< Ezekieli 15 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
La parole du Seigneur me fut adressée en ces termes:
2 “Mwanadamu, je, ni vipi mti wa mzabibu unaweza kuwa bora zaidi kuliko tawi la mti mwingine wowote ndani ya msitu?
"Fils de l’homme, qu’adviendra-t-il du bois de la vigne parmi tous les bois, du sarment qui se trouve dans les arbres de la forêt?
3 Je, mti wake kamwe huchukuliwa na kutengeneza chochote cha manufaa? Je, watu hutengeneza vigingi vya kuningʼinizia vitu kutokana na huo mti wake?
Est-ce qu’on en prendra du bois pour le travailler, en fera-t-on des chevilles, pour y suspendre quelque ustensile?
4 Nao baada ya kutiwa motoni kama nishati na moto ukateketeza ncha zote mbili na kuunguza sehemu ya kati, je, unafaa kwa lolote?
Voici qu’on l’a donné en aliment au feu; les deux bouts, le feu les a consumés et le dedans en est noirci: pourra-t-il être de quelque usage?
5 Kama haukufaa kitu chochote ulipokuwa mzima, je, si zaidi sana sasa ambapo hauwezekani kufanyishwa chochote cha kufaa baada ya moto kuuchoma na kuuunguza?
Quoi! Quand il était intact, on ne l’employait à rien; maintenant que le feu l’a consumé et noirci, il serait encore de quelque usage?
6 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kama nilivyoutoa mti wa mzabibu miongoni mwa miti ya msituni kuwa nishati kwa ajili ya moto, hivyo ndivyo nitakavyowatendea watu waishio Yerusalemu.
C’Est pourquoi, ainsi a dit le Seigneur Dieu, tel le bois de la vigne parmi les bois de la forêt, que j’ai donné en aliment au feu, ainsi je traite les habitants de Jérusalem.
7 Nitaukaza uso wangu dhidi yao. Ingawa watakuwa wameokoka kwenye moto, bado moto utawateketeza. Nami nitakapoukaza uso wangu dhidi yao, ninyi mtajua kwamba Mimi ndimi Bwana.
Je dirigerai ma face contre eux: ils sont sortis du feu et le feu les consumera, et vous saurez que je suis l’Eternel quand je tournerai ma face contre eux.
8 Nitaifanya nchi kuwa ukiwa kwa sababu wamekuwa si waaminifu, asema Bwana Mwenyezi.”
Et je ferai de leur terre une désolation, parce qu’ils se sont montrés infidèles," dit le Seigneur Dieu.