< Ezekieli 21 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de l’Eternel me fut adressée en ces termes:
2 “Mwanadamu, uelekeze uso wako juu ya Yerusalemu na uhubiri dhidi ya mahali patakatifu. Tabiri dhidi ya nchi ya Israeli
"Fils de l’homme, dirige ta face vers Jérusalem, prêche sur les sanctuaires et prophétise sur la terre d’Israël.
3 uiambie: ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Mimi niko kinyume nawe. Nitautoa upanga wangu kwenye ala yake na kumkatilia mbali mwenye haki na mwovu.
Tu diras au pays d’Israël: Ainsi parle l’Eternel: Me voici contre toi, je sortirai mon épée de son fourreau et j’extirperai de toi justes et impies.
4 Kwa sababu nitamkatilia mbali mwenye haki na mwovu, upanga wangu utakuwa wazi dhidi ya kila mmoja kuanzia kusini mpaka kaskazini.
Parce que je veux extirper de toi justes et impies, c’est pourquoi mon épée sortira de son fourreau contre toute chair du Sud au Nord.
5 Ndipo watu wote watajua ya kuwa Mimi Bwana nimeutoa upanga wangu kwenye ala yake, nao hautarudi humo tena.’
Et toute chair saura que c’est moi, l’Eternel, qui ai tiré mon épée du fourreau: elle n’y rentrera plus.
6 “Kwa hiyo lia kwa uchungu, mwanadamu! Lia kwa uchungu mbele yao kwa moyo uliopondeka na kwa huzuni nyingi.
Et toi, fils de l’homme, pousse des soupirs: les reins brisés, dans l’amertume, pousse des soupirs à leurs yeux.
7 Nao watakapokuuliza, ‘Kwa nini unalia kwa uchungu?’ Utasema hivi, ‘Kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila moyo utayeyuka na kila mkono utalegea, kila roho itazimia na kila goti litalegea kama maji.’ Habari hizo zinakuja! Hakika zitatokea, asema Bwana Mwenyezi.”
Alors s’ils te disent: "Pourquoi soupires-tu?" tu répondras: "C’Est à cause de la nouvelle qui arrive, qui fait fondre tous les coeurs, défaillir toutes les mains, se troubler tous les esprits, s’en aller en eau tous les genoux; elle arrive et s’accomplit dit le Seigneur Dieu."
8 Neno la Bwana likanijia, kusema:
La parole de l’Eternel me fut adressée en ces termes:
9 “Mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Upanga, upanga, ulionolewa na kusuguliwa:
"Fils de l’homme, prophétise et dis: Ainsi parle le Seigneur: Dis qu’une épée, une épée a été aiguisée et polie.
10 umenolewa kwa ajili ya mauaji, umesuguliwa ili ungʼae kama umeme wa radi! “‘Je, tuifurahie fimbo ya utawala ya mwanangu Yuda? Upanga unaidharau kila fimbo ya namna hiyo.
C’Est pour procéder à la tuerie qu’elle a été aiguisée, c’est pour qu’elle jette des éclairs qu’elle a été polie. Ou se peut-il que nous connaissions encore la joie? La verge qui frappe mon fils voit avec dédain tout instrument de bois.
11 “‘Upanga umewekwa tayari ili kusuguliwa, ili upate kushikwa mkononi, umenolewa na kusuguliwa, umewekwa tayari kwa mkono wa muuaji.
Il l’a donnée à polir pour qu’on la saisisse par la main; on l’a aiguisée, l’épée, et on l’a polie pour la mettre en la main du meurtrier.
12 Piga kelele na uomboleze, ee mwanadamu, kwa kuwa upanga u dhidi ya watu wangu; u dhidi ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa wauawe kwa upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo pigapiga kifua chako.
Crie et lamente-toi, fils de l’homme, car cette épée a sévi sur mon peuple, elle a sévi sur tous les princes d’Israël; ils ont été livrés à l’épée avec mon peuple, c’est pourquoi frappe-toi la hanche.
13 “‘Kwa maana upanga huu umejaribiwa na kuhakikishwa, itakuwaje basi fimbo ya ufalme ya Yuda inayoudharau kama haitakuwepo tena, bali itakuwa imeondolewa kabisa? asema Bwana Mwenyezi.’
C’Est une épreuve. Et que sera-ce s’il s’y ajoute la verge dédaigneuse? Rien ne sera plus, dit le Seigneur Dieu.
14 “Hivyo basi, mwanadamu, tabiri na ukapige makofi. Upanga wako na upige mara mbili, naam, hata mara tatu. Ni upanga wa kuchinja, upanga wa mauaji makuu, ukiwashambulia kutoka kila upande.
Et toi, fils de l’homme, prophétise et frappe d’une main contre l’autre et que l’épée redouble ses coups par trois fois! C’Est une épée de massacres, l’épée de la grande victime qui les pourchasse.
15 Ili mioyo ipate kuyeyuka na wanaouawa wawe wengi, nimeweka upanga wa kuchinja kwenye malango yao yote. Lo! Umetengenezwa umetemete kama umeme wa radi, umeshikwa kwa ajili ya kuua.
C’Est afin de faire fondre les coeurs et de multiplier les chutes auprès de toutes leurs portes, que j’ai brandi le brillant de l’épée; ah! Elle est préparée pour étinceler et aiguisée pour tuer.
16 Ee upanga, kata upande wa kuume, kisha upande wa kushoto, mahali popote makali yako yatakapoelekezwa.
Sois tranchante à droite, avance à gauche, partout où tes lames sont dirigées.
17 Mimi nami nitapiga makofi, nayo ghadhabu yangu itapungua. Mimi Bwana nimesema.”
Et moi aussi, je frapperai d’une main contre l’autre et j’assouvirai ma colère, moi, l’Eternel, je l’ai dit."
