< Ezekieli 21 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
E veiu a mim a palavra do Senhor, dizendo:
2 “Mwanadamu, uelekeze uso wako juu ya Yerusalemu na uhubiri dhidi ya mahali patakatifu. Tabiri dhidi ya nchi ya Israeli
Filho do homem, dirige o teu rosto contra Jerusalem, e derrama as tuas palavras contra os sanctuarios, e prophetiza contra a terra de Israel.
3 uiambie: ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Mimi niko kinyume nawe. Nitautoa upanga wangu kwenye ala yake na kumkatilia mbali mwenye haki na mwovu.
E dize á terra de Israel: Assim diz o Senhor: Eis me aqui contra ti, e tirarei a minha espada da sua bainha, e exterminarei do meio de ti o justo e o impio.
4 Kwa sababu nitamkatilia mbali mwenye haki na mwovu, upanga wangu utakuwa wazi dhidi ya kila mmoja kuanzia kusini mpaka kaskazini.
E, porquanto hei de exterminar do meio de ti o justo e o impio, por isso sairá a minha espada da sua bainha contra toda a carne, desde o sul até ao norte.
5 Ndipo watu wote watajua ya kuwa Mimi Bwana nimeutoa upanga wangu kwenye ala yake, nao hautarudi humo tena.’
E saberá toda a carne que eu, o Senhor, tirei a minha espada da sua bainha: nunca mais voltará a ella.
6 “Kwa hiyo lia kwa uchungu, mwanadamu! Lia kwa uchungu mbele yao kwa moyo uliopondeka na kwa huzuni nyingi.
Tu, porém, ó filho do homem, suspira; suspira aos olhos d'elles, com quebrantamento dos lombos e com amargura.
7 Nao watakapokuuliza, ‘Kwa nini unalia kwa uchungu?’ Utasema hivi, ‘Kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila moyo utayeyuka na kila mkono utalegea, kila roho itazimia na kila goti litalegea kama maji.’ Habari hizo zinakuja! Hakika zitatokea, asema Bwana Mwenyezi.”
E será que, quando elles te disserem: Porque suspiras tu? dirás: Pela fama, porque já vem; e todo o coração desmaiará, e todas as mãos se enfraquecerão, e todo o espirito se angustiará, e todos os joelhos se desfarão em aguas; eis que já vem, e se fará, diz o Senhor Jehovah.
8 Neno la Bwana likanijia, kusema:
E veiu a mim a palavra do Senhor, dizendo:
9 “Mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Upanga, upanga, ulionolewa na kusuguliwa:
Filho do homem, prophetiza, e dize: Assim diz o Senhor: dize: A espada, a espada está afiada, e tambem açacalada.
10 umenolewa kwa ajili ya mauaji, umesuguliwa ili ungʼae kama umeme wa radi! “‘Je, tuifurahie fimbo ya utawala ya mwanangu Yuda? Upanga unaidharau kila fimbo ya namna hiyo.
Para matar com grande matança está afiada, para reduzir está açacalada: alegrar-nos-hemos pois? a vara de meu filho é que despreza todo o madeiro.
11 “‘Upanga umewekwa tayari ili kusuguliwa, ili upate kushikwa mkononi, umenolewa na kusuguliwa, umewekwa tayari kwa mkono wa muuaji.
E a deu a açacalar, para usar d'ella com a mão: esta espada está afiada, e está açacalada, para a metter na mão do que está para matar.
12 Piga kelele na uomboleze, ee mwanadamu, kwa kuwa upanga u dhidi ya watu wangu; u dhidi ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa wauawe kwa upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo pigapiga kifua chako.
Grita e uiva, ó filho do homem, porque esta será contra o meu povo, será contra todos os principes de Israel: espantos terá o meu povo por causa da espada; portanto bate na côxa.
13 “‘Kwa maana upanga huu umejaribiwa na kuhakikishwa, itakuwaje basi fimbo ya ufalme ya Yuda inayoudharau kama haitakuwepo tena, bali itakuwa imeondolewa kabisa? asema Bwana Mwenyezi.’
Quando se fez a prova que havia então? porventura tambem não haveria vara desprezadora? diz o Senhor Jehovah.
14 “Hivyo basi, mwanadamu, tabiri na ukapige makofi. Upanga wako na upige mara mbili, naam, hata mara tatu. Ni upanga wa kuchinja, upanga wa mauaji makuu, ukiwashambulia kutoka kila upande.
Tu pois, ó filho do homem, prophetiza, e bate com as mãos uma na outra; porque a espada até á terceira vez se dobrará: a espada é dos atravessados grandes, que entrará a elles até nas recamaras.
15 Ili mioyo ipate kuyeyuka na wanaouawa wawe wengi, nimeweka upanga wa kuchinja kwenye malango yao yote. Lo! Umetengenezwa umetemete kama umeme wa radi, umeshikwa kwa ajili ya kuua.
Para que desmaie o coração, e se multipliquem os tropeços, contra todas as suas portas puz a ponta da espada, a que foi feita para reduzir, e está reservada para matar!
16 Ee upanga, kata upande wa kuume, kisha upande wa kushoto, mahali popote makali yako yatakapoelekezwa.
Ó espada, reune-te, vira-te para a direita; prepara-te, vira-te para a esquerda, para onde quer que o teu rosto se dirigir.
17 Mimi nami nitapiga makofi, nayo ghadhabu yangu itapungua. Mimi Bwana nimesema.”
E tambem eu baterei com as minhas mãos uma na outra, e farei descançar a minha indignação: eu, o Senhor, o fallei.
