< Ezekieli 18 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
Et la parole du Seigneur me vint, disant:
2 “Je, ninyi watu mna maana gani kutumia mithali hii inayohusu nchi ya Israeli: “‘Baba wamekula zabibu zenye chachu, nayo meno ya watoto yametiwa ganzi’?
Fils de l'homme, d'où vient cette parabole qui se dit parmi les enfants d'Israël: Les pères ont mangé du verjus, et les dents des enfants en ont été agacées?
3 “Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hamtatumia tena mithali hii katika Israeli.
Par ma vie, dit le Seigneur, on ne répètera plus cette parabole en Israël.
4 Kwa kuwa kila roho ni mali yangu, kama vile ilivyo roho ya baba, vivyo hivyo roho ya mtoto ni mali yangu. Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa.
Car toutes les âmes sont à moi; les âmes des fils sont à moi, comme l'âme du père. L'âme qui pèche, voilà celle qui mourra.
5 “Mtu aweza kuwa ni mwenye haki atendaye yaliyo haki na sawa.
L'homme qui sera juste, qui observera les jugements et l'équité,
6 Hakula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima wala hakuziinulia macho sanamu za nyumba ya Israeli. Hakumtia unajisi mke wa jirani yake, wala hakukutana kimwili na mwanamke wakati wa siku zake za hedhi.
Ne mangera pas sur les hauts lieux; il ne lèvera pas les yeux sur les idoles de la maison d'Israël; il ne profanera point la femme de son prochain; il ne s'approchera pas de sa femme dans son impureté.
7 Hamwonei mtu yeyote, bali hurudisha kilichowekwa rehani kwake. Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake na huwapa nguo walio uchi.
Il n'opprimera pas âme qui vive; il rendra le gage du débiteur; il ne commettra aucune rapine; il donnera de son pain au pauvre, et il vêtira les nus.
8 Hakopeshi kwa riba wala hajipatii faida ya ziada. Huuzuia mkono wake usifanye mabaya, naye huhukumu kwa haki kati ya mtu na mtu.
Et il ne placera pas son argent à usure, et il ne prendra pas plus qu'il ne lui est dû, et il détournera la main de l'iniquité, et il rendra un jugement juste entre un homme et son prochain.
9 Huzifuata amri zangu na kuzishika sheria zangu kwa uaminifu. Huyo mtu ni mwenye haki; hakika ataishi, asema Bwana Mwenyezi.
Celui-là aura marché en mes commandements; il aura gardé mes ordonnances pour les mettre en pratique. Celui-là est juste, et il vivra de la vie, dit le Seigneur.
10 “Aweza kuwa ana mwana jeuri, amwagaye damu au atendaye mojawapo ya mambo haya
Et s'il a engendré un fils corrompu qui verse le sang et commette des péchés,
11 (ingawa baba yake hakufanya mojawapo ya haya): “Hula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima. Humtia unajisi mke wa jirani yake.
Celui-là n'aura pas marché dans la voie de son père; mais il aura mangé sur les hauts lieux, il aura profané la femme de son prochain;
12 Huwaonea maskini na wahitaji. Hunyangʼanyana. Harudishi kile kilichowekwa rehani kwake. Huziinulia sanamu macho. Hufanya mambo ya machukizo.
Il aura opprimé le pauvre et le mendiant; il aura pris avec violence; il n'aura pas rendu le gage; il aura arrêté ses regards sur les idoles; il aura fait l'iniquité;
13 Hukopesha kwa riba na kutafuta faida ya ziada. Je, mtu wa namna hii ataishi? Hapana, hataishi! Kwa sababu amefanya mambo haya yote ya machukizo, hakika atauawa na damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.
Il aura placé à usure; il se sera fait rendre plus qu'il ne lui était dû; celui-là ne vivra pas de la vie: pour avoir fait toutes ces iniquités, il mourra de mort, et son sang sera sur sa tête.
14 “Lakini yawezekana mwana huyo ana mwana aonaye dhambi hizi zote anazofanya baba yake, naye ingawa anaziona, yeye hafanyi mabaya kama haya:
Et si cet homme a engendré un fils qui ait vu tous les péchés commis par son père, mais qui en ait eu peur et ne les ait pas commis;
15 “Hakula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima, wala hainulii macho sanamu za nyumba ya Israeli. Hakumtia unajisi mke wa jirani yake.
Qui ne monte pas sur les hauts lieux; qui n'arrête pas ses regards sur les idoles de la maison d'Israël; qui ne profane point la femme de son prochain;
16 Hakumwonea mtu yeyote wala hakutaka rehani kwa ajili ya mkopo. Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake na huwapa nguo walio uchi.
Qui n'opprime pas âme qui vive; qui ne retienne pas de gages; qui ne commette aucune rapine; qui donne de son pain au pauvre et vêtisse les nus;
17 Huuzuia mkono wake usitende dhambi, hakopeshi kwa riba wala hajipatii faida ya ziada. Huzishika amri zangu na kuzifuata sheria zangu. Hatakufa kwa ajili ya dhambi za baba yake; hakika ataishi.
Qui détourne sa main de l'iniquité, qui ne reçoive ni usure ni plus qu'il ne lui est dû; qui fasse justice; qui marche en mes commandements: il ne mourra pas à cause des iniquités de son père, il vivra de la vie.
