< Ezekieli 17 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
And the word of the Lord came to me, saying:
2 “Mwanadamu, tega kitendawili, ukawaambie nyumba ya Israeli fumbo.
“Son of man, propose an enigma and describe a parable to the house of Israel,
3 Waambie hivi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tai mkubwa mwenye mabawa yenye nguvu, yaliyojaa manyoya marefu ya rangi mbalimbali, alikuja Lebanoni. Akatua kwenye kilele cha mwerezi,
and you shall say: Thus says the Lord God: A large eagle, with great wings and elongated pinions, full of feathers with many colors, came to Lebanon. And he took the kernel of the cedar.
4 akakwanyua ncha yake na kuichukua mpaka nchi ya wafanyabiashara, akaipanda huko katika mji wa wachuuzi.
He tore off the summit of its branches, and he transported it to the land of Canaan; he placed it in a city of merchants.
5 “‘Akachukua baadhi ya mbegu za nchi yako na kuziweka katika udongo wenye rutuba. Akazipanda kama mti umeao kando ya maji mengi,
And he took from the seed of the land and placed it in the ground for seed, so that it might take firm root above many waters; he placed it at the surface.
6 nazo zikaota na kuwa mzabibu mfupi, unaoeneza matawi yake. Matawi yake yakamwelekea huyo tai, mizizi yake ikabaki chini ya huo mzabibu. Kwa hiyo ukawa mzabibu na kutoa matawi na vitawi vyenye majani mengi.
And when it had germinated, it increased into a more extensive vine, low in height, with its branches facing toward itself. And its roots were underneath it. And so, it became a vine, and sprouted branches, and produced shoots.
7 “‘Lakini kulikuwa na tai mwingine mkubwa, mwenye mabawa yenye nguvu yaliyojaa manyoya. Tazama! Huu mzabibu ukatoa mizizi yake kumwelekea huyo tai kutoka mle kwenye shamba lile ulikopandwa na kutanda matawi yake kumwelekea kwa ajili ya kupata maji.
And there was another large eagle, with great wings and many feathers. And behold, this vine seemed to bend its roots towards him, extending its branches toward him, so that he might irrigate it from the garden of its germination.
8 Ulikuwa umepandwa katika udongo mzuri wenye maji mengi ili uweze kutoa matawi, kuzaa matunda na uweze kuwa mzabibu mzuri sana.’
It had been planted in a good land, above many waters, so that it would produce branches and bear fruit, so that it would become a large vine.
9 “Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, utastawi? Je, hautangʼolewa na kuondolewa matunda yake, ili uweze kunyauka? Majani yake mapya yanayochipua yote yatanyauka. Hautahitaji mkono wenye nguvu au watu wengi kuungʼoa na mizizi yake.
Speak: Thus says the Lord God: What if it does not prosper? Should he not pull up its roots, and strip off its fruit, and dry up all the branches that it has produced, and let it wither, though he is without a strong arm and without many people to pull it up by the root?
10 Hata kama utapandwa pengine, Je, utastawi? Je, hautanyauka kabisa wakati upepo wa mashariki utakapoupiga, yaani, hautanyauka kabisa katika udongo mzuri ambamo ulikuwa umestawi vizuri?’”
Behold, it has been planted. What if it does not prosper? Should it not be dried up when the burning wind touches it, and should it not wither in the garden of its germination?”
11 Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
And the word of the Lord came to me, saying:
12 “Waambie nyumba hii ya kuasi, ‘Je, mnajua hii ina maana gani?’ Waambie: ‘Mfalme wa Babeli alikwenda Yerusalemu na kumchukua mfalme na watu maarufu, akarudi nao na kuwaleta mpaka Babeli.
“Say to the provoking house: Do you not know what these things signify? Say: Behold, the king of Babylon arrives in Jerusalem. And he will take away its king and princes, and he will lead them away to himself in Babylon.
