< Ezekieli 14 >

1 Baadhi ya wazee wa Israeli walinijia na kuketi mbele yangu.
Quelques-uns des anciens d'Israël vinrent auprès de moi et s'assirent devant moi.
2 Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
Et la parole de Yahweh me fut adressée en ces termes:
3 “Mwanadamu, watu hawa wameweka sanamu katika mioyo yao na kuweka vitu viovu vya kukwaza mbele ya macho yao. Je, kweli niwaruhusu waniulize jambo lolote?
" Fils de l'homme, ces gens-là ont dressé dans leur cœur leurs infâmes idoles, et ils mettent devant leur face le scandale qui les fait pécher: me laisserai-je interroger par eux?
4 Kwa hiyo sema nao uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati Mwisraeli yeyote anapoweka sanamu moyoni mwake na kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akaenda kwa nabii, Mimi Bwana nitamjibu peke yangu sawasawa na ukubwa wa ibada yake ya sanamu.
C'est pourquoi parle-leur et dis-leur: Ainsi parle le Seigneur Yahweh: Quiconque de la maison d'Israël dresse en son cœur ses infâmes idoles et met devant sa face le scandale qui le fait pécher, s'il vient vers le prophète, moi, Yahweh, je lui répondrai par moi-même, comme le mérite la multitude de ses idoles,
5 Nitafanya jambo hili ili kukamata tena mioyo ya watu wa Israeli, ambao wote wameniacha kwa ajili ya sanamu zao.’
afin de prendre la maison d'Israël par son propre cœur, elle qui, avec toutes ses idoles infâmes, s'est détournée de moi.
6 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tubuni! Geukeni kutoka kwenye sanamu zenu na mkatae matendo yenu yote ya machukizo!
C'est pourquoi dis à la maison d'Israël: Ainsi parle le Seigneur Yahweh: Revenez et détournez-vous de vos idoles infâmes, et détournez votre face de toutes vos abominations.
7 “‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi katika Israeli anapojitenga nami na kujiwekea sanamu katika moyo wake na kwa hivyo kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akamwendea nabii kuuliza shauri kwangu, mimi Bwana nitamjibu mwenyewe.
Car quiconque de la maison d'Israël ou des étrangers séjournant en Israël se détourne de moi, dresse dans son cœur ses infâmes idoles et met devant sa face le scandale qui le fait pécher, s'il vient vers le prophète afin qu'il m'interroge pour lui, moi Yahweh je lui répondrai moi-même.
8 Nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo na kumwadhibu na kumfanya ishara kwa watu. Nitamkatilia mbali kutoka watu wangu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Je dirigerai ma face contre cet homme, je le détruirai pour faire de lui un signe et un proverbe; je le retrancherai du milieu de mon peuple, et vous saurez que je suis Yahweh.
9 “‘Naye nabii kama atakuwa ameshawishika kutoa unabii, Mimi Bwana nitakuwa nimemshawishi nabii huyo, nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yake na kumwangamiza kutoka miongoni mwa watu wangu Israeli.
Et si le prophète se laisse séduire et qu'il prononce quelque parole, c'est moi, Yahweh, qui aurai séduit ce prophète; et j'étendrai ma main sur lui, et je l'exterminerai du milieu de mon peuple d'Israël.
10 Watachukua hatia yao, nabii atakuwa na hatia sawa na yule mtu aliyekuja kuuliza neno kwake.
Ils porteront ainsi la peine de leur iniquité, — telle l'iniquité de celui qui interroge, telle l'iniquité du prophète, —
11 “‘Ndipo watu wa Israeli hawataniacha tena, wala kujitia unajisi tena kwa dhambi zao zote. Ndipo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao, asema Bwana Mwenyezi.’”
