< Ezekieli 17 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
HERRENs Ord kom til mig således:
2 “Mwanadamu, tega kitendawili, ukawaambie nyumba ya Israeli fumbo.
Menneskesøn, fremsæt en Gåde og tal i Lignelse til Israels Slægt;
3 Waambie hivi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tai mkubwa mwenye mabawa yenye nguvu, yaliyojaa manyoya marefu ya rangi mbalimbali, alikuja Lebanoni. Akatua kwenye kilele cha mwerezi,
sig: Så siger den Herre HERREN: Den store Ørn med vældigt Vingefang, lange Vinger, tæt Fjederham og brogede Farver kom til Libanon og tog Cederens Top;
4 akakwanyua ncha yake na kuichukua mpaka nchi ya wafanyabiashara, akaipanda huko katika mji wa wachuuzi.
Spidsen af dens Skud brød den af, bragte den til et Kræmmerland og satte den i en Handelsby.
5 “‘Akachukua baadhi ya mbegu za nchi yako na kuziweka katika udongo wenye rutuba. Akazipanda kama mti umeao kando ya maji mengi,
Så tog den en Plante der i Landet og plantede den i en Sædemark ved rigeligt Vand...",
6 nazo zikaota na kuwa mzabibu mfupi, unaoeneza matawi yake. Matawi yake yakamwelekea huyo tai, mizizi yake ikabaki chini ya huo mzabibu. Kwa hiyo ukawa mzabibu na kutoa matawi na vitawi vyenye majani mengi.
for at den skulde vokse og blive en yppig, lavstammet Vinstok, hvis Ranker skulde vende sig til den, og hvis Rødder skulde blive under den. Og den blev en Vinstok, som skød Grene og bredte sine Kviste.
7 “‘Lakini kulikuwa na tai mwingine mkubwa, mwenye mabawa yenye nguvu yaliyojaa manyoya. Tazama! Huu mzabibu ukatoa mizizi yake kumwelekea huyo tai kutoka mle kwenye shamba lile ulikopandwa na kutanda matawi yake kumwelekea kwa ajili ya kupata maji.
Men der var en anden stor Ørn med vældigt Vingefang og rig Fjederham; og se, Vinstokken bøjede sine Rødder imod den og strakte sine Ranker hen til den, for at den skulde give den mere Vand end Bedet, den stod i.
8 Ulikuwa umepandwa katika udongo mzuri wenye maji mengi ili uweze kutoa matawi, kuzaa matunda na uweze kuwa mzabibu mzuri sana.’
På en frugtbar Mark ved rigeligt Vand var den plantet for at skyde Grene, bære Frugt og blive en herlig Vinstok.
9 “Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, utastawi? Je, hautangʼolewa na kuondolewa matunda yake, ili uweze kunyauka? Majani yake mapya yanayochipua yote yatanyauka. Hautahitaji mkono wenye nguvu au watu wengi kuungʼoa na mizizi yake.
Sig derfor: Så siger den Herre HERREN: Mon det lykkes den? Mon den første Ørn ikke rykker dens Rødder op og afriver dens Frugt, så alle de friske Skud tørres hen? Der skal jo ingen kraftig Arm eller mange Folk til at rive den løs fra Roden.
10 Hata kama utapandwa pengine, Je, utastawi? Je, hautanyauka kabisa wakati upepo wa mashariki utakapoupiga, yaani, hautanyauka kabisa katika udongo mzuri ambamo ulikuwa umestawi vizuri?’”
Se, den er plantet, men mon det lykkes den? Mon den ikke, så snart Østenvinden når den, hentørres i Bedet, den voksede i?
11 Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
Og HERRENs Ord kom til mig således:
12 “Waambie nyumba hii ya kuasi, ‘Je, mnajua hii ina maana gani?’ Waambie: ‘Mfalme wa Babeli alikwenda Yerusalemu na kumchukua mfalme na watu maarufu, akarudi nao na kuwaleta mpaka Babeli.
Sig til den genstridige Slægt: Ved I ikke, hvad dette betyder? Sig: Babels Konge kom til Jerusalem, tog Kongen og Fyrsterne og førte dem med hjem til Babel.
13 Ndipo akamchukua mmoja wa jamaa ya mfalme na kufanya mapatano naye, akamfanya aape. Akawachukua pia viongozi wa nchi,
Derpå tog han entling af kongehuset og sluttede Pagt med ham og lod ham aflægge Ed. Landets Stormænd tog han dog med,
14 ili kuudhoofisha ufalme huo, usiweze kuinuka tena, ila uweze kuendelea tu chini ya mapatano yake.
for at Riget skulde holdes nede og ikke hovmode sig, men holde hans Pagt, at den måtte stå fast.