18 Neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de l’Eternel me fut adressée en ces termes:
19 “Mwanadamu, weka alama njia mbili ambazo upanga wa mfalme wa Babeli utapitia, njia hizo zikianzia katika nchi hiyo hiyo. Weka kibao pale ambapo njia zinagawanyika kuelekea mjini.
"O toi, fils de l’homme, fais-toi deux chemins par où vienne l’épée du roi de Babylone; ils doivent partir tous deux d’un même pays; et grave une main indicatrice, grave-la au point de départ du chemin de la ville.
20 Weka alama njia moja kwa ajili ya upanga upate kuja dhidi ya Raba ya Waamoni na nyingine upate kuja dhidi ya Yuda na Yerusalemu iliyozungushiwa ngome.
Fais un chemin par où vienne l’épée contre Rabba capitale des fils d’Ammon et contre Juda dans Jérusalem la forte.
21 Kwa kuwa mfalme wa Babeli sasa amesimama katika njia panda, katika makutano ya njia mbili, akipiga ramli: anapiga kura kwa kutumia mishale, anataka shauri kwa sanamu zake, anachunguza maini ya wanyama.
Car le roi de Babylone s’est porté à la naissance du chemin, au commencement des deux chemins, pour consulter le sort; il a agité les flèches, interrogé les Teraphim, examiné le foie.
22 Upande wake wa kuume inakuja kura ya Yerusalemu, ambapo ataweka vyombo vya kuvunjia boma, ili kuamrisha mauaji, kupiga ukelele wa vita, kuweka vyombo vya kuvunjia boma kwenye malango, kuweka jeshi kuzunguka na kufanya uzingiraji.
Dans sa main droite se trouvait le sort "Jérusalem" pour y dresser des béliers, y proclamer la tuerie, pour y proférer des cris de guerre, pour dresser des béliers contre (es portes, pour y jeter une chaussée et bâtir des ouvrages de siège.
23 Itakuwa kama kupiga ramli kwa uongo kwa wale watu ambao wameapa kumtii yeye. Lakini mfalme wa Babeli atawakumbusha juu ya uovu wao na kuwachukua mateka.
Mais cela paraîtra à leurs yeux un sort mensonger, on leur a fait serments sur serments; mais lui leur rappellera leur crime, pour qu’ils soient capturés.
24 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu enyi watu mmekumbusha uovu wenu kwa kuasi waziwazi, mkidhihirisha dhambi zenu katika yale yote mfanyayo, kwa kuwa mmefanya jambo hili, mtachukuliwa mateka.
C’Est pourquoi, ainsi parle le Seigneur Dieu, puisque vous avez réveillé le souvenir de votre crime, en dévoilant vos fautes, en montrant à nu vos péchés dans toutes vos actions, puisqu’il est fait mention de vous, vous serez capturés par la main.
25 “‘Ee mtawala kafiri na mwovu wa Israeli, ambaye siku yako imewadia, ambaye wakati wako wa adhabu umefikia kilele chake,
Et toi, impie, désigné à la mort, prince d’Israël dont le jour est venu, à l’heure où ton crime prend fin,
26 hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Vua kilemba, ondoa taji. Kwa kuwa mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa. Aliye mnyonge atakwezwa na aliyekwezwa atashushwa.
ainsi parle le Seigneur Dieu: Bas la tiare, plus de couronne! Tout à l’inverse! Que ce qui est bas s’élève, que ce qui est élevé s’abaisse!
27 Mahame! Mahame! Nitaufanya mji kuwa mahame! Hautajengwa upya mpaka aje yule ambaye ndiye mwenye haki nao; yeye ndiye nitakayempa.’
Ruine, ruine, ruine, voilà ce que j’en ferai; cela non plus n’existe plus, jusqu’à ce que vienne celui qui y a droit et à qui je le donnerai.
28 “Nawe, mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu Waamoni na matukano yao. “‘Upanga, upanga, umefutwa kwa ajili ya kuua, umesuguliwa ili kuangamiza na unametameta kama umeme wa radi!
Et toi, fils de l’homme, prophétise et dis: "Ainsi parle le Seigneur Dieu à l’égard des fils d’Ammon et de leurs outrages: Dis: Epée, épée dégainée, affilée pour la tuerie, pour briller comme l’éclair,
29 Wakati wakitoa maono ya uongo kwa ajili yako, wanapobashiri uongo kwa ajili yako, wanakuweka wewe kwenye shingo za watu wapotovu, wale walio waovu, wale ambao siku yao imewadia, wakati wa adhabu yao ya mwisho.
tandis qu’on t’adresse des prophéties vaines et des oracles de mensonge, on te pose sur le cou des cadavres des méchants dont le jour est venu, à l’heure où l’iniquité prend fin!
30 Urudishe upanga kwenye ala yake! Katika mahali ulipoumbiwa, katika nchi ya baba zako, huko nitakuhukumu.
Qu’elle rentre dans son fourreau! A l’endroit où tu fus créée, en ton pays d’extraction je te jugerai.
31 Nitamwaga ghadhabu yangu juu yako na kupuliza moto wa hasira yangu dhidi yako; nitakutia mikononi mwa watu wakatili, watu stadi katika kuangamiza.
J’Épancherai sur, toi ma colère; le feu de ma fureur, je le soufflerai sur toi et je te livrerai dans les mains de sauvages, artisans de la destruction.
32 Mtakuwa kuni za kuwashia moto, damu yenu itamwagwa katika nchi yenu, wala hamtakumbukwa tena; kwa maana Mimi Bwana nimesema.’”
Tu seras la proie du feu; ton sang coulera par tout le pays; on ne fera plus mention de toi, car moi, l’Eternel, j’ai parlé."

< Ezekieli 21 >