< Ezekieli 19 >
1 “Wewe fanya maombolezo kuhusu wakuu wa Israeli
“Now you, take up a lamentation against the leaders of Israel
2 na useme: “‘Tazama jinsi gani mama yako alivyokuwa simba jike miongoni mwa simba! Alilala katikati ya wana simba na kulisha watoto wake.
and say, 'Who was your mother? A lioness, she lived with a lion's son; in the midst of young lions, she nurtured her cubs.
3 Alimlea mmoja wa watoto wake, naye akawa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
She is the one who raised up one of her cubs to become a young lion, a lion who learned to tear apart his victims, and then he devoured men.
4 Mataifa wakasikia habari zake, naye akanaswa katika shimo lao. Wakamwongoza kwa ndoana mpaka nchi ya Misri.
Then the nations heard about him. He was caught in their trap, and they brought him with hooks to the land of Egypt.
5 “‘Mama yake alipongoja na kuona tumaini lake halitimiziki, nayo matarajio yake yametoweka, akamchukua mwanawe mwingine na kumfanya simba mwenye nguvu.
Then she saw that although she had waited for his return, her expectation was now gone, so she took another of her cubs and raised him to become a young lion.
6 Alizungukazunguka miongoni mwa simba, kwa kuwa sasa alikuwa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
This young lion roamed about in the midst of lions. He was a young lion and learned to tear his victims; he devoured men.
7 Akabomoa ngome zao na kuiharibu miji yao. Nchi na wote waliokuwa ndani yake wakatiwa hofu kwa kunguruma kwake.
He seized their widows and ruined their cities. The land and its fullness were abandoned because of the sound of his roaring.
8 Kisha mataifa wakaja dhidi yake kutoka sehemu zilizomzunguka. Wakatanda nyavu zao kwa ajili yake, naye akanaswa katika shimo lao.
But the nations came against him from the surrounding provinces; they spread their nets over him. He was caught in their trap.
9 Kwa kutumia ndoana wakamvutia kwenye tundu na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli. Wakamtia gerezani, hivyo kunguruma kwake hakukusikika tena katika milima ya Israeli.
With hooks they put him in a cage and then they brought him to the king of Babylon. They brought him to the strongholds so that his voice would no longer be heard on the mountains of Israel.
10 “‘Mama yako alikuwa kama mzabibu katika shamba lako la mizabibu uliopandwa kando ya maji, ukiwa unazaa sana na wenye matawi mengi kwa sababu ya wingi wa maji.
Your mother was like a vine planted in your blood beside the water. it was fruitful and full of branches because of the abundance of water.
11 Matawi yake yalikuwa na nguvu, yaliyofaa kuwa fimbo ya enzi ya mtawala. Ulikuwa mrefu kupita miti mingine katikati ya matawi manene; ulionekana kwa urahisi kwa ajili ya urefu wake na wingi wa matawi yake.
It had strong branches that were used for rulers' scepters, and its size was exalted above the branches, and its height was seen by the greatness of its foliage.
12 Lakini ulingʼolewa kwa hasira kali na kutupwa chini. Upepo wa mashariki uliufanya usinyae, matunda yake yakapukutika, matawi yake yenye nguvu yakanyauka na moto ukayateketeza.
But the vine was uprooted in fury and thrown down to the earth, and an eastern wind dried out its fruit. Its strong branches were broken off and withered and fire consumed them.
13 Sasa umepandwa jangwani katika nchi kame na ya kiu.
So now it is planted in the wilderness, in a land of drought and thirst.
14 Moto ulienea kuanzia katika mmojawapo ya matawi yake makubwa na kuteketeza matunda yake. Hakuna tawi lenye nguvu lililobaki juu yake lifaalo kuwa fimbo ya enzi ya mtawala.’ Hili ndilo ombolezo, na litumike kama ombolezo.”
For fire went out from her large branches and consumed its fruit. There is no strong branch on it, no scepter to rule.' This is a lamentation and will be sung as a lamentation.”