< Ezekieli 19 >

1 “Wewe fanya maombolezo kuhusu wakuu wa Israeli
And thou, sone of man, take weiling on the princes of Israel;
2 na useme: “‘Tazama jinsi gani mama yako alivyokuwa simba jike miongoni mwa simba! Alilala katikati ya wana simba na kulisha watoto wake.
and thou schalt seie, Whi thi modir, a lionesse, lai among liouns? In the myddis of litle liouns sche nurschide hir whelpis,
3 Alimlea mmoja wa watoto wake, naye akawa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
and ledde out oon of hir litle liouns; he was maad a lioun, and he lernyde to take prei, and to ete men.
4 Mataifa wakasikia habari zake, naye akanaswa katika shimo lao. Wakamwongoza kwa ndoana mpaka nchi ya Misri.
And hethene men herden of hym, and token hym not withouten her woundis; and thei brouyten hym in chaynes in to the lond of Egipt.
5 “‘Mama yake alipongoja na kuona tumaini lake halitimiziki, nayo matarajio yake yametoweka, akamchukua mwanawe mwingine na kumfanya simba mwenye nguvu.
Which modir whanne sche hadde seyn, that sche was sijk, and the abiding of hym perischide, took oon of her litle liouns, and made hym a lioun.
6 Alizungukazunguka miongoni mwa simba, kwa kuwa sasa alikuwa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
Which yede among liouns, and was maad a lioun;
7 Akabomoa ngome zao na kuiharibu miji yao. Nchi na wote waliokuwa ndani yake wakatiwa hofu kwa kunguruma kwake.
and lernede to take prey, and to deuoure men. He lernyde to make widewis, and to brynge the citees of men in to desert; and the lond and the fulnesse therof was maad desolat, of the vois of his roryng.
8 Kisha mataifa wakaja dhidi yake kutoka sehemu zilizomzunguka. Wakatanda nyavu zao kwa ajili yake, naye akanaswa katika shimo lao.
And hethene men camen togidere ayens hym on ech side fro prouynces, and spredden on hym her net; he was takun in the woundis of tho hethene men.
9 Kwa kutumia ndoana wakamvutia kwenye tundu na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli. Wakamtia gerezani, hivyo kunguruma kwake hakukusikika tena katika milima ya Israeli.
And thei senten hym in to a caue in chaines, and brouyten hym to the kyng of Babiloyne; and thei senten hym in to prisoun, that his vois were no more herd on the hillis of Israel.
10 “‘Mama yako alikuwa kama mzabibu katika shamba lako la mizabibu uliopandwa kando ya maji, ukiwa unazaa sana na wenye matawi mengi kwa sababu ya wingi wa maji.
Thi modir as a vyner in thi blood was plauntid on watre; the fruitis therof and the boowis therof encreessiden of many watris.
11 Matawi yake yalikuwa na nguvu, yaliyofaa kuwa fimbo ya enzi ya mtawala. Ulikuwa mrefu kupita miti mingine katikati ya matawi manene; ulionekana kwa urahisi kwa ajili ya urefu wake na wingi wa matawi yake.
And sadde yerdis weren maad to it in to septris of lordis, and the stature therof was enhaunsid among boowis; and it siy his hiynesse in the multitude of hise siouns.
12 Lakini ulingʼolewa kwa hasira kali na kutupwa chini. Upepo wa mashariki uliufanya usinyae, matunda yake yakapukutika, matawi yake yenye nguvu yakanyauka na moto ukayateketeza.
And it was drawun out in wraththe, and was cast forth in to erthe; and a brennynge wynd dryede the fruyt therof, and the yerdis of strengthe therof welewiden, and weren maad drie, and fier eet it.
13 Sasa umepandwa jangwani katika nchi kame na ya kiu.
And now it is plauntid ouer in desert, in a lond with out weie, and thristi.
14 Moto ulienea kuanzia katika mmojawapo ya matawi yake makubwa na kuteketeza matunda yake. Hakuna tawi lenye nguvu lililobaki juu yake lifaalo kuwa fimbo ya enzi ya mtawala.’ Hili ndilo ombolezo, na litumike kama ombolezo.”
And fier yede out of the yerde of the braunchis therof, that eet the fruyt therof. And a stronge yerde, the ceptre of lordis, was not in it. It is weilyng, and it schal be in to weilyng.

< Ezekieli 19 >