afin que la maison d'Israël ne s'égare plus loin de moi, et qu'elle ne se souille plus par toutes ses transgressions. Alors ils seront mon peuple, et moi je serai leur Dieu, — oracle du Seigneur Yahweh. "
12 Neno la Bwana likanijia kusema,
La parole de Yahweh me fut adressée en ces termes:
13 “Mwanadamu, kama nchi itanitenda dhambi kwa kutokuwa waaminifu nami nikinyoosha mkono wangu dhidi yake kukatilia mbali upatikanaji wake wa chakula na kuipelekea njaa na kuua watu wake na wanyama wao,
" Fils de l'homme, si un pays péchait contre moi par révolte, et si j'étendais ma main sur lui en brisant pour lui le bâton du pain, et si je lui envoyais la famine, en exterminant hommes et bêtes,
14 hata kama watu hawa watatu: Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa ndani ya nchi hiyo, ndio hao tu wangeweza kujiokoa wenyewe kwa uadilifu wao, asema Bwana Mwenyezi.
et qu'il y eut ces trois hommes au milieu de ce pays, Noé, Daniel et Job, ... eux sauveraient leur âme par leur justice, — oracle du Seigneur Yahweh.
15 “Au kama nikipeleka wanyama pori katika nchi hiyo yote na kuifanya isiwe na watoto, nayo ikawa ukiwa kwamba hakuna mtu apitaye katika nchi hiyo kwa sababu ya wanyama pori,
Si je faisais passer dans le pays des bêtes malfaisantes, et qu'il fût dépeuplé, et qu'il devint un désert où personne ne passerait à cause des bêtes,
16 hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao peke yao wangeokolewa, lakini nchi ingekuwa ukiwa.
et qu'il y eût ces trois hommes au milieu de ce pays, je suis vivant, — oracle du Seigneur Yahweh: Ils ne sauveraient ni fils ni filles; eux seuls seraient sauvés, mais le pays serait dévasté.
17 “Au kama nikileta upanga dhidi ya nchi hiyo na kusema, ‘Upanga na upite katika nchi yote,’ nami nikiua watu wake na wanyama wao,
Ou si je faisais venir l'épée sur ce pays, et que je dise: Que l'épée passe sur le pays!... en exterminant hommes et bêtes,
18 hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao wenyewe tu wangeokolewa.
et qu'il y eût ces trois hommes au milieu de ce pays, je suis vivant, — oracle du Seigneur Yahweh: Ils ne sauveraient ni fils, ni filles; eux seuls seraient sauvés.
19 “Au kama nikipeleka tauni katika nchi hiyo na kumwaga ghadhabu yangu juu yake kwa njia ya kumwaga damu, kuua watu wake na wanyama wao,
Ou si j'envoyais la peste sur ce pays, et que je répandisse sur lui mon courroux dans le sang, en exterminant hommes et bêtes,
20 hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kumwokoa mwana wala binti. Wao wangeweza kujiokoa wenyewe tu kwa uadilifu wao.
et que Noé, Daniel et Job fussent au milieu de ce pays, je suis vivant, — oracle du Seigneur Yahweh: Ils ne sauveraient ni fils, ni filles, mais eux sauveraient leur âme par leur justice.
21 “Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Itakuwa vibaya kiasi gani nitakapopeleka dhidi ya Yerusalemu hukumu zangu nne za kutisha, yaani, upanga, njaa, wanyama pori na tauni, ili kuua watu wake na wanyama wao!
Car ainsi parle le Seigneur Yahweh: Même quand j'aurai envoyé contre Jérusalem mes quatre châtiments terribles, l'épée, la famine, les bêtes malfaisantes et la peste, en exterminant hommes et bêtes,
22 Lakini watakuwepo wenye kuokoka, wana na binti wataletwa kutoka nje ya nchi hiyo. Watawajia ninyi, nanyi mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, mtafarijika kuhusu maafa niliyoleta juu ya Yerusalemu, kwa ajili ya yale yote niliyoleta juu yake.
voici qu'il y aura un reste qui échappera, qui sortira de la ville, des fils et des filles. Voici qu'ils viendront vers vous; vous verrez leur conduite et leurs œuvres, et vous vous consolerez du mal que j'aurai fait venir sur Jérusalem, de tout ce que j'aurai fait venir sur elle.
23 Mtafarijika wakati mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, kwa kuwa mtajua kwamba sikufanya lolote ndani yake bila sababu, asema Bwana Mwenyezi.”
Ils vous consoleront, quand vous verrez leur conduite et leurs œuvres, et vous saurez que ce n'est pas sans cause que j'aurai fait tout ce que je lui aurai fait, — oracle du Seigneur Yahweh. "

< Ezekieli 14 >