13 Ndipo akamchukua mmoja wa jamaa ya mfalme na kufanya mapatano naye, akamfanya aape. Akawachukua pia viongozi wa nchi,
And he will take one from the offspring of the king, and he will strike a pact with him and receive an oath from him. Moreover, he will take away the strong ones of the land,
14 ili kuudhoofisha ufalme huo, usiweze kuinuka tena, ila uweze kuendelea tu chini ya mapatano yake.
so that it may be a lowly kingdom, and may not lift itself up, and may instead keep his pact and serve it.
15 Lakini mfalme aliasi dhidi yake kwa kutuma wajumbe wake kwenda Misri ili kupatiwa farasi na jeshi kubwa. Je, atashinda? Je, atafanikiwa? Je, mtu afanyaye mambo kama hayo ataokoka? Je, atavunja mapatano na bado aokoke?
But, withdrawing from him, he sent messengers to Egypt, so that it would give him horses and many people. Should he who has done these things prosper and obtain safety? And should he who has broken the pact go free?
16 “‘Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, atafia huko Babeli, katika nchi ya mfalme aliyemketisha katika kiti cha enzi, ambaye alidharau kiapo chake na kuvunja mapatano yake.
As I live, says the Lord God, in the place of the king, who appointed him as king, whose oath he has made void, and whose pact he has broken, under which he was living with him, in the midst of Babylon, he shall die.
17 Farao na jeshi lake kubwa, na wingi wake wa watu hawataweza kusaidia chochote katika vita, wakati watakapozungukwa na jeshi ili kukatilia mbali maisha ya watu wengi.
And not with a great army, nor with many people will Pharaoh undertake a battle against him, when he will cast up ramparts and build defenses, in order to put to death many souls.
18 Alidharau kiapo kwa kuvunja Agano. Kwa sababu aliahidi kwa mkono wake mwenyewe na bado akafanya mambo haya yote, hataokoka.
For he has despised an oath, in that he broke the pact. And behold, he had given his hand. And so, since he has done all these things, he shall not escape.
19 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakika kama niishivyo, nitaleta juu ya kichwa chake kiapo changu, alichokidharau na Agano langu lile alilolivunja.
Because of this, thus says the Lord God: As I live, I will place upon his head the oath that he has spurned and the pact that he has betrayed.
20 Nitautandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa katika mtego wangu. Nitamleta mpaka Babeli na kutekeleza hukumu juu yake huko kwa kuwa hakuwa mwaminifu kwangu.
And I will spread my net over him, and he will be captured in my dragnet. And I will lead him into Babylon, and I will judge him there for the transgression by which he has despised me.
21 Askari wake wote wanaotoroka wataanguka kwa upanga, nao watakaonusurika watatawanyika katika pande zote za dunia. Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesema.
And all his fugitives, with all his procession, will fall by the sword. Then the remainder will be scattered into every wind. And you shall know that I, the Lord, have spoken.”
22 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi mwenyewe nitachukua chipukizi kutoka kwenye kilele cha juu sana cha mwerezi na kukipanda, nitavunja kitawi kichanga kutoka matawi yake ya juu kabisa na kukipanda juu ya mlima mrefu ulioinuka sana.
Thus says the Lord God: “I myself will take from the kernel of the exalted cedar, and I will establish it. I will tear off a tender twig from the top of its branches, and I will plant it on a mountain, lofty and exalted.
23 Katika vilele vya mlima mrefu wa Israeli nitakipanda, kitatoa matawi na kuzaa matunda na kuwa mwerezi mzuri sana. Ndege wa kila aina wataweka viota vyao ndani yake, nao watapata makazi katika kivuli cha matawi yake.
On the sublime mountains of Israel, I will plant it. And it shall spring forth in buds and bear fruit, and it shall be a great cedar. And all the birds will live under it, and every bird will make its nest under the shadow of its branches.
24 Miti yote ya kondeni itajua kuwa Mimi Bwana ninaishusha miti mirefu na kuikuza miti mifupi kuwa miti mirefu. Mimi naikausha miti mibichi na kuifanya miti mikavu istawi. “‘Mimi Bwana nimesema, nami nitatenda.’”
And all the trees of the regions will know that I, the Lord, have brought low the sublime tree, and have exalted the lowly tree, and have dried up the green tree, and have caused the dry tree to flourish. I, the Lord, have spoken and acted.”