< Ezekieli 14 >

1 Baadhi ya wazee wa Israeli walinijia na kuketi mbele yangu.
E vieram a mim alguns homens dos anciãos de Israel, e se assentaram diante de mim.
2 Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
Então veiu a mim a palavra do Senhor, dizendo:
3 “Mwanadamu, watu hawa wameweka sanamu katika mioyo yao na kuweka vitu viovu vya kukwaza mbele ya macho yao. Je, kweli niwaruhusu waniulize jambo lolote?
Filho do homem, estes homens levantaram os seus idolos sobre os seus corações, e o tropeço da sua maldade pozeram diante da sua face; porventura pois devéras me perguntam?
4 Kwa hiyo sema nao uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati Mwisraeli yeyote anapoweka sanamu moyoni mwake na kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akaenda kwa nabii, Mimi Bwana nitamjibu peke yangu sawasawa na ukubwa wa ibada yake ya sanamu.
Portanto falla com elles, e dize-lhes: Assim diz o Senhor Jehovah: Qualquer homem da casa de Israel, que levantar os seus idolos sobre o seu coração, e o tropeço da sua maldade pozer diante da sua face, e vier ao propheta, eu, o Senhor, vindo elle, lhe responderei conforme a multidão dos seus idolos;
5 Nitafanya jambo hili ili kukamata tena mioyo ya watu wa Israeli, ambao wote wameniacha kwa ajili ya sanamu zao.’
Para apanhar a casa de Israel no seu coração, porquanto todos se apartaram de mim para seguirem os seus idolos.
6 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tubuni! Geukeni kutoka kwenye sanamu zenu na mkatae matendo yenu yote ya machukizo!
Portanto dize á casa de Israel: Assim diz o Senhor Jehovah: Convertei-vos, e deixae-vos converter dos vossos idolos; e desviae os vossos rostos de todas as vossas abominações.
7 “‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi katika Israeli anapojitenga nami na kujiwekea sanamu katika moyo wake na kwa hivyo kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akamwendea nabii kuuliza shauri kwangu, mimi Bwana nitamjibu mwenyewe.
Porque qualquer homem da casa de Israel, e dos estrangeiros que peregrinam em Israel, que se alienar de mim, e levantar os seus idolos sobre o seu coração, e pozer o tropeço da sua maldade diante do seu rosto, e vier ao propheta, para me consultar por meio d'elle, eu, o Senhor, lhe responderei por mim mesmo.
8 Nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo na kumwadhibu na kumfanya ishara kwa watu. Nitamkatilia mbali kutoka watu wangu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
E porei o meu rosto contra o tal homem, e o assolarei para que sirva de signal e de dictado, e arrancal-o-hei do meio do meu povo: e sabereis que eu sou o Senhor.
9 “‘Naye nabii kama atakuwa ameshawishika kutoa unabii, Mimi Bwana nitakuwa nimemshawishi nabii huyo, nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yake na kumwangamiza kutoka miongoni mwa watu wangu Israeli.
E quando o propheta se deixar persuadir, e fallar alguma coisa, eu, o Senhor, persuadi esse propheta; e estenderei a minha mão contra elle, e destruil-o-hei do meio do meu povo Israel,
10 Watachukua hatia yao, nabii atakuwa na hatia sawa na yule mtu aliyekuja kuuliza neno kwake.
E levarão a sua maldade: como fôr a maldade do que pergunta, assim será a maldade do propheta;
11 “‘Ndipo watu wa Israeli hawataniacha tena, wala kujitia unajisi tena kwa dhambi zao zote. Ndipo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao, asema Bwana Mwenyezi.’”
Para que a casa de Israel não se desvie mais d'após mim, nem se contamine mais com todas as suas transgressões: então elles me serão por povo, e eu lhes serei por Deus, diz o Senhor Jehovah.
