< Ezekieli 17 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de l’Eternel me fut adressée en ces termes:
2 “Mwanadamu, tega kitendawili, ukawaambie nyumba ya Israeli fumbo.
"Fils de l’homme, propose une énigme et imagine une parabole à l’adresse de la maison d’Israël.
3 Waambie hivi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tai mkubwa mwenye mabawa yenye nguvu, yaliyojaa manyoya marefu ya rangi mbalimbali, alikuja Lebanoni. Akatua kwenye kilele cha mwerezi,
Tu diras: Ainsi parle le Seigneur Dieu: L’Aigle géant, aux grandes ailes, aux longues pennes, au plumage épais, aux nuances variées, vint vers le Liban et enleva la cime du cèdre.
4 akakwanyua ncha yake na kuichukua mpaka nchi ya wafanyabiashara, akaipanda huko katika mji wa wachuuzi.
Il arracha l’extrémité de ses branches, l’apporta dans un pays marchand et la plaça dans une ville de commerçants.
5 “‘Akachukua baadhi ya mbegu za nchi yako na kuziweka katika udongo wenye rutuba. Akazipanda kama mti umeao kando ya maji mengi,
Il prit de la semence du pays et la déposa dans un champ de culture; l’ayant ainsi prise, il la mit près des grandes eaux, en un lieu bien arrosé.
6 nazo zikaota na kuwa mzabibu mfupi, unaoeneza matawi yake. Matawi yake yakamwelekea huyo tai, mizizi yake ikabaki chini ya huo mzabibu. Kwa hiyo ukawa mzabibu na kutoa matawi na vitawi vyenye majani mengi.
Elle poussa et devint une vigne plantureuse, de peu de hauteur, de sorte que ses rameaux se tournaient vers lui (l’aigle) et que ses racines s’étendaient sous lui; devenue une vigne, elle produisit dès branches et projeta des rameaux.
7 “‘Lakini kulikuwa na tai mwingine mkubwa, mwenye mabawa yenye nguvu yaliyojaa manyoya. Tazama! Huu mzabibu ukatoa mizizi yake kumwelekea huyo tai kutoka mle kwenye shamba lile ulikopandwa na kutanda matawi yake kumwelekea kwa ajili ya kupata maji.
Mais il y eut un autre grand aigle aux grandes ailes et au plumage abondant, et alors cette vigne inclina ses racines vers lui et projeta ses sarments de son côté, afin qu’il l’abreuvât de préférence aux plates-bandes où elle était plantée.
8 Ulikuwa umepandwa katika udongo mzuri wenye maji mengi ili uweze kutoa matawi, kuzaa matunda na uweze kuwa mzabibu mzuri sana.’
Elle était plantée dans un champ excellent près d’eaux abondantes, de façon é produire des branches, à porter des fruits et devenir une vigne splendide.
9 “Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, utastawi? Je, hautangʼolewa na kuondolewa matunda yake, ili uweze kunyauka? Majani yake mapya yanayochipua yote yatanyauka. Hautahitaji mkono wenye nguvu au watu wengi kuungʼoa na mizizi yake.
Dis: Ainsi parie le Seigneur Dieu: Prospérera-t-elle? N’Arrachera-t-il pas ses racines, ne coupera-t-il pas son fruit de sorte qu’il se dessèche; toutes les feuilles produites par elles ne seront-elles pas fanées? Et il n’aura pas besoin d’un bras puissant ni d’un peuple nombreux pour l’arracher de ses racines.
10 Hata kama utapandwa pengine, Je, utastawi? Je, hautanyauka kabisa wakati upepo wa mashariki utakapoupiga, yaani, hautanyauka kabisa katika udongo mzuri ambamo ulikuwa umestawi vizuri?’”
La voilà plantée, réussira-t-elle? Quand l’aura atteinte le vent d’est, ne se desséchera-t-elle pas? Oui, elle se desséchera, sur les plates-bandes où elle croissait!"
11 Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
La parole de l’Eternel me fut adressée en ces termes:
12 “Waambie nyumba hii ya kuasi, ‘Je, mnajua hii ina maana gani?’ Waambie: ‘Mfalme wa Babeli alikwenda Yerusalemu na kumchukua mfalme na watu maarufu, akarudi nao na kuwaleta mpaka Babeli.
"Eh bien! Dis à la maison de rébellion: Ne savez-vous pas ce que signifient ces choses? Dis: Voici qu’est venu le roi de Babel à Jérusalem; il a pris son roi et ses princes et les a amenés chez lui à Babylone.
