v spomin bo priklical krivičnost, da bodo lahko zajeti.‹
24 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu enyi watu mmekumbusha uovu wenu kwa kuasi waziwazi, mkidhihirisha dhambi zenu katika yale yote mfanyayo, kwa kuwa mmefanya jambo hili, mtachukuliwa mateka.
Zato tako govori Gospod Bog: ›Ker ste storili, da se bo spominjalo vaše krivičnosti v tem, da so vaši prestopki odkriti, tako da se pri vseh vaših dejanjih pojavijo vaši grehi; ker jaz pravim, da ste prišli v spomin, boste zajeti z roko.
25 “‘Ee mtawala kafiri na mwovu wa Israeli, ambaye siku yako imewadia, ambaye wakati wako wa adhabu umefikia kilele chake,
In ti, oskrunjen, zloben Izraelov princ, katerega dan je prišel, ko se krivičnosti naredi konec, ‹
26 hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Vua kilemba, ondoa taji. Kwa kuwa mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa. Aliye mnyonge atakwezwa na aliyekwezwa atashushwa.
tako govori Gospod Bog: ›Odstrani diadem in snemi krono. To ne bo [več] isto. Povišaj tistega, ki je nizek in ponižaj tistega, ki je visok.
27 Mahame! Mahame! Nitaufanya mji kuwa mahame! Hautajengwa upya mpaka aje yule ambaye ndiye mwenye haki nao; yeye ndiye nitakayempa.’
Jaz bom to preobrnil, preobrnil, preobrnil in tega ne bo nič več, dokler ne pride tisti, katerega pravica je to in njemu jo bom izročil.‹
28 “Nawe, mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu Waamoni na matukano yao. “‘Upanga, upanga, umefutwa kwa ajili ya kuua, umesuguliwa ili kuangamiza na unametameta kama umeme wa radi!
Ti pa, človeški sin, prerokuj in reci: ›Tako govori Gospod Bog glede Amóncev in glede njihove graje; celo reci: ›Meč, meč je izvlečen. Za pokol je zglajen, da použiva zaradi lesketanja.
29 Wakati wakitoa maono ya uongo kwa ajili yako, wanapobashiri uongo kwa ajili yako, wanakuweka wewe kwenye shingo za watu wapotovu, wale walio waovu, wale ambao siku yao imewadia, wakati wa adhabu yao ya mwisho.
Medtem ko zate vidijo ničnost, medtem ko ti vedežujejo laž, da te privedejo nad vratove tistih, ki so umorjeni izmed zlobnih, katerih dan je prišel, ko bo njihova krivičnost končana.
30 Urudishe upanga kwenye ala yake! Katika mahali ulipoumbiwa, katika nchi ya baba zako, huko nitakuhukumu.
Ali mu bom povzročil, da se vrne v svojo nožnico? Sodil te bom na kraju, kjer si bil ustvarjen, v deželi tvojega rojstva.
31 Nitamwaga ghadhabu yangu juu yako na kupuliza moto wa hasira yangu dhidi yako; nitakutia mikononi mwa watu wakatili, watu stadi katika kuangamiza.
In nate bom izlil svoje ogorčenje in zoper tebe bom pihal v ognju svojega besa in te izročil v roko brutalnežev in veščih, da uničujejo.
32 Mtakuwa kuni za kuwashia moto, damu yenu itamwagwa katika nchi yenu, wala hamtakumbukwa tena; kwa maana Mimi Bwana nimesema.’”
Ti boš za gorivo ognju; tvoja kri bo v sredi dežele; ne bo se te več spominjalo, kajti jaz, Gospod, sem to govoril.‹«

< Ezekieli 21 >