< Ezekieli 17 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
RAB bana şöyle seslendi:
2 “Mwanadamu, tega kitendawili, ukawaambie nyumba ya Israeli fumbo.
“Ey insanoğlu, İsrail halkına bir bilmece sor, simgesel bir öykü anlat.
3 Waambie hivi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tai mkubwa mwenye mabawa yenye nguvu, yaliyojaa manyoya marefu ya rangi mbalimbali, alikuja Lebanoni. Akatua kwenye kilele cha mwerezi,
De ki, ‘Egemen RAB şöyle diyor: Kanatları uzun ve güçlü, renk renk tüylerle dolu iri bir kartal Lübnan'a geldi, bir sedir ağacının tepesine konup onu ele geçirdi.
4 akakwanyua ncha yake na kuichukua mpaka nchi ya wafanyabiashara, akaipanda huko katika mji wa wachuuzi.
Ağacın tepesindeki filizleri koparıp ticaret ülkesine götürdü, tüccarlar kentine yerleştirdi.
5 “‘Akachukua baadhi ya mbegu za nchi yako na kuziweka katika udongo wenye rutuba. Akazipanda kama mti umeao kando ya maji mengi,
“‘Ülkenin tohumundan alıp verimli toprağa ekti; onu söğüt ağacı gibi akarsuların kıyısına dikti.
6 nazo zikaota na kuwa mzabibu mfupi, unaoeneza matawi yake. Matawi yake yakamwelekea huyo tai, mizizi yake ikabaki chini ya huo mzabibu. Kwa hiyo ukawa mzabibu na kutoa matawi na vitawi vyenye majani mengi.
Tohum filizlenip yerde yayılan bodur bir asma oldu. Dalları kartala doğru yayıldı, kökleriyse aşağıya, derine indi. Böylece dal salan, filiz veren bir asma oldu.
7 “‘Lakini kulikuwa na tai mwingine mkubwa, mwenye mabawa yenye nguvu yaliyojaa manyoya. Tazama! Huu mzabibu ukatoa mizizi yake kumwelekea huyo tai kutoka mle kwenye shamba lile ulikopandwa na kutanda matawi yake kumwelekea kwa ajili ya kupata maji.
“‘Gelgelelim, kanatları güçlü, bol tüylü başka bir iri kartal da vardı. Asma bu kez dikildiği yerden köklerini bu kartala doğru çevirdi; sulasın diye dallarını ona doğru saldı.
8 Ulikuwa umepandwa katika udongo mzuri wenye maji mengi ili uweze kutoa matawi, kuzaa matunda na uweze kuwa mzabibu mzuri sana.’
Dallansın, ürün versin, görkemli bir asma olsun diye akarsuların kıyısındaki verimli toprağa dikilmişti.’
9 “Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, utastawi? Je, hautangʼolewa na kuondolewa matunda yake, ili uweze kunyauka? Majani yake mapya yanayochipua yote yatanyauka. Hautahitaji mkono wenye nguvu au watu wengi kuungʼoa na mizizi yake.
“Onlara de ki, ‘Egemen RAB şöyle diyor: Asma serpilecek mi? Kurusun diye ilk kartal kökünü söküp meyvesini koparmayacak mı? Asmanın yeni filizlenen bütün dalları kuruyacak. Kökünden söküp atmak için güçlü ele ya da büyük orduya gerek duyulmayacak.
10 Hata kama utapandwa pengine, Je, utastawi? Je, hautanyauka kabisa wakati upepo wa mashariki utakapoupiga, yaani, hautanyauka kabisa katika udongo mzuri ambamo ulikuwa umestawi vizuri?’”
Evet, asma dikilmiş, ama serpilip gelişecek mi? Doğu rüzgarı ona çarpınca büsbütün kurumayacak mı? Evet, filizlendiği yerde solup kuruyacak.’”
11 Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
RAB bana şöyle seslendi:
12 “Waambie nyumba hii ya kuasi, ‘Je, mnajua hii ina maana gani?’ Waambie: ‘Mfalme wa Babeli alikwenda Yerusalemu na kumchukua mfalme na watu maarufu, akarudi nao na kuwaleta mpaka Babeli.
“O asi halka de ki, ‘Bunların ne anlama geldiğini bilmiyor musunuz?’ Onlara de ki, ‘Babil Kralı Yeruşalim'e gitti; kralını, önderlerini tutsak alıp kendisiyle birlikte Babil'e götürdü.
13 Ndipo akamchukua mmoja wa jamaa ya mfalme na kufanya mapatano naye, akamfanya aape. Akawachukua pia viongozi wa nchi,
Sonra kralın soyundan gelen birini alıp ant içirerek onunla bir antlaşma yaptı. Ülkenin önderlerini de tutsak aldı.
14 ili kuudhoofisha ufalme huo, usiweze kuinuka tena, ila uweze kuendelea tu chini ya mapatano yake.
Öyle ki, ülke gerilesin, bir daha yükselmesin, ancak yaptığı antlaşmayı yerine getirerek yaşayabilsin.
15 Lakini mfalme aliasi dhidi yake kwa kutuma wajumbe wake kwenda Misri ili kupatiwa farasi na jeshi kubwa. Je, atashinda? Je, atafanikiwa? Je, mtu afanyaye mambo kama hayo ataokoka? Je, atavunja mapatano na bado aokoke?
Ne var ki, Yahuda Kralı, kendisine at ve çok sayıda asker vermesi için Mısır'a elçiler göndererek Babil Kralı'na başkaldırdı. Yahuda Kralı başaracak mı? Böyle şeyler yapan kurtulur mu? Yaptığı antlaşmayı bozan kurtulur mu?
16 “‘Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, atafia huko Babeli, katika nchi ya mfalme aliyemketisha katika kiti cha enzi, ambaye alidharau kiapo chake na kuvunja mapatano yake.
“‘Egemen RAB, varlığım hakkı için diyor, onu tahta oturtan kralın ülkesinde, Babil'de ölecek. Çünkü içtiği andı küçümsedi, yaptığı antlaşmayı bozdu.
17 Farao na jeshi lake kubwa, na wingi wake wa watu hawataweza kusaidia chochote katika vita, wakati watakapozungukwa na jeshi ili kukatilia mbali maisha ya watu wengi.
Babilliler birçok kişiyi yok etmek için toprak rampalar, kuşatma duvarları yaptığında, firavun güçlü ordusu ve büyük kalabalıklarla savaşta ona yardımcı olmayacak.
18 Alidharau kiapo kwa kuvunja Agano. Kwa sababu aliahidi kwa mkono wake mwenyewe na bado akafanya mambo haya yote, hataokoka.
Yaptığı antlaşmayı bozarak içtiği andı küçümsedi. Söz verdiği halde, bütün bunları yaptı. Bu yüzden kurtulmayacak.
19 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakika kama niishivyo, nitaleta juu ya kichwa chake kiapo changu, alichokidharau na Agano langu lile alilolivunja.
“‘Bu nedenle Egemen RAB şöyle diyor: Varlığım hakkı için, bana içtiği andı küçümsediği, antlaşmamı bozduğu için onu cezalandıracağım.
20 Nitautandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa katika mtego wangu. Nitamleta mpaka Babeli na kutekeleza hukumu juu yake huko kwa kuwa hakuwa mwaminifu kwangu.
Ağımı gereceğim, tuzağıma düşecek. Onu Babil'e getirecek, bana sadakatsizliğinden ötürü orada yargılayacağım.
21 Askari wake wote wanaotoroka wataanguka kwa upanga, nao watakaonusurika watatawanyika katika pande zote za dunia. Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesema.
En seçkin askerleri kılıçtan geçirilecek, sağ kalanlar dünyanın dört bucağına dağılacak. O zaman konuşanın ben RAB olduğumu anlayacaksınız.
22 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi mwenyewe nitachukua chipukizi kutoka kwenye kilele cha juu sana cha mwerezi na kukipanda, nitavunja kitawi kichanga kutoka matawi yake ya juu kabisa na kukipanda juu ya mlima mrefu ulioinuka sana.
“‘Egemen RAB şöyle diyor: Sedir ağacının tepesinden Bir filiz alıp dikeceğim. En yüksek dallarından körpe bir çubuk koparıp Yüksek, ulu bir dağın üzerine dikeceğim.
23 Katika vilele vya mlima mrefu wa Israeli nitakipanda, kitatoa matawi na kuzaa matunda na kuwa mwerezi mzuri sana. Ndege wa kila aina wataweka viota vyao ndani yake, nao watapata makazi katika kivuli cha matawi yake.
Onu İsrail'in en yüksek dağının üzerine dikeceğim. Dal budak salıp ürün verecek, Görkemli bir sedir ağacı olacak. Her çeşit kuş dallarına tüneyecek, Gölgesinde barınacak.
24 Miti yote ya kondeni itajua kuwa Mimi Bwana ninaishusha miti mirefu na kuikuza miti mifupi kuwa miti mirefu. Mimi naikausha miti mibichi na kuifanya miti mikavu istawi. “‘Mimi Bwana nimesema, nami nitatenda.’”
Bütün orman ağaçları Her yüksek ağacı bodurlaştıranın, Her bodur ağacı yükseltenin, Her yeşil ağacı kurutanın Ve kuru ağacı yeşertenin Ben RAB olduğumu anlayacaklar. Bunu ben RAB söylüyorum ve dediğimi yapacağım.’”

< Ezekieli 17 >