< Ezekieli 15 >
1 Neno la Bwana likanijia kusema:
And there is a word of YHWH to me, saying,
2 “Mwanadamu, je, ni vipi mti wa mzabibu unaweza kuwa bora zaidi kuliko tawi la mti mwingine wowote ndani ya msitu?
“Son of man, What is the vine-tree more than any tree? The vine-branch that has been, Among trees of the forest?
3 Je, mti wake kamwe huchukuliwa na kutengeneza chochote cha manufaa? Je, watu hutengeneza vigingi vya kuningʼinizia vitu kutokana na huo mti wake?
Is wood taken from it to use for work? Do they take a pin of it to hang any vessel on it?
4 Nao baada ya kutiwa motoni kama nishati na moto ukateketeza ncha zote mbili na kuunguza sehemu ya kati, je, unafaa kwa lolote?
Behold, it has been given to the fire for fuel, The fire has eaten its two ends, And its midst has been scorched! Is it profitable for work?
5 Kama haukufaa kitu chochote ulipokuwa mzima, je, si zaidi sana sasa ambapo hauwezekani kufanyishwa chochote cha kufaa baada ya moto kuuchoma na kuuunguza?
Behold, in its being perfect it is not used for work, How much less when fire has eaten of it, And it is scorched, Has it been used yet for work?”
6 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kama nilivyoutoa mti wa mzabibu miongoni mwa miti ya msituni kuwa nishati kwa ajili ya moto, hivyo ndivyo nitakavyowatendea watu waishio Yerusalemu.
Therefore, thus said Lord YHWH: “As the vine-tree among trees of the forest, That I have given to the fire for fuel, So I have given the inhabitants of Jerusalem.
7 Nitaukaza uso wangu dhidi yao. Ingawa watakuwa wameokoka kwenye moto, bado moto utawateketeza. Nami nitakapoukaza uso wangu dhidi yao, ninyi mtajua kwamba Mimi ndimi Bwana.
And I have set My face against them, They have gone forth from the fire, And the fire consumes them, And you have known that I [am] YHWH, In My setting My face against them.
8 Nitaifanya nchi kuwa ukiwa kwa sababu wamekuwa si waaminifu, asema Bwana Mwenyezi.”
And I have made the land a desolation, Because they have committed a trespass,” A declaration of Lord YHWH!