< Ezekieli 19 >

1 “Wewe fanya maombolezo kuhusu wakuu wa Israeli
Moreover take thou up a lamentation for the princes of Israel,
2 na useme: “‘Tazama jinsi gani mama yako alivyokuwa simba jike miongoni mwa simba! Alilala katikati ya wana simba na kulisha watoto wake.
And say, What [is] thy mother: A lioness: she lay down among lions, she nourished her whelps among young lions.
3 Alimlea mmoja wa watoto wake, naye akawa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
And she brought up one of her whelps: it became a young lion, and it learned to catch the prey; it devoured men.
4 Mataifa wakasikia habari zake, naye akanaswa katika shimo lao. Wakamwongoza kwa ndoana mpaka nchi ya Misri.
The nations also heard of him; he was taken in their pit, and they brought him with chains to the land of Egypt.
5 “‘Mama yake alipongoja na kuona tumaini lake halitimiziki, nayo matarajio yake yametoweka, akamchukua mwanawe mwingine na kumfanya simba mwenye nguvu.
Now when she saw that she had waited, [and] her hope was lost, then she took another of her whelps, [and] made him a young lion.
6 Alizungukazunguka miongoni mwa simba, kwa kuwa sasa alikuwa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
And he went up and down among the lions, he became a young lion, and learned to catch the prey, [and] devoured men.
7 Akabomoa ngome zao na kuiharibu miji yao. Nchi na wote waliokuwa ndani yake wakatiwa hofu kwa kunguruma kwake.
And he knew their desolate palaces, and he laid waste their cities; and the land was desolate, and the fullness of it, by the noise of his roaring.
8 Kisha mataifa wakaja dhidi yake kutoka sehemu zilizomzunguka. Wakatanda nyavu zao kwa ajili yake, naye akanaswa katika shimo lao.
Then the nations set against him on every side from the provinces, and spread their net over him: he was taken in their pit.
9 Kwa kutumia ndoana wakamvutia kwenye tundu na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli. Wakamtia gerezani, hivyo kunguruma kwake hakukusikika tena katika milima ya Israeli.
And they put him in custody in chains, and brought him to the king of Babylon: they brought him into holds, that his voice should no more be heard upon the mountains of Israel.
10 “‘Mama yako alikuwa kama mzabibu katika shamba lako la mizabibu uliopandwa kando ya maji, ukiwa unazaa sana na wenye matawi mengi kwa sababu ya wingi wa maji.
Thy mother [is] like a vine in thy blood, planted by the waters: she was fruitful and full of branches by reason of many waters.
11 Matawi yake yalikuwa na nguvu, yaliyofaa kuwa fimbo ya enzi ya mtawala. Ulikuwa mrefu kupita miti mingine katikati ya matawi manene; ulionekana kwa urahisi kwa ajili ya urefu wake na wingi wa matawi yake.
And she had strong rods for the scepters of them that bore rule, and her stature was exalted among the thick branches, and she appeared in her hight with the multitude of her branches.
12 Lakini ulingʼolewa kwa hasira kali na kutupwa chini. Upepo wa mashariki uliufanya usinyae, matunda yake yakapukutika, matawi yake yenye nguvu yakanyauka na moto ukayateketeza.
But she was plucked up in fury, she was cast down to the ground, and the east wind dried up her fruit: her strong rods were broken and withered; the fire consumed them.
13 Sasa umepandwa jangwani katika nchi kame na ya kiu.
And now she [is] planted in the wilderness, in a dry and thirsty ground.
14 Moto ulienea kuanzia katika mmojawapo ya matawi yake makubwa na kuteketeza matunda yake. Hakuna tawi lenye nguvu lililobaki juu yake lifaalo kuwa fimbo ya enzi ya mtawala.’ Hili ndilo ombolezo, na litumike kama ombolezo.”
And fire hath gone out of a rod of her branches, [which] hath devoured her fruit, so that she hath no strong rod [to be] a scepter to rule. This [is] a lamentation, and shall be for a lamentation.

< Ezekieli 19 >