18 Neno la Bwana likanijia kusema:
E veiu a mim a palavra do Senhor, dizendo:
19 “Mwanadamu, weka alama njia mbili ambazo upanga wa mfalme wa Babeli utapitia, njia hizo zikianzia katika nchi hiyo hiyo. Weka kibao pale ambapo njia zinagawanyika kuelekea mjini.
Tu pois, ó filho do homem, propõe dois caminhos, por onde venha a espada do rei de Babylonia: ambos procederão de uma mesma terra, e escolhe uma banda; no cimo do caminho da cidade o escolhe.
20 Weka alama njia moja kwa ajili ya upanga upate kuja dhidi ya Raba ya Waamoni na nyingine upate kuja dhidi ya Yuda na Yerusalemu iliyozungushiwa ngome.
Um caminho proporás, por onde virá a espada contra Rabba dos filhos d'Ammon, e contra Judah, em Jerusalem, a fortificada.
21 Kwa kuwa mfalme wa Babeli sasa amesimama katika njia panda, katika makutano ya njia mbili, akipiga ramli: anapiga kura kwa kutumia mishale, anataka shauri kwa sanamu zake, anachunguza maini ya wanyama.
Porque o rei de Babylonia parará na encruzilhada, no cimo dos dois caminhos, para usar de adivinhações: aguçará as suas frechas, consultará os terafins, attentará para o figado
22 Upande wake wa kuume inakuja kura ya Yerusalemu, ambapo ataweka vyombo vya kuvunjia boma, ili kuamrisha mauaji, kupiga ukelele wa vita, kuweka vyombo vya kuvunjia boma kwenye malango, kuweka jeshi kuzunguka na kufanya uzingiraji.
Á sua direita estará a adivinhação sobre Jerusalem, para ordenar os arietes, para abrir a bocca á matança, para levantar a voz com jubilo, para pôr os arietes contra as portas, para levantar uma tranqueira, para edificar um baluarte.
23 Itakuwa kama kupiga ramli kwa uongo kwa wale watu ambao wameapa kumtii yeye. Lakini mfalme wa Babeli atawakumbusha juu ya uovu wao na kuwachukua mateka.
Isto será aos olhos d'elles como adivinhação vã, porquanto foram ajuramentados com juramentos entre elles; porém elle se lembrará da maldade, para que sejam apanhados.
24 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu enyi watu mmekumbusha uovu wenu kwa kuasi waziwazi, mkidhihirisha dhambi zenu katika yale yote mfanyayo, kwa kuwa mmefanya jambo hili, mtachukuliwa mateka.
Portanto assim diz o Senhor Jehovah: Porquanto me fazeis lembrar da vossa maldade, descobrindo-se as vossas prevaricações, apparecendo os vossos peccados em todos os vossos tratos, porquanto viestes em memoria, sereis apanhados na mão.
25 “‘Ee mtawala kafiri na mwovu wa Israeli, ambaye siku yako imewadia, ambaye wakati wako wa adhabu umefikia kilele chake,
E tu, ó profano e impio principe d'Israel, cujo dia virá no campo da extrema maldade,
26 hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Vua kilemba, ondoa taji. Kwa kuwa mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa. Aliye mnyonge atakwezwa na aliyekwezwa atashushwa.
Assim diz o Senhor Jehovah: Tira para fóra o diadema, e levanta de ti a corôa; esta não será a mesma; exalta ao humilde, e humilha ao soberbo.
27 Mahame! Mahame! Nitaufanya mji kuwa mahame! Hautajengwa upya mpaka aje yule ambaye ndiye mwenye haki nao; yeye ndiye nitakayempa.’
Ao revéz, ao revéz, ao revéz porei aquella corôa, e ella mais não será, até que venha aquelle a quem pertence de direito, e a elle a darei.
28 “Nawe, mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu Waamoni na matukano yao. “‘Upanga, upanga, umefutwa kwa ajili ya kuua, umesuguliwa ili kuangamiza na unametameta kama umeme wa radi!
E tu, ó filho do homem, prophetiza, e dize: Assim diz o Senhor Jehovah ácerca dos filhos de Ammon, e ácerca do seu desprezo: dize pois: A espada, a espada está desembainhada, açacalada para a matança, para consumir, para reluzir;
29 Wakati wakitoa maono ya uongo kwa ajili yako, wanapobashiri uongo kwa ajili yako, wanakuweka wewe kwenye shingo za watu wapotovu, wale walio waovu, wale ambao siku yao imewadia, wakati wa adhabu yao ya mwisho.
Entretanto que te vêem vaidade, entretanto que te adivinham mentira, para te pôrem aos pescoços dos traspassados pelos impios, cujo dia virá no tempo da extrema maldade.
30 Urudishe upanga kwenye ala yake! Katika mahali ulipoumbiwa, katika nchi ya baba zako, huko nitakuhukumu.
Torna a tua espada á sua bainha: no logar em que foste creado, na terra do teu nascimento, julgarei.
31 Nitamwaga ghadhabu yangu juu yako na kupuliza moto wa hasira yangu dhidi yako; nitakutia mikononi mwa watu wakatili, watu stadi katika kuangamiza.
E derramarei sobre ti a minha indignação, assoprarei contra ti o fogo do meu furor, entregar-te-hei nas mãos dos homens fogosos, inventores de destruição.
32 Mtakuwa kuni za kuwashia moto, damu yenu itamwagwa katika nchi yenu, wala hamtakumbukwa tena; kwa maana Mimi Bwana nimesema.’”
Para o fogo servirás de pasto: o teu sangue será no meio da terra: não virás em memoria; porque eu, o Senhor, o fallei.

< Ezekieli 21 >