< Ezekieli 18 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de Yahvé me fut adressée de nouveau, en disant:
2 “Je, ninyi watu mna maana gani kutumia mithali hii inayohusu nchi ya Israeli: “‘Baba wamekula zabibu zenye chachu, nayo meno ya watoto yametiwa ganzi’?
« Que veux-tu dire par là, que tu utilises ce proverbe concernant le pays d'Israël, en disant, Les pères ont mangé des raisins aigres, et les enfants ont les dents serrées »?
3 “Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hamtatumia tena mithali hii katika Israeli.
« Je suis vivant », dit le Seigneur Yahvé, « vous n'utiliserez plus ce proverbe en Israël.
4 Kwa kuwa kila roho ni mali yangu, kama vile ilivyo roho ya baba, vivyo hivyo roho ya mtoto ni mali yangu. Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa.
Voici, toutes les âmes sont à moi; comme l'âme du père, ainsi l'âme du fils est à moi. L'âme qui pèche, c'est elle qui mourra.
5 “Mtu aweza kuwa ni mwenye haki atendaye yaliyo haki na sawa.
« Mais si un homme est juste, et fait ce qui est légal et juste,
6 Hakula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima wala hakuziinulia macho sanamu za nyumba ya Israeli. Hakumtia unajisi mke wa jirani yake, wala hakukutana kimwili na mwanamke wakati wa siku zake za hedhi.
et n'a pas mangé sur les montagnes, n'a pas levé les yeux vers les idoles de la maison d'Israël, n'a pas souillé la femme de son voisin, ne s'est pas approché d'une femme dans son impureté,
7 Hamwonei mtu yeyote, bali hurudisha kilichowekwa rehani kwake. Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake na huwapa nguo walio uchi.
et n'a fait de tort à personne, mais a rendu au débiteur son gage, n'a rien pris par vol, a donné son pain aux affamés, et a couvert le nu d'un vêtement;
8 Hakopeshi kwa riba wala hajipatii faida ya ziada. Huuzuia mkono wake usifanye mabaya, naye huhukumu kwa haki kati ya mtu na mtu.
celui qui ne leur a pas prêté avec intérêt, n'a pas pris d'augmentation de leur part, qui a retiré sa main de l'iniquité, a exécuté la vraie justice entre l'homme et l'homme,
9 Huzifuata amri zangu na kuzishika sheria zangu kwa uaminifu. Huyo mtu ni mwenye haki; hakika ataishi, asema Bwana Mwenyezi.
a marché dans mes statuts, et a gardé mes ordonnances, pour traiter véritablement; il est juste, il vivra », dit le Seigneur Yahvé.
10 “Aweza kuwa ana mwana jeuri, amwagaye damu au atendaye mojawapo ya mambo haya
« S'il engendre un fils qui est un voleur et qui verse le sang, et qui fait l'une de ces choses,
11 (ingawa baba yake hakufanya mojawapo ya haya): “Hula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima. Humtia unajisi mke wa jirani yake.
ou qui ne fait aucune de ces choses. mais a mangé dans les sanctuaires de la montagne et a souillé la femme de son voisin,
12 Huwaonea maskini na wahitaji. Hunyangʼanyana. Harudishi kile kilichowekwa rehani kwake. Huziinulia sanamu macho. Hufanya mambo ya machukizo.
a fait du tort aux pauvres et aux nécessiteux, a pris par vol, n'a pas rétabli l'engagement, et a levé les yeux vers les idoles, a commis une abomination,
13 Hukopesha kwa riba na kutafuta faida ya ziada. Je, mtu wa namna hii ataishi? Hapana, hataishi! Kwa sababu amefanya mambo haya yote ya machukizo, hakika atauawa na damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.
a prêté avec intérêt, et a pris l'argent des pauvres, vivra-t-il alors? Il ne vivra pas. Il a commis toutes ces abominations. Il mourra sûrement. Son sang sera sur lui.
14 “Lakini yawezekana mwana huyo ana mwana aonaye dhambi hizi zote anazofanya baba yake, naye ingawa anaziona, yeye hafanyi mabaya kama haya:
« Or, voici, s'il engendre un fils qui voit tous les péchés de son père, qu'il a commis, et qui a peur, il ne fait pas de même,
15 “Hakula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima, wala hainulii macho sanamu za nyumba ya Israeli. Hakumtia unajisi mke wa jirani yake.
qui n'a pas mangé sur les montagnes, n'a pas levé les yeux vers les idoles de la maison d'Israël, n'a pas souillé la femme de son voisin,
16 Hakumwonea mtu yeyote wala hakutaka rehani kwa ajili ya mkopo. Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake na huwapa nguo walio uchi.
Le na fait de tort à personne, n'a pas pris de gage, n'a pas été prise en flagrant délit de vol, mais a donné son pain aux affamés, et a couvert le nu d'un vêtement;
17 Huuzuia mkono wake usitende dhambi, hakopeshi kwa riba wala hajipatii faida ya ziada. Huzishika amri zangu na kuzifuata sheria zangu. Hatakufa kwa ajili ya dhambi za baba yake; hakika ataishi.
qui a retiré sa main des pauvres, qui n'a pas reçu d'intérêt ou d'augmentation, a exécuté mes ordonnances, a marché dans mes statuts; il ne mourra pas pour l'iniquité de son père. Il vivra certainement.
18 Lakini baba yake atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe, kwa sababu alitoza bei isiyo halali kwa nguvu, akamnyangʼanya ndugu yake na kufanya yaliyo mabaya miongoni mwa watu wake.
Quant à son père, parce qu'il a opprimé cruellement, dépouillé son frère, et fait ce qui n'est pas bien au milieu de son peuple, voici, il mourra dans son iniquité.
19 “Lakini mnauliza, ‘Kwa nini mwana asiadhibiwe kwa uovu wa baba yake?’ Kwa vile mwana ametenda yaliyo haki na sawa na amekuwa mwangalifu kuzishika amri zangu zote, hakika ataishi.
Et vous dites: « Pourquoi le fils ne porte-t-il pas l'iniquité du père? Quand le fils aura fait ce qui est licite et juste, quand il aura observé toutes mes lois et les aura mises en pratique, il vivra.
20 Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa. Mwana hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya baba yake, wala baba hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya mwanawe. Haki ya mtu mwenye haki itahesabiwa juu yake na uovu wa mtu mwovu utalipizwa juu yake.
L'âme qui pèche, elle, mourra. Le fils ne portera pas l'iniquité du père, et le père ne portera pas l'iniquité du fils. La justice des justes sera sur lui, et la méchanceté des méchants sera sur lui.
21 “Lakini mtu mwovu akiacha dhambi zake zote alizozitenda na kushika amri zangu zote na kufanya lililo haki na sawa, hakika ataishi, hatakufa.
« Mais si le méchant se détourne de tous les péchés qu'il a commis, s'il observe toutes mes lois, s'il fait ce qui est licite et juste, il vivra. Il ne mourra pas.
22 Hakuna kosa lolote alilotenda litakalokumbukwa juu yake. Kwa ajili ya mambo ya haki aliyoyatenda, ataishi.
On ne se souviendra pas contre lui des fautes qu'il a commises. Il vivra selon la justice qu'il a pratiquée.
23 Je, mimi ninafurahia kifo cha mtu mwovu? Asema Bwana Mwenyezi. Je, si mimi ninafurahi wanapogeuka kutoka njia zao mbaya na kuishi?
Est-ce que je prends plaisir à la mort du méchant, dit le Seigneur Yahvé, et ne préfère-t-il pas qu'il revienne de sa voie et qu'il vive?
24 “Lakini kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi na kufanya mambo ya machukizo ambayo mtu mwovu hufanya, Je, ataishi? Hakuna hata mojawapo ya matendo ya haki aliyotenda litakalokumbukwa. Kwa sababu ya kukosa uaminifu kwake anayo hatia na kwa sababu ya dhambi alizozitenda, atakufa.
« Mais quand le juste se détourne de sa justice, qu'il commet l'iniquité et qu'il se conforme à toutes les abominations que fait le méchant, doit-il vivre? On ne se souviendra d'aucune des actions justes qu'il a accomplies. Il mourra de la faute qu'il a commise et du péché qu'il a commis.
25 “Lakini mnasema, ‘Njia ya Bwana si ya haki.’ Sikia, ee nyumba ya Israeli: Njia yangu siyo iliyo ya haki? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki?
« Et vous dites: 'La voie du Seigneur n'est pas égale'. Écoutez maintenant, maison d'Israël: Ma voie n'est-elle pas égale? Vos voies ne sont-elles pas inégales?
26 Kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi, atakufa kwa ajili ya dhambi yake, kwa sababu ya dhambi alizotenda, atakufa.
Si le juste se détourne de sa justice, commet l'iniquité et meurt par elle, il meurt par l'iniquité qu'il a commise.
27 Lakini mtu mwovu akigeuka kutoka maovu aliyoyatenda na kufanya yaliyo haki na sawa, ataokoa maisha yake.
De même, si le méchant se détourne de la méchanceté qu'il a commise et fait ce qui est licite et juste, il sauvera son âme en vie.
28 Kwa kuwa anayafikiria na kugeuka kutoka makosa yake yote aliyoyatenda na kuyaacha, hakika ataishi, hatakufa.
Parce qu'il réfléchit et se détourne de toutes les transgressions qu'il a commises, il vivra. Il ne mourra pas.
29 Lakini nyumba ya Israeli inasema, ‘Njia za Bwana si haki.’ Je, njia zangu si za haki, ee nyumba ya Israeli? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki?”
Mais la maison d'Israël dit: « La voie de l'Éternel n'est pas droite ». Maison d'Israël, mes voies ne sont-elles pas équitables? Tes voies ne sont-elles pas injustes?
30 “Kwa hiyo, ee nyumba ya Israeli, nitawahukumu, kila mmoja sawasawa na njia zake, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni! Geukeni kutoka makosa yenu yote, ndipo dhambi haitakuwa anguko lenu.
« C'est pourquoi je vous jugerai, maison d'Israël, chacun selon ses voies, dit le Seigneur Yahvé. « Revenez, et détournez-vous de toutes vos transgressions, afin que l'iniquité ne soit pas votre ruine.
31 Tupilieni mbali makosa yenu yote mliyoyatenda, nanyi mpate moyo mpya na roho mpya. Kwa nini mfe, ee nyumba ya Israeli?
Rejetez loin de vous toutes les transgressions que vous avez commises, et faites-vous un cœur nouveau et un esprit nouveau. Car pourquoi mourrez-vous, maison d'Israël?
32 Kwa maana sifurahii kifo cha mtu awaye yote afaye katika uovu, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni basi, mkaishi!
Car je ne prends aucun plaisir à la mort de celui qui meurt, dit le Seigneur Yahvé. « C'est pourquoi tournez-vous, et vivez!

< Ezekieli 18 >