12 Neno la Bwana likanijia kusema,
Veiu ainda a mim a palavra do Senhor, dizendo:
13 “Mwanadamu, kama nchi itanitenda dhambi kwa kutokuwa waaminifu nami nikinyoosha mkono wangu dhidi yake kukatilia mbali upatikanaji wake wa chakula na kuipelekea njaa na kuua watu wake na wanyama wao,
Filho do homem, quando uma terra peccar contra mim, gravemente rebellando, então estenderei a minha mão contra ella, e lhe quebrarei o sustento do pão, e enviarei contra ella fome, e arrancarei d'ella homens e animaes:
14 hata kama watu hawa watatu: Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa ndani ya nchi hiyo, ndio hao tu wangeweza kujiokoa wenyewe kwa uadilifu wao, asema Bwana Mwenyezi.
Ainda que estivessem no meio d'ella estes tres homens, Noé, Daniel e Job, elles pela sua justiça livrariam sómente a sua alma, diz o Senhor Jehovah.
15 “Au kama nikipeleka wanyama pori katika nchi hiyo yote na kuifanya isiwe na watoto, nayo ikawa ukiwa kwamba hakuna mtu apitaye katika nchi hiyo kwa sababu ya wanyama pori,
Se eu fizer passar pela terra as más bestas, e ellas a despojarem de filhos, que ella seja assolada, e ninguem possa passar por ella por causa das bestas;
16 hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao peke yao wangeokolewa, lakini nchi ingekuwa ukiwa.
E estes tres homens estivessem no meio d'ella, vivo eu, diz o Senhor Jehovah, que nem a filhos nem a filhas livrariam; elles só ficariam livres, e a terra seria assolada.
17 “Au kama nikileta upanga dhidi ya nchi hiyo na kusema, ‘Upanga na upite katika nchi yote,’ nami nikiua watu wake na wanyama wao,
Ou, se eu trouxer a espada sobre a tal terra, e disser: Espada, passa pela terra: e eu arrancar d'ella homens e bestas:
18 hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao wenyewe tu wangeokolewa.
Ainda que aquelles tres homens estivessem n'ella, vivo eu, diz o Senhor Jehovah, que nem filhos nem filhas livrariam, senão elles só ficariam livres.
19 “Au kama nikipeleka tauni katika nchi hiyo na kumwaga ghadhabu yangu juu yake kwa njia ya kumwaga damu, kuua watu wake na wanyama wao,
Ou, se eu enviar a peste sobre a tal terra, e derramar o meu furor sobre ella com sangue, para arrancar d'ella homens e bestas:
20 hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kumwokoa mwana wala binti. Wao wangeweza kujiokoa wenyewe tu kwa uadilifu wao.
Ainda que Noé, Daniel e Job estivessem no meio d'ella, vivo eu, diz o Senhor Jehovah, que nem um filho nem uma filha livrariam a sua alma, mas só elles livrarão as suas proprias almas pela sua justiça.
21 “Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Itakuwa vibaya kiasi gani nitakapopeleka dhidi ya Yerusalemu hukumu zangu nne za kutisha, yaani, upanga, njaa, wanyama pori na tauni, ili kuua watu wake na wanyama wao!
Porque assim diz o Senhor Jehovah: Quanto mais, se eu enviar os meus quatro maus juizos, a espada, e a fome, e as más bestas, e a peste, contra Jerusalem, para arrancar d'ella homens e bestas?
22 Lakini watakuwepo wenye kuokoka, wana na binti wataletwa kutoka nje ya nchi hiyo. Watawajia ninyi, nanyi mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, mtafarijika kuhusu maafa niliyoleta juu ya Yerusalemu, kwa ajili ya yale yote niliyoleta juu yake.
Porém eis que alguns dos que escaparem ficarão de resto n'ella, que serão tirados para fóra, assim filhos como filhas; eis que elles sairão a vós, e vereis o seu caminho e os seus feitos; e ficareis consolados do mal que eu trouxe sobre Jerusalem, e de tudo o que trouxe sobre ella.
23 Mtafarijika wakati mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, kwa kuwa mtajua kwamba sikufanya lolote ndani yake bila sababu, asema Bwana Mwenyezi.”
E vos consolarão, quando virdes o seu caminho e os seus feitos; e sabereis que não fiz sem razão tudo quanto fiz n'ella, diz o Senhor Jehovah.

< Ezekieli 14 >