15 Lakini mfalme aliasi dhidi yake kwa kutuma wajumbe wake kwenda Misri ili kupatiwa farasi na jeshi kubwa. Je, atashinda? Je, atafanikiwa? Je, mtu afanyaye mambo kama hayo ataokoka? Je, atavunja mapatano na bado aokoke?
Men han faldt fra og sendte sine Bud til Ægypten, for at de skulde give ham Heste og Folk i Mængde. Mon det lykkes ham? Mon den, der bærer sig således ad, slipper godt derfra? Skal den, der bryder en Pagt, slippe fra det?
16 “‘Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, atafia huko Babeli, katika nchi ya mfalme aliyemketisha katika kiti cha enzi, ambaye alidharau kiapo chake na kuvunja mapatano yake.
Så sandt jeg lever, lyder det fra den Herre HERREN: Hvor den Konge bor, som gjorde ham til Konge, hvis Ed han lod hånt om, og hvis Pagt han brød, der hos ham i Babel skal han dø.
17 Farao na jeshi lake kubwa, na wingi wake wa watu hawataweza kusaidia chochote katika vita, wakati watakapozungukwa na jeshi ili kukatilia mbali maisha ya watu wengi.
Og Farao skal ikke hjælpe ham i Krigen med en stor Hær eller en talrig Skare, når der opkastes Stormvold og bygges Belejringstårne til Undergang for mange Mennesker.
18 Alidharau kiapo kwa kuvunja Agano. Kwa sababu aliahidi kwa mkono wake mwenyewe na bado akafanya mambo haya yote, hataokoka.
Thi han lod hånt om Eden og brød Pagten trods givet Håndslag; alt dette gjorde han; han skal ikke undslippe!
19 “‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakika kama niishivyo, nitaleta juu ya kichwa chake kiapo changu, alichokidharau na Agano langu lile alilolivunja.
Sig derfor: Så siger den Herre HERREN: Så sandt jeg lever: Min Ed, som han lod hånt om, og min Pagt, som han brød, vil jeg visselig lade komme over hans Hoved!
20 Nitautandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa katika mtego wangu. Nitamleta mpaka Babeli na kutekeleza hukumu juu yake huko kwa kuwa hakuwa mwaminifu kwangu.
Jeg breder mit Net over ham, så han fanges i mit Garn, og jeg bringer ham til Babel for der at gå i Rette med ham for den Troløshed, han viste mig.
21 Askari wake wote wanaotoroka wataanguka kwa upanga, nao watakaonusurika watatawanyika katika pande zote za dunia. Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesema.
Alle hans udvalgte Folk i alle hans Hære skal falde for Sværd, og de, der er til Rest, spredes for alle Vinde; og I skal kende, at jeg, HERREN, har talet.
22 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi mwenyewe nitachukua chipukizi kutoka kwenye kilele cha juu sana cha mwerezi na kukipanda, nitavunja kitawi kichanga kutoka matawi yake ya juu kabisa na kukipanda juu ya mlima mrefu ulioinuka sana.
Så siger den Herre HERREN: Så tager jeg selv en Gren af Cederens Top, af dens Skuds Spidser bryder jeg en tynd Kvist og planter den på et højt, knejsende Bjerg.
23 Katika vilele vya mlima mrefu wa Israeli nitakipanda, kitatoa matawi na kuzaa matunda na kuwa mwerezi mzuri sana. Ndege wa kila aina wataweka viota vyao ndani yake, nao watapata makazi katika kivuli cha matawi yake.
På Israels høje Bjerg vil jeg plante den, og den skal skyde Grene og bære Løv og blive en herlig Ceder. Under den skal alle vingede Fugle bygge, i dens Grenes Skygge skal de bo.
24 Miti yote ya kondeni itajua kuwa Mimi Bwana ninaishusha miti mirefu na kuikuza miti mifupi kuwa miti mirefu. Mimi naikausha miti mibichi na kuifanya miti mikavu istawi. “‘Mimi Bwana nimesema, nami nitatenda.’”
Og alle Markens Træer skal kende, at jeg, HERREN, nedbøjer det høje Træ og ophøjer det lave, udtørrer det friske Træ og lader det tørre blomstre. Jeg, HERREN, har talt og grebet ind.

< Ezekieli 17 >