18 Lakini baba yake atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe, kwa sababu alitoza bei isiyo halali kwa nguvu, akamnyangʼanya ndugu yake na kufanya yaliyo mabaya miongoni mwa watu wake.
Et son père, pour avoir opprimé, pour avoir pris avec violence, pour avoir fait le mal devant mon peuple, mourra dans son iniquité.
19 “Lakini mnauliza, ‘Kwa nini mwana asiadhibiwe kwa uovu wa baba yake?’ Kwa vile mwana ametenda yaliyo haki na sawa na amekuwa mwangalifu kuzishika amri zangu zote, hakika ataishi.
Et vous direz: Pourquoi le fils n'a-t-il pas porté la peine de l'iniquité du père? Parce que le fils a fait justice et miséricorde, qu'il a gardé mes ordonnances et les a mises en pratique: il vivra de la vie.
20 Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa. Mwana hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya baba yake, wala baba hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya mwanawe. Haki ya mtu mwenye haki itahesabiwa juu yake na uovu wa mtu mwovu utalipizwa juu yake.
Et l'âme qui pèche mourra; le fils ne portera pas la peine de l'iniquité du père; le père ne portera pas la peine de l'iniquité du fils. La justice du juste sera sur lui, et l'iniquité de l'injuste sera sur lui.
21 “Lakini mtu mwovu akiacha dhambi zake zote alizozitenda na kushika amri zangu zote na kufanya lililo haki na sawa, hakika ataishi, hatakufa.
Et le pécheur, s'il revient de ses dérèglements, garde tous mes commandements, s'il fait justice et miséricorde, vivra de la vie et ne mourra point.
22 Hakuna kosa lolote alilotenda litakalokumbukwa juu yake. Kwa ajili ya mambo ya haki aliyoyatenda, ataishi.
Toutes ses iniquités seront oubliées; il vivra dans son équité et à cause d'elle.
23 Je, mimi ninafurahia kifo cha mtu mwovu? Asema Bwana Mwenyezi. Je, si mimi ninafurahi wanapogeuka kutoka njia zao mbaya na kuishi?
Est-ce que je veux la mort du pécheur? dit le Seigneur. Est-ce que je ne veux pas plutôt qu'il se détourne de sa voie mauvaise et qu'il vive?
24 “Lakini kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi na kufanya mambo ya machukizo ambayo mtu mwovu hufanya, Je, ataishi? Hakuna hata mojawapo ya matendo ya haki aliyotenda litakalokumbukwa. Kwa sababu ya kukosa uaminifu kwake anayo hatia na kwa sababu ya dhambi alizozitenda, atakufa.
Si le juste se détourne de sa justice et tombe dans tous les péchés que fait l'homme inique, toutes les œuvres de sa justice seront oubliées; il mourra dans sa chute et dans ses péchés.
25 “Lakini mnasema, ‘Njia ya Bwana si ya haki.’ Sikia, ee nyumba ya Israeli: Njia yangu siyo iliyo ya haki? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki?
Et vous dites: La voie du Seigneur n'est pas droite! Écoutez donc, ô vous tous, maison d'Israël: Est-ce ma voie qui n'est pas droite? Est-ce votre voie qui est droite!
26 Kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi, atakufa kwa ajili ya dhambi yake, kwa sababu ya dhambi alizotenda, atakufa.
Quand le juste se détourne de sa justice, quand il fait un péché, quand il meurt dans le péché qu'il a fait, il meurt en ce péché.
27 Lakini mtu mwovu akigeuka kutoka maovu aliyoyatenda na kufanya yaliyo haki na sawa, ataokoa maisha yake.
Et quand l'impie revient de son impiété, et qu'il fait jugement et justice, celui-là sauve son âme.
28 Kwa kuwa anayafikiria na kugeuka kutoka makosa yake yote aliyoyatenda na kuyaacha, hakika ataishi, hatakufa.
Il s'est converti de toutes les impiétés qu'il avait faites; il vivra de la vie et ne mourra point.
29 Lakini nyumba ya Israeli inasema, ‘Njia za Bwana si haki.’ Je, njia zangu si za haki, ee nyumba ya Israeli? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki?”
Et en la maison d'Israël ils disent: La voie du Seigneur n'est pas droite! Est-ce ma voie qui n'est pas droite, maison d'Israël? N'est-ce pas votre voie qui n'est pas droite?
30 “Kwa hiyo, ee nyumba ya Israeli, nitawahukumu, kila mmoja sawasawa na njia zake, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni! Geukeni kutoka makosa yenu yote, ndipo dhambi haitakuwa anguko lenu.
Je jugerai chacun de vous selon sa voie, maison d'Israël, dit le Seigneur; convertissez-vous, revenez de toutes vos impiétés, et vous ne serez point punis pour cause d'iniquités.
31 Tupilieni mbali makosa yenu yote mliyoyatenda, nanyi mpate moyo mpya na roho mpya. Kwa nini mfe, ee nyumba ya Israeli?
Repoussez loin de vous toutes les impiétés que vous avez commises contre moi; faites-vous un nouveau cœur, un esprit nouveau; et pourquoi péririez- vous, maison d'Israël?
32 Kwa maana sifurahii kifo cha mtu awaye yote afaye katika uovu, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni basi, mkaishi!
Ce n'est pas moi qui veux la mort de celui qui périt, dit le Seigneur.

< Ezekieli 18 >