< Ezekieli 19 >

1 “Wewe fanya maombolezo kuhusu wakuu wa Israeli
A ty uczyń narzekanie nad książętami Izraelskimi,
2 na useme: “‘Tazama jinsi gani mama yako alivyokuwa simba jike miongoni mwa simba! Alilala katikati ya wana simba na kulisha watoto wake.
A mów: Cóż była matka twoja? Lwica między lwami leżąca, która w pośrodku lwiąt wychowywała szczenięta swoje.
3 Alimlea mmoja wa watoto wake, naye akawa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
A gdy odchowała jedno z szczeniąt swoich, stało się lwem, tak, że nauczywszy się chwytać łupu pożerał i ludzi.
4 Mataifa wakasikia habari zake, naye akanaswa katika shimo lao. Wakamwongoza kwa ndoana mpaka nchi ya Misri.
To gdy usłyszały o nim narody, w jamie ich pojmany jest, a zawiedziony w łańcuchach do ziemi Egipskiej.
5 “‘Mama yake alipongoja na kuona tumaini lake halitimiziki, nayo matarajio yake yametoweka, akamchukua mwanawe mwingine na kumfanya simba mwenye nguvu.
Co widząc lwica, że nadzieja jej, którą miała, zginęła, wziąwszy jedno z szczeniąt swoich, lwem je uczyniła;
6 Alizungukazunguka miongoni mwa simba, kwa kuwa sasa alikuwa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
Który chodząc w pośrodku lwów stał się lwem, a nauczywszy się chwytać łupu pożerał i ludzi.
7 Akabomoa ngome zao na kuiharibu miji yao. Nchi na wote waliokuwa ndani yake wakatiwa hofu kwa kunguruma kwake.
Poburzył też pałace ich, i miasta ich spustoszył, tak, iż i ziemia i pełność jej od głosu ryku jego spustoszała.
8 Kisha mataifa wakaja dhidi yake kutoka sehemu zilizomzunguka. Wakatanda nyavu zao kwa ajili yake, naye akanaswa katika shimo lao.
I zeszły się przeciwko niemu narody z okolicznych krain, i zarzucili nań sieci swoje; a tak w jamie ich pojmany jest.
9 Kwa kutumia ndoana wakamvutia kwenye tundu na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli. Wakamtia gerezani, hivyo kunguruma kwake hakukusikika tena katika milima ya Israeli.
I wsadzili go do klatki w łańcuchach, i przywiedli go do króla Babilońskiego, i wprowadzili go do więzienia ciężkiego, aby więcej nie był słyszany głos jego po górach Izraelskich.
10 “‘Mama yako alikuwa kama mzabibu katika shamba lako la mizabibu uliopandwa kando ya maji, ukiwa unazaa sana na wenye matawi mengi kwa sababu ya wingi wa maji.
Matka twoja była czasu pokoju twego jako winna macica przy wodach szczepiona; płodną i gałęzistą była dla wód obfitych.
11 Matawi yake yalikuwa na nguvu, yaliyofaa kuwa fimbo ya enzi ya mtawala. Ulikuwa mrefu kupita miti mingine katikati ya matawi manene; ulionekana kwa urahisi kwa ajili ya urefu wake na wingi wa matawi yake.
I miała rózgi mocne na sceptry panujących, a wywyższył się wzrost jej między gęstemi gałęziami, tak, że była okazała dla wysokości swojej, i dla mnóstwa latorośli swoich.
12 Lakini ulingʼolewa kwa hasira kali na kutupwa chini. Upepo wa mashariki uliufanya usinyae, matunda yake yakapukutika, matawi yake yenye nguvu yakanyauka na moto ukayateketeza.
Ale w rozgniewaniu wyrwana będąc, na ziemię porzucona jest, a wiatr wschodni ususzył owoc jej; obłamane są i poschły rózgi mocy jej, ogień pożarł je.
13 Sasa umepandwa jangwani katika nchi kame na ya kiu.
A teraz wszczepiona jest na puszczy w ziemi suchej i pragnącej.
14 Moto ulienea kuanzia katika mmojawapo ya matawi yake makubwa na kuteketeza matunda yake. Hakuna tawi lenye nguvu lililobaki juu yake lifaalo kuwa fimbo ya enzi ya mtawala.’ Hili ndilo ombolezo, na litumike kama ombolezo.”
Nadto wyszedł ogień z rózgi latorośli jej, a pożarł owoc jej, tak, że niemasz na niej rózgi mocnej dla sceptru panującego. Toć jest narzekanie, i będzie narzekaniem.

< Ezekieli 19 >