< Ezekieli 18 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de l'Éternel me fut encore adressée en ces termes:
2 “Je, ninyi watu mna maana gani kutumia mithali hii inayohusu nchi ya Israeli: “‘Baba wamekula zabibu zenye chachu, nayo meno ya watoto yametiwa ganzi’?
Que voulez-vous dire, vous qui répétez continuellement ce proverbe, dans le pays d'Israël, en disant: “Les pères ont mangé du raisin vert, et les dents des enfants en sont agacées?”
3 “Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hamtatumia tena mithali hii katika Israeli.
Je suis vivant! dit le Seigneur, l'Éternel, vous n'aurez plus lieu de répéter ce proverbe en Israël.
4 Kwa kuwa kila roho ni mali yangu, kama vile ilivyo roho ya baba, vivyo hivyo roho ya mtoto ni mali yangu. Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa.
Voici, toutes les âmes sont à moi, l'âme du père comme l'âme du fils; toutes deux sont à moi; l'âme qui pèche est celle qui mourra.
5 “Mtu aweza kuwa ni mwenye haki atendaye yaliyo haki na sawa.
L'homme qui est juste, qui pratique la droiture et la justice,
6 Hakula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima wala hakuziinulia macho sanamu za nyumba ya Israeli. Hakumtia unajisi mke wa jirani yake, wala hakukutana kimwili na mwanamke wakati wa siku zake za hedhi.
Qui ne mange point sur les montagnes, qui ne lève pas les yeux vers les idoles de la maison d'Israël, qui ne déshonore pas la femme de son prochain, ni ne s'approche d'une femme pendant sa souillure;
7 Hamwonei mtu yeyote, bali hurudisha kilichowekwa rehani kwake. Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake na huwapa nguo walio uchi.
L'homme qui ne fait de tort à personne, qui rend au débiteur son gage, qui ne commet point de rapine, qui donne de son pain à l'affamé, et couvre d'un vêtement celui qui est nu,
8 Hakopeshi kwa riba wala hajipatii faida ya ziada. Huuzuia mkono wake usifanye mabaya, naye huhukumu kwa haki kati ya mtu na mtu.
Qui ne prête point à usure, qui ne retient pas au-delà de ce qui lui est dû, qui détourne sa main de l'iniquité, qui rend son jugement selon la vérité entre un homme et un autre,
9 Huzifuata amri zangu na kuzishika sheria zangu kwa uaminifu. Huyo mtu ni mwenye haki; hakika ataishi, asema Bwana Mwenyezi.
Qui marche selon mes statuts et observe mes ordonnances, en se conduisant avec droiture, - cet homme est juste, et certainement il vivra, dit le Seigneur, l'Éternel.
10 “Aweza kuwa ana mwana jeuri, amwagaye damu au atendaye mojawapo ya mambo haya
Mais s'il a donné le jour à un fils violent, qui répande le sang, et ne fasse à son frère que l'une de ces choses et non pas les autres;
11 (ingawa baba yake hakufanya mojawapo ya haya): “Hula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima. Humtia unajisi mke wa jirani yake.
Qu'il mange sur les montagnes, qu'il déshonore la femme de son prochain,
12 Huwaonea maskini na wahitaji. Hunyangʼanyana. Harudishi kile kilichowekwa rehani kwake. Huziinulia sanamu macho. Hufanya mambo ya machukizo.
Qu'il fasse tort à l'affligé et au pauvre, qu'il commette des rapines et ne rende point le gage, qu'il lève les yeux vers les idoles et commette des abominations,
13 Hukopesha kwa riba na kutafuta faida ya ziada. Je, mtu wa namna hii ataishi? Hapana, hataishi! Kwa sababu amefanya mambo haya yote ya machukizo, hakika atauawa na damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.
Qu'il prête à usure, qu'il retienne plus qu'il ne lui est dû, - ce fils-là vivrait-il? Il ne vivra pas! Parce qu'il a commis toutes ces abominations, certainement il mourra, et son sang sera sur lui.
14 “Lakini yawezekana mwana huyo ana mwana aonaye dhambi hizi zote anazofanya baba yake, naye ingawa anaziona, yeye hafanyi mabaya kama haya:
Mais voici, si ce dernier à son tour a donné le jour à un fils qui voie tous les péchés qu'a commis son père, et qui prenne soin de ne rien faire de semblable;
15 “Hakula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima, wala hainulii macho sanamu za nyumba ya Israeli. Hakumtia unajisi mke wa jirani yake.
Qu'il ne mange point sur les montagnes, qu'il ne lève point les yeux vers les idoles de la maison d'Israël, qu'il ne déshonore pas la femme de son prochain,
16 Hakumwonea mtu yeyote wala hakutaka rehani kwa ajili ya mkopo. Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake na huwapa nguo walio uchi.
Qu'il ne fasse tort à personne, qu'il ne retienne point le gage et ne commette point de rapine, qu'il donne de son pain à l'affamé, et couvre d'un vêtement celui qui est nu;
17 Huuzuia mkono wake usitende dhambi, hakopeshi kwa riba wala hajipatii faida ya ziada. Huzishika amri zangu na kuzifuata sheria zangu. Hatakufa kwa ajili ya dhambi za baba yake; hakika ataishi.
Qu'il détourne sa main de l'iniquité, qu'il ne retienne ni usure ni bénéfice, qu'il observe mes ordonnances et marche selon mes statuts, - cet homme ne mourra point pour l'iniquité de son père; certainement il vivra.
18 Lakini baba yake atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe, kwa sababu alitoza bei isiyo halali kwa nguvu, akamnyangʼanya ndugu yake na kufanya yaliyo mabaya miongoni mwa watu wake.
Mais c'est son père, qui a usé de violences et commis des rapines envers son frère, et fait ce qui n'est pas bien, au milieu de son peuple, voici, c'est lui qui mourra pour son iniquité.
19 “Lakini mnauliza, ‘Kwa nini mwana asiadhibiwe kwa uovu wa baba yake?’ Kwa vile mwana ametenda yaliyo haki na sawa na amekuwa mwangalifu kuzishika amri zangu zote, hakika ataishi.
Et vous dites: “Pourquoi le fils ne porte-t-il pas l'iniquité de son père? “C'est que le fils a agi selon la droiture et la justice, c'est qu'il a gardé tous mes statuts et les a mis en pratique; certainement il vivra.
20 Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa. Mwana hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya baba yake, wala baba hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya mwanawe. Haki ya mtu mwenye haki itahesabiwa juu yake na uovu wa mtu mwovu utalipizwa juu yake.
L'âme qui pèche est celle qui mourra. Le fils ne portera point l'inquité du père, et le père ne portera point l'iniquité du fils; la justice du juste sera sur lui, et la méchanceté du méchant sera sur lui.
21 “Lakini mtu mwovu akiacha dhambi zake zote alizozitenda na kushika amri zangu zote na kufanya lililo haki na sawa, hakika ataishi, hatakufa.
Si le méchant se détourne de tous les péchés qu'il a commis, s'il garde tous mes statuts, et s'il agit selon la droiture et la justice, certainement il vivra et ne mourra point.
22 Hakuna kosa lolote alilotenda litakalokumbukwa juu yake. Kwa ajili ya mambo ya haki aliyoyatenda, ataishi.
On ne se souviendra contre lui d'aucune de toutes les transgressions qu'il aura commises; il vivra à cause de la justice qu'il aura pratiquée.
23 Je, mimi ninafurahia kifo cha mtu mwovu? Asema Bwana Mwenyezi. Je, si mimi ninafurahi wanapogeuka kutoka njia zao mbaya na kuishi?
Prendrais-je plaisir en aucune manière à la mort du méchant? dit le Seigneur, l'Éternel; n'est-ce pas plutôt à ce qu'il se détourne de ses voies et qu'il vive?
24 “Lakini kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi na kufanya mambo ya machukizo ambayo mtu mwovu hufanya, Je, ataishi? Hakuna hata mojawapo ya matendo ya haki aliyotenda litakalokumbukwa. Kwa sababu ya kukosa uaminifu kwake anayo hatia na kwa sababu ya dhambi alizozitenda, atakufa.
Mais si le juste se détourne de sa justice, qu'il commette l'iniquité, en suivant toutes les abominations que le méchant a accoutumé de commettre, vivrait-il? On ne se souviendra plus d'aucun des actes de justice qu'il aura accomplis, à cause de l'infidélité dont il s'est rendu coupable, et du péché qu'il a commis; c'est à cause de cela qu'il mourra.
25 “Lakini mnasema, ‘Njia ya Bwana si ya haki.’ Sikia, ee nyumba ya Israeli: Njia yangu siyo iliyo ya haki? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki?
Et vous dites: “La voie du Seigneur n'est pas bien réglée. “Écoutez maintenant, maison d'Israël: Est-ce ma voie qui n'est pas bien réglée? Ne sont-ce pas plutôt vos voies qui ne sont pas bien réglées?
26 Kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi, atakufa kwa ajili ya dhambi yake, kwa sababu ya dhambi alizotenda, atakufa.
Si le juste se détourne de sa justice, qu'il commette l'iniquité, que pour cela il meure, c'est à cause de l'iniquité qu'il a commise qu'il meurt.
27 Lakini mtu mwovu akigeuka kutoka maovu aliyoyatenda na kufanya yaliyo haki na sawa, ataokoa maisha yake.
Et si le méchant se détourne de la méchanceté qu'il a commise, et qu'il pratique la droiture et la justice, il fera vivre son âme.
28 Kwa kuwa anayafikiria na kugeuka kutoka makosa yake yote aliyoyatenda na kuyaacha, hakika ataishi, hatakufa.
S'il ouvre les yeux, et se détourne de toutes les transgressions qu'il a commises, certainement il vivra et ne mourra point.
29 Lakini nyumba ya Israeli inasema, ‘Njia za Bwana si haki.’ Je, njia zangu si za haki, ee nyumba ya Israeli? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki?”
Cependant la maison d'Israël dit: “La voie du Seigneur n'est pas bien réglée. “Sont-ce mes voies, ô maison d'Israël, qui ne sont pas bien réglées? Ne sont-ce pas plutôt vos voies qui ne sont pas bien réglées?
30 “Kwa hiyo, ee nyumba ya Israeli, nitawahukumu, kila mmoja sawasawa na njia zake, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni! Geukeni kutoka makosa yenu yote, ndipo dhambi haitakuwa anguko lenu.
C'est pourquoi je vous jugerai chacun selon ses voies, ô maison d'Israël, dit le Seigneur, l'Éternel. Convertissez-vous, et détournez-vous de toutes vos transgressions, afin que l'iniquité ne devienne point pour vous une cause de ruine.
31 Tupilieni mbali makosa yenu yote mliyoyatenda, nanyi mpate moyo mpya na roho mpya. Kwa nini mfe, ee nyumba ya Israeli?
Rejetez loin de vous toutes les transgressions dont vous vous êtes rendus coupables, et faites-vous un cœur nouveau et un esprit nouveau; car pourquoi mourriez-vous, ô maison d'Israël?
32 Kwa maana sifurahii kifo cha mtu awaye yote afaye katika uovu, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni basi, mkaishi!
En effet, je ne prends point plaisir à la mort de celui qui meurt, dit le Seigneur l'Éternel; convertissez-vous et vivez!