< Ezekieli 15 >

1 Neno la Bwana likanijia kusema:
Et la parole du Seigneur me fut adressée, disant:
2 “Mwanadamu, je, ni vipi mti wa mzabibu unaweza kuwa bora zaidi kuliko tawi la mti mwingine wowote ndani ya msitu?
Fils d’un homme, que fera-t-on de l’arbre de la vigne entre tous les arbres des bois, qui sont parmi les arbres des forêts?
3 Je, mti wake kamwe huchukuliwa na kutengeneza chochote cha manufaa? Je, watu hutengeneza vigingi vya kuningʼinizia vitu kutokana na huo mti wake?
Est-ce qu’on prendra du bois de la vigne pour faire un ouvrage, ou en façonnera-t-on une cheville pour y suspendre un objet quelconque?
4 Nao baada ya kutiwa motoni kama nishati na moto ukateketeza ncha zote mbili na kuunguza sehemu ya kati, je, unafaa kwa lolote?
Voilà qu’on le met au feu, pour en être la proie; le feu consume les deux extrémités, et le milieu est réduit en cendre brûlante; est-ce qu’il sera utile pour un ouvrage?
5 Kama haukufaa kitu chochote ulipokuwa mzima, je, si zaidi sana sasa ambapo hauwezekani kufanyishwa chochote cha kufaa baada ya moto kuuchoma na kuuunguza?
Et même lorsqu’il était entier, il n’était propre à aucun ouvrage; combien plus, lorsque le feu l’aura dévoré et entièrement brûlé, on n’en fera aucun ouvrage?
6 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kama nilivyoutoa mti wa mzabibu miongoni mwa miti ya msituni kuwa nishati kwa ajili ya moto, hivyo ndivyo nitakavyowatendea watu waishio Yerusalemu.
À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur Dieu: Comme l’arbre de la vigne parmi les arbres des forêts, que j’ai mis au feu pour le dévorer, ainsi je livrerai les habitants de Jérusalem.
7 Nitaukaza uso wangu dhidi yao. Ingawa watakuwa wameokoka kwenye moto, bado moto utawateketeza. Nami nitakapoukaza uso wangu dhidi yao, ninyi mtajua kwamba Mimi ndimi Bwana.
Et je tournerai ma face contre eux; ils sortiront du feu, et le feu les consumera; et vous saurez que je suis le Seigneur, lorsque j’aurai tourné ma face contre eux,
8 Nitaifanya nchi kuwa ukiwa kwa sababu wamekuwa si waaminifu, asema Bwana Mwenyezi.”
Et que j’aurai rendu la terre inaccessible et désolée, parce qu’ils se sont montrés prévaricateurs, dit le Seigneur Dieu.

< Ezekieli 15 >