13 Ndipo akamchukua mmoja wa jamaa ya mfalme na kufanya mapatano naye, akamfanya aape. Akawachukua pia viongozi wa nchi,
II a pris un rejeton de race royale, il a contracté une alliance avec lui, il l’a engagé par un serment, mais il a emmené les grands du pays,
14 ili kuudhoofisha ufalme huo, usiweze kuinuka tena, ila uweze kuendelea tu chini ya mapatano yake.
pour que le royaume fût abaissé et ne se relevât plus, et qu’il gardât son alliance et en assurât la durée.
15 Lakini mfalme aliasi dhidi yake kwa kutuma wajumbe wake kwenda Misri ili kupatiwa farasi na jeshi kubwa. Je, atashinda? Je, atafanikiwa? Je, mtu afanyaye mambo kama hayo ataokoka? Je, atavunja mapatano na bado aokoke?
Mais il se révolta contre lui, envoyant des messagers en Egypte pour qu’on lui fournît des chevaux et de grandes troupes. Peut-il réussir et se sauver, celui qui agit de la sorte? II romprait l’alliance et se sauverait!
16 “‘Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, atafia huko Babeli, katika nchi ya mfalme aliyemketisha katika kiti cha enzi, ambaye alidharau kiapo chake na kuvunja mapatano yake.
Je le jure par ma vie, dit le Seigneur Dieu, c’est au pays du roi qui l’a appelé au pouvoir et dont il a méprisé le serment et rompu le pacte, c’est chez lui, à Babel, qu’il périra!
17 Farao na jeshi lake kubwa, na wingi wake wa watu hawataweza kusaidia chochote katika vita, wakati watakapozungukwa na jeshi ili kukatilia mbali maisha ya watu wengi.
Et ce n’est pas avec de grandes forces et une multitude nombreuse que Pharaon agira pour lui dans la guerre, quand on élèvera des chaussées et qu’on bâtira des ouvrages, pour massacrer beaucoup de monde.
18 Alidharau kiapo kwa kuvunja Agano. Kwa sababu aliahidi kwa mkono wake mwenyewe na bado akafanya mambo haya yote, hataokoka.
Il a méprisé le serment en rompant le pacte; or il avait donné sa main, et il a fait tout cela! Il ne se sauvera pas.
19 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakika kama niishivyo, nitaleta juu ya kichwa chake kiapo changu, alichokidharau na Agano langu lile alilolivunja.
C’Est pourquoi, ainsi parle le Seigneur Dieu. Par ma vie, je le jure, mon serment qu’il a méprisé et mon pacte qu’il a rompu, je le ferai retomber sur sa tête.
20 Nitautandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa katika mtego wangu. Nitamleta mpaka Babeli na kutekeleza hukumu juu yake huko kwa kuwa hakuwa mwaminifu kwangu.
J’Étendrai sur lui mon réseau, et il sera pris dans mon filet; je l’amènerai à Babel et là je lui demanderai compte de l’infidélité qu’il a commise envers moi.
21 Askari wake wote wanaotoroka wataanguka kwa upanga, nao watakaonusurika watatawanyika katika pande zote za dunia. Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesema.
Et tous ses fugitifs, dans toutes ses troupes, tomberont sous le glaive, et les survivants se disperseront en tous sens, et vous saurez que moi, l’Eternel, j’ai parlé."
22 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi mwenyewe nitachukua chipukizi kutoka kwenye kilele cha juu sana cha mwerezi na kukipanda, nitavunja kitawi kichanga kutoka matawi yake ya juu kabisa na kukipanda juu ya mlima mrefu ulioinuka sana.
Ainsi parle le Seigneur Dieu: "Je détacherai, moi, un peu de la cime élevée du cèdre et le mettrai en terre, je trancherai un rameau tendre de l’extrémité de ses branches et je le planterai, moi, sur une montagne haute et élancée.
23 Katika vilele vya mlima mrefu wa Israeli nitakipanda, kitatoa matawi na kuzaa matunda na kuwa mwerezi mzuri sana. Ndege wa kila aina wataweka viota vyao ndani yake, nao watapata makazi katika kivuli cha matawi yake.
Sur la montagne la plus élevée d’Israël je le planterai; il portera des branches, produira des fruits et deviendra un cèdre majestueux; sous lui habiteront tous les oiseaux de tout plumage, ils habiteront à l’ombre de ses rameaux,
24 Miti yote ya kondeni itajua kuwa Mimi Bwana ninaishusha miti mirefu na kuikuza miti mifupi kuwa miti mirefu. Mimi naikausha miti mibichi na kuifanya miti mikavu istawi. “‘Mimi Bwana nimesema, nami nitatenda.’”
Et tous les arbres des champs sauront que moi, l’Eternel, j’ai humilié un arbre élevé et élevé un arbre humble, j’ai desséché un arbre vert et lait fleurir un arbre sec; moi l’Eternel, j’ai